Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/03 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Desemba 8
  • Juma Linaloanza Desemba 15
  • Juma Linaloanza Desemba 22
  • Juma Linaloanza Desemba 29
  • Juma Linaloanza Januari 5
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 12/03 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Desemba 8

Wimbo 221

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Novemba 15 na Amkeni! la Novemba 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa.

Dak. 20: “Ni Nini Kinacholeta Umoja wa Kweli Miongoni mwa Wakristo?”a Mnapozungumzia fungu la 5, waombe wasikilizaji wasimulie mambo waliyoona katika makusanyiko, ujenzi, au kazi ya kutoa misaada wakati wa msiba, ambayo yanaonyesha umoja wetu wa Kikristo.

Dak. 15: “Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya Mwaka wa 2004.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Tia ndani maelezo kutoka katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2003.

Wimbo 108 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 15

Wimbo 71

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote wapitie Sanduku la Swali lenye kichwa “Je, Uko Tayari kwa Hali ya Dharura?” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1999 na wale walio na video Transfusion-Alternative Health Care—Meeting Patient Needs and Rights waitazame ili kujitayarisha kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi wa juma la Desemba 29. Zungumzieni sanduku “Tafadhali Watembelee Bila Kukawia.” Waonyeshe wasikilizaji fomu ya S-70 ikiwa ipo. Taja mipango ya pekee ya utumishi wa shambani kwa ajili ya Desemba 25 na Januari 1.

Dak. 15: Funzo la Kibinafsi—Tendo la Ibada. Hotuba kutoka gazeti la Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 2000, ukurasa wa 14-15, fungu la 6-10.

Dak. 20: “Wasaidie Wale ‘Walio na Mwelekeo Unaofaa.’”b Tumia maswali yaliyo kwenye makala. Rudia madokezo ya jinsi ya kufanya ziara za kurudia yaliyo kwenye ukurasa wa 3 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1997.

Wimbo 42 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 22

Wimbo 10

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1 na Amkeni! la Desemba 8. Wakumbushe wote kuhusu Mkutano wa Utumishi wa pekee juma lijalo ambapo tutapitia video Patient Needs and Rights ikiwa inapatikana, na kuzungumzia na kugawa kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 18: “Kuwatafuta Wale Wanaostahili.”c Fanya mazungumzo yafaane na hali za kwenu. Watu wanapatikana lini nyumbani? Kuhubiri saa za jioni-jioni kumekuwa na matokeo gani? Tunaweza kutumia njia gani kuwasiliana na watu ambao mara nyingi hawapatikani nyumbani?

Wimbo 209 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 29

Wimbo 200

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wahubiri wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Desemba. Taja toleo la vichapo la Januari.

Dak. 17: Zungumzia Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1999, “Je, Uko Tayari kwa Hali ya Dharura?” au mahali ambapo video inapatikana zungumzia “Video Inayoonyesha Njia Muhimu ya Matibabu.” Sehemu hii ishughulikiwe na mzee anayestahili. Soma Matendo 15:28, 29, kisha ukazie kifupi kwamba sababu kuu inayofanya Wakristo wakatae kutiwa damu mishipani ni kuheshimu sheria ya Mungu kuhusu utakatifu wa damu. Kisha zungumzia video, Patient Needs and Rights ukitumia maswali yaliyo kwenye makala. Malizia kwa kusoma fungu la mwisho.

Dak. 23: Kukabili Matibabu Bila Hofu. Hotuba itolewe na mzee anayestahili akitumia muhtasari kutoka ofisi ya tawi. Pitia mambo makuu katika sanduku “Maandalizi ya Kutusaidia Tujiepushe na Damu.”

Wimbo 182 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Januari 5

Wimbo 103

Taarifa: Makutaniko yasibadili kamwe Mkutano wao wa Utumishi juma linaloanza Januari 5 na kuufanya kabla ya tarehe hiyo isipokuwa tu wawe na ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Katika kila kutaniko, nyongeza kuhusu kusanyiko yapaswa kuzungumziwa katika Mkutano wa Utumishi juma ambalo imeratibiwa isipokuwa kuwe na kusanyiko la mzunguko juma hilo.

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 15: Kazi Yenu Si ya Bure. (1 Kor. 15:58) Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Panga mapema wahubiri ambao wamekuwa watendaji kwa muda mrefu wasimulie jinsi kazi ya kuhubiri ilivyofanywa miaka ya zamani. Kulikuwa na wahubiri wangapi kutanikoni? Eneo la kutaniko lilikuwa kubwa kadiri gani? Watu waliitikiaje ujumbe wa Ufalme? Ulikabili upinzani gani? Kumekuwa na ongezeko gani katika kazi ya Ufalme kwenye eneo lenu miaka ambayo imepita?

Dak. 25: “Makusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova ya 2004 ya ‘Tembea Pamoja na Mungu.’” Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Unapozungumzia fungu la 3 omba baadhi ya wasikilizaji wasome mambo yote yanayotajwa katika sanduku kwenye ukurasa wa 4. Watie moyo wote wafanye mipango ya kusanyiko mapema iwezekanavyo.

Wimbo 7 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki