Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwyp makala 76
  • Kwa Nini Uhudhurie Mikutano Kwenye Jumba la Ufalme?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Uhudhurie Mikutano Kwenye Jumba la Ufalme?
  • Vijana Huuliza
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni nini hutendeka katika Jumba la Ufalme?
  • Kwa nini unapaswa kuhudhuria?
  • Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Hapa Ni Mahali Petu pa Ibada
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mipango ya Mahali pa Ibada
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kwa Nini Tunapaswa Kukutanika Pamoja kwa Ajili ya Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Vijana Huuliza
ijwyp makala 76
Kijana anawatazama watu wakitembea kuelekea Jumba la Ufalme

VIJANA HUULIZA

Kwa Nini Uhudhurie Mikutano Kwenye Jumba la Ufalme?

Mashahidi wa Yehova hufanya mikutano mara mbili kila juma katika majengo yao ya ibada yanayoitwa, Majumba ya Ufalme. Ni nini hutendeka huko, na utapata manufaa gani kwa kuhudhuria?

  • Ni nini hutendeka katika Jumba la Ufalme?

  • Kwa nini unapaswa kuhudhuria?

  • Vijana wenzako wanasema nini

Ni nini hutendeka katika Jumba la Ufalme?

Jumba la Ufalme ni kituo cha kujifunzia ambacho hukazia hasa kuwaandalia watu elimu ya Biblia inayofaa. Mikutano hiyo inaweza kukusaidia:

  • kujifunza kweli kumhusu Mungu.

  • kuelewa maana ya matukio ya sasa.

  • kuboresha utu wako.

  • kupata marafiki wanaofaa kabisa.

Je, wajua? Jengo la ibada la Mashahidi wa Yehova linaitwa Jumba la Ufalme kwa sababu wao huzungumzia sana kuhusu Ufalme wa Mungu katika mikutano yao.​—Mathayo 6:​9, 10; 24:14; Luka 4:​43.

Kwa nini unapaswa kuhudhuria?

Habari utakayopata itakusaidia. Kanuni za Biblia zinazozungumziwa kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova zitakusaidia ‘ujipatie uelewaji.’ (Methali 4:5) Hilo linamaanisha kwamba Biblia inaweza kukusaidia kufanya maamuzi mazuri maishani. Pia, inaweza kukusaidia kupata majibu ya maswali muhimu zaidi maishani, kama vile:

  • Ni nini kusudi la uhai?

  • Je, Mungu ndiye anayepaswa kulaumiwa kwa sababu ya kuteseka kwetu?

  • Ni nini hutupata tunapokufa?

Vifuatavyo ni baadhi ya vichwa vya hotuba zinazotolewa katika mikutano yetu ya mwisho-juma:

  • Kwa Nini Uongozwe na Biblia?

  • Unaweza Kupata Wapi Msaada Nyakati za Taabu?

  • Mambo Ambayo Ufalme wa Mungu Unatufanyia Sasa.

“Mwanafunzi mwenzangu alihudhuria mkutano mmoja. Aliketi pamoja na familia yetu, na tulitumia vitabu nilivyokuwa nimebeba. Baadaye, aliniambia kwamba alivutiwa sana na maelezo ambayo watu walitoa wakati wa sehemu za maswali na majibu. Pia alisema kwamba kanisani kwao hawana machapisho ya kujifunzia kama yetu.”​—Brenda.

Je, wajua? Hakuna kiingilio kwenye Jumba la Ufalme, wala sadaka hazikusanywi.

Utatiwa moyo na watu utakaokutana nao. Biblia inasema kwamba sababu moja Wakristo wanapaswa kukutana ni ili ‘kutiana moyo.’ (Waebrania 10:24, 25) Inaburudisha sana kuwa na marafiki wanaofaa na wanaomtanguliza Mungu na watu wengine katika ulimwengu huu uliojaa ubinafsi.

“Baada ya siku ndefu, mimi hujihisi nikiwa nimechoka na kuhuzunika, lakini sikuzote watu kwenye Jumba la Ufalme hunifanya nijihisi vizuri. Ninaporudi nyumbani baada ya mkutano, mimi huwa na furaha na ninajihisi nikiwa tayari kuanza siku nyingine.”​—Elisa.

Je, wajua? Kuna makutaniko zaidi ya 120,000 ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote yanayokutanika katika majumba zaidi ya 60,000. Kila mwaka, kwa wastani, Majumba ya Ufalme karibu 1,500 hujengwa ili kushughulikia ongezeko la wahudhuriaji.a

Vijana wenzako wanasema nini

Jessica

“Nilipokuwa katika shule ya sekondari, mwanafunzi mwenzangu aliambatana nami kwenye mikutano kadhaa, naye alivutiwa na jinsi watu wa umri mbalimbali walivyokuwa wakijifunza Biblia pamoja. Hivi karibuni mwajiri wangu alihudhuria, naye alishangazwa na jinsi tulivyorejelea Biblia mara nyingi. Kuona jinsi watu wengine walivyothamini mikutano yetu kulinichochea niithamini hata zaidi!”​—Jessica.

Timothy

“Mikutano huniletea kitulizo kutokana na mahangaiko ya kila siku. Tunajifunza jinsi ya kuwa na maisha yenye kuridhisha, jinsi ya kuwa watu wazuri zaidi, na mambo mengine mengi. Sikuzote mimi huondoka kwenye Jumba la Ufalme nikiwa nimetiwa moyo na kuburudishwa.”​—Timothy.

Jacob

“Mwanamume mmoja niliyemkaribisha kwenye mkutano wetu alisema hivi baadaye: ‘Nilihudhuria ili tu kuona ikiwa ningeweza kukosoa mambo mnayoamini. Kumbe mambo ambayo mimi niliamini ndiyo yenye kasoro!’ Pia alivutiwa na jinsi Mashahidi wa Yehova walivyomwonyesha urafiki. Alisema hivi: ‘Hata ingawa ilikuwa mara ya kwanza kwetu kukutana, mlinitendea kana kwamba mmenijua kwa miaka mingi!’”​—Jacob.

Madison

“Kuna pindi ambapo nimejiambia, ‘Nitaondoka punde tu baada ya mikutano.’ Lakini mikutano inapoendelea, hisia hiyo hutoweka. Baada ya mikutano, mimi hujikuta nikizungumza na watu na hata sikumbuki sababu iliyonifanya nitake kuondoka haraka. Nisingekuwa na marafiki wazuri ikiwa nisingekuwa nikihudhuria mikutano.”​—Madison.

a Ili upate mahali ambapo mikutano inafanyiwa, nenda kwenye ukurasa wa “Mikutano ya Kutaniko ya Mashahidi wa Yehova” na ubofye “Pata Eneo Lililo Karibu Nawe.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki