Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/97 uku. 3
  • Kwa Nini Twafuliza Kurudi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Twafuliza Kurudi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Endelea Kuhubiri Ule Ufalme
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Sababu Inayotufanya Turudi Tena na Tena
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Kwa Nini Twendelee Kuhubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Endelea Kuhubiri!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 5/97 uku. 3

Kwa Nini Twafuliza Kurudi?

1 Je, umepata kujiuliza swali hilo, labda ulipokuwa unajitayarisha siku ya kwenda katika utumishi wa shambani? Katika sehemu fulani ambazo maeneo yetu yamehubiriwa mara nyingi, wenye nyumba wengine huenda wakatutambua na hutufukuza haraka. Wengine huenda wakatuambia tusirudi. Hata hivyo kuna sababu nyingi zenye nguvu zinazofanya tufulize kurudi.

2 Kwanza, twaamriwa tufulize kuhubiri ujumbe wa Ufalme hadi mwisho uje. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Nabii Isaya alitaka kujua angeendelea na kuhubiri kwake hata lini. Jibu alilopokea limerekodiwa kwenye Isaya 6:11. Ni wazi kwamba—aliambiwa alipaswa kufuliza kurudi kwa watu akiwa na ujumbe wa Mungu. Hali kadhalika leo, ingawa huenda wengine wakatufukuza, Yehova anatazamia twendelee kuwatembelea watu wanaoishi katika eneo letu. (Eze. 3:10, 11) Hili ni daraka takatifu ambalo tumekabidhiwa.—1 Kor. 9:17.

3 Sababu nyingine ya sisi kuendelea kurudi ni kwamba hii hutupa fursa ya kuonyesha kina cha ujitoaji wetu kwa Yehova. (1 Yoh. 5:3) Mbali na hilo, tunapofikiria kwa uzito wakati ujao wa wanadamu, twawezaje kujizuia kuonya jirani zetu kwa upendo? (2 Tim. 4:2; Yak. 2:8) Kuwa kwetu waaminifu katika kutimiza mgawo wetu huandaa fursa za tena na tena kwao kuitikia ujumbe wa Mungu wa wokovu, ili wasiweze kusema hawakuonywa.—Eze. 5:13.

4 Kwa kuongezea, hatujui kamwe ni lini watu fulani watakuwa wamebadilika moyoni. Waweza kuchochewa na badiliko katika hali zao za kibinafsi, msiba katika familia yao, au hali za ulimwengu ambazo zawasababisha wafikiri kwa uzito juu ya wakati wao ujao. Kisha kwa upande ule mwingine, jambo fulani tusemalo milangoni pao huenda likaamsha itikio lenye kupendeza. (Mhu. 9:11; 1 Kor. 7:31) Pia, watu huhama. Huenda tukapata wakazi wapya katika eneo letu ambao wataitikia habari njema—labda watu wachanga walio watu wazima wachanga ambao sasa wanaishi peke yao na ambao hufikiria kwa uzito juu ya kusudi lao maishani.

5 Je, tutafuliza kurudi? Ndiyo! Maandiko yanatupa kichocheo cha kutosha turudie watu tena na tena. Mwishowe, kazi ya kuhubiri imalizikapo, Yehova atatubariki kwa jitihada yetu yenye kuendelea katika huduma, naye atabariki wale ambao wameitikia kwa shukrani habari njema za Ufalme.—1 Tim. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki