Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/07 uku. 4
  • Sababu Inayotufanya Turudi Tena na Tena

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu Inayotufanya Turudi Tena na Tena
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • “Tumehubiri Eneo Letu Mara Nyingi Sana!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Usichoke Kutenda Yaliyo Mema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kwa Nini Twendelee Kuhubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kwa Nini Twafuliza Kurudi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 7/07 uku. 4

Sababu Inayotufanya Turudi Tena na Tena

1 Katika sehemu nyingi, sisi humaliza eneo haraka sana. Tunarudi kwenye nyumba zilezile tena na tena, hata ingawa wenye nyumba walituambia hawapendezwi na ujumbe wetu. Kwa nini tunaendelea kuwatembelea wale ambao hawakuwa wameitikia vizuri wakati uliopita?

2 Upendo kwa Yehova na Watu: Sababu kubwa ya sisi kuendelea kuhubiri ni upendo wetu kwa Yehova. Mioyo yetu inatusukuma tuendelee kuwaambia wengine kuhusu Mungu wetu mkuu. (Luka 6:45) Upendo wetu kwa Yehova unatusukuma kutii amri zake na kuwasaidia wengine kufanya vivyo hivyo. (Met. 27:11; 1 Yoh. 5:3) Kuendelea kwetu kwa uaminifu katika huduma hii hakutegemei itikio la watu. Hata ingawa Wakristo wa karne ya kwanza waliteswa, waliendelea kuhubiri “bila kuacha.” (Mdo. 5:42) Badala ya kuruhusu watu wanaokataa ujumbe wetu watuvunje moyo, sisi tunaendelea kusimama imara tukionyesha kina cha upendo na ujitoaji wetu kwa Yehova.

3 Sababu nyingine inayotufanya tuendelee kuhubiri ni upendo wetu kwa jirani. (Luka 10:27) Yehova hataki yeyote aangamizwe. (2 Pet. 3:9) Hata kwenye eneo linalohubiriwa mara kwa mara, bado watu wanaotaka kumtumikia Yehova wanapatikana. Kwa mfano, huko Guadeloupe, ambako kila mtu 1 kati ya 56 ni Shahidi wa Yehova, watu 214 walibatizwa mwaka jana. Karibu watu 20,000 walihudhuria Ukumbusho, hiyo ni sawa na mtu 1 kati ya watu 22 katika nchi hiyo ya Guadeloupe!

4 Mabadiliko Katika Eneo: Eneo hubadilika kila mara. Mahali ambapo hatukusikilizwa vizuri wakati uliopita, huenda mtu fulani katika familia hiyo ambaye hajawahi kusikia ujumbe wetu akafungua mlango na kutusikiliza. Au huenda tunaweza kukuta wakazi wapya ambao wanapendezwa. Watoto ambao wazazi wao hawapendezwi hukua na kuondoka nyumbani. Huenda watu kama hao wakapenda kusikiliza ujumbe wa Ufalme.

5 Watu hubadilika pia. Wakati fulani mtume Paulo alikuwa “mkufuru na mtesaji na mtu mwenye dharau.” (1 Tim. 1:13) Vivyo hivyo, wengi wanaomtumikia Yehova leo wakati fulani walikuwa hawapendezwi na ukweli. Huenda wengine hata walipinga habari njema wakati fulani. Kadiri hali za ulimwengu zinavyobadilika, huenda zikawachochea watu waliokuwa wakipinga au wenye ubaridi wasikilize. Wengine husukumwa kusikiliza baada ya kukumbana na jambo fulani, kama vile kifo cha mtu fulani katika familia, kupoteza kazi, matatizo ya kifedha, au ugonjwa.

6 Mfumo huu unakaribia kwisha, lakini kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha inaongezeka. (Isa. 60:22) Hivyo, tunaendelea kuhubiri kwa shauku na kujitahidi kuwa na mtazamo mzuri. Huenda mtu tutakayezungumza naye tena atasikiliza. Tunapaswa kuendelea kuhubiri! ‘Kwa kufanya hivyo tutajiokoa sisi wenyewe na wale wanaotusikiliza pia.’—1 Tim. 4:16.

[Maswali ya Funzo]

1. Ni swali gani linalozuka kuhusiana na kazi yetu ya kuhubiri?

2. Sababu ya msingi ya sisi kuendelea katika huduma yetu ni ipi?

3. Upendo wetu kuelekea watu unatuchocheaje tuendelee kuhubiri?

4. Eneo linaweza kubadilikaje?

5. Ni nini kinachoweza kuwachochea watu waitikie?

6. Kwa nini tunapaswa kuendelea kuhubiri kwa shauku?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki