Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Septemba 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: “Baraka ya Yehova Hututajirisha.” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.—Ona Insight, Buku la 2, ukurasa wa 804, fungu la 6-7, mahali kichapo hicho kinapopatikana.
Dak. 20: “Tumia Matukio ya Karibuni Kuamsha Upendezi.” Mazungumzo na wasikilizaji na maonyesho. Taja matukio kadhaa ya karibuni ambayo yametokeza upendezi kwenu. Matukio hayo yamezusha mahangaiko gani ya wakati ujao? Ukitumia kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 12, toa madokezo ya jinsi ya kutayarisha utangulizi utakaoongoza kwenye mazungumzo ya Biblia. Panga uwe na maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri.
Wimbo 224 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Tulitimiza Nini Mwaka Uliopita? Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi. Zungumzia mambo makuu kutoka katika ripoti ya kutaniko ya mwaka wa utumishi wa 2000. Toa pongezi kwa mambo mazuri yaliyotimizwa. Taja sehemu ambazo zahitaji kufanyiwa maendeleo. Kazia yale ambayo kutaniko limetimiza kuhusu hudhurio la mikutano, kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia, na kuwa wa kawaida katika utumishi wa shambani. Eleza miradi inayofaa kwa mwaka ujao.
Dak. 20: “Maisha Yamo Hatarini!” Mazungumzo na wasikilizaji. Kazia maandiko yaliyotajwa katika makala.
Wimbo 30 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 25
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Septemba. Zungumzia Sanduku la Swali.
Dak. 15: “Mpango Wetu wa Kugawanya Vichapo Uliorahisishwa.” Tia ndani onyesho la mhubiri mwenye uzoefu akionyesha kikamili jinsi ya kutoa vichapo kutia ndani kumwomba mwenye nyumba kama angependa kutoa mchango kwa ajili ya kazi yetu.
Dak. 15: Magazeti Yetu Hayapotezi Thamani Yake. Wewe hufanyaje matoleo ya zamani ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanapolundamana? Wahubiri wengine huyatupa, wakifikiri kwamba habari hizo si za kisasa tena. Badala yake, Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1993, ukurasa wa 3, ilitusihi tubebe matoleo ya zamani na kuyatoa inapofaa. Unaweza kuchukua makala zinazofaa, ambazo zavutia wanaume, wanawake, wataalamu, wazee, vijana; kisha uyatoe magazeti hayo fursa inapotokea. Toa onyesho la jinsi makala zinavyoweza kuteuliwa na kutolewa. Simulia mambo yaliyoonwa yenye mafanikio ambayo wahubiri wamepata walipokuwa wakiangusha magazeti ya zamani.
Wimbo 115 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 2
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Julisha kutaniko juu ya ugawanyaji wa pekee uliopangwa kwa ajili ya trakti Habari za Ufalme Na. 36, ambao utaanza Jumatatu, Oktoba 16, na kuendelea hadi Ijumaa, Novemba 17. Sihi watu wote, kutia ndani wachanga na wapya, washiriki kikamili. Viongozi wa funzo wanapaswa kuanza sasa kutia moyo na kupanga kila mmoja katika kikundi chao ashiriki kwa bidii kadiri awezavyo. Tia ndani mambo yaliyoonwa yenye kujenga kuhusu ugawanyaji uliopita wa Habari za Ufalme.
Dak. 15: “Je, Nihame?” Hotuba itolewe na mzee. Eleza kwa nini twahitaji kutumia utambuzi tunapoamua kuhamia kwingine. Zungumzia jinsi ya kutumia shauri lipatikanalo kwenye Mithali 22:3. Tia ndani maelezo ya kutahadhari yaliyo kwenye Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1988, ukurasa wa 22.
Dak. 15: Mambo Yaliyoonwa Juu ya Kuanzisha Mazungumzo. Katika programu ya Mkutano wa Utumishi ya juma la Septemba 11, ilipendekezwa kwamba tubuni utangulizi mbalimbali wa matukio ya sasa ili kuamsha upendezi na kuanzisha mazungumzo katika huduma. Alika wasikilizaji wasimulie matokeo mazuri ambayo wamefurahia kufikia sasa kwa kutumia madokezo hayo.
Wimbo 205 na sala ya kumalizia.