Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
Pitio la vitabu vikiwa vimefungwa kuhusu habari iliyozungumziwa katika migawo ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwa juma la Septemba 4 hadi Desemba 18, 2000. Tumia karatasi tofauti ya kuandika majibu kwa maswali mengi kadiri uwezavyo kwa wakati uliogawiwa.
[Taarifa: Wakati wa pitio la kuandika, ni Biblia pekee inayoweza kutumiwa kujibu swali lolote. Marejezo yanayofuata maswali ni kwa ajili ya utafiti wako wa kibinafsi. Nambari za ukurasa na fungu huenda zisipatikane katika marejezo yote kwenye Mnara wa Mlinzi.]
Jibu kila ya taarifa zifuatazo Kweli au Si Kweli:
1. Daudi alimzuia Abishai asimwue Shimei kwa sababu Daudi alikuwa na hatia ya mashtaka yaliyofanywa dhidi yake na Shimei. (2 Sam. 16:5-13) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w99-SW 5/1 uku. 32 fu. 3.] Si kweli. Daudi hakuwa na hatia kuhusiana na mashtaka ya Shimei, na alikinza kwa unyenyekevu kishawishi cha kulipiza kisasi. Badala yake, aliacha jambo hilo mikononi mwa Yehova.
2. Dhamiri iliyo safi, iliyozoezwa vizuri huongoza kwenye uhusiano wa kibinafsi ulio mchangamfu na Mungu, na pia ni muhimu kwa wokovu wetu. (Ebr. 10:22; 1 Pet. 1:15, 16) [w98-SW 9/1 uku. 4 fu. 4] Kweli.
3. Masimulizi ya 1 Wafalme yana thamani ya kihistoria tu kwa Mkristo kwa sababu baada ya kifo cha Solomoni ni wafalme 2 tu kati ya wafalme 14 waliotawala Israeli na Yuda waliofaulu kufanya yaliyo haki machoni pa Yehova. [si-SW uku. 64 fu. 1] Si Kweli. Masimulizi ya 1 Wafalme yana maonyo, unabii mbalimbali, na vifananishi, ‘vilivyopuliziwa na vinavyofaa’ na yanahusiana moja kwa moja na kichwa kikuu cha Ufalme cha “kila Andiko.” (2 Tim. 3:16, 17)
4. Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu waweza kulinganishwa na utawala wa miaka 40 wenye amani na ufanisi wa Solomoni. (1 Fal. 4:24, 25, 29) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w90-SW 6/1 uku. 6 fu. 5.] Kweli.
5. Ni wazi kwamba Abiya ndiye aliyekuwa mwabudu mwaminifu wa Yehova peke yake kutoka kwa nyumba ya Yeroboamu kwa sababu alizikwa kwa heshima. (1 Fal. 14:10, 13) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w95-SW 4/1 uku. 12 fu. 11.] Si Kweli. Bado alikufa kama vile wengine wa nyumba mbovu ya Yeroboamu, lakini Yehova alithamini angalau “jambo lililo jema” aliloona katika Abiya na akatenda kulingana nalo.
6. Mtu anakuwa mtumishi aliyekomaa wa Mungu anapopata ubatizo wa Kikristo. [w98-SW 10/1 uku. 28 fu. 2] Si Kweli. Ubatizo huashiria mwanzo wa maisha ya Mkristo; ni lazima bado Mkristo aliyebatizwa ‘azidi kusonga mbele kwenye ukomavu,’ na kuwa “mwanamume aliyekua kabisa,” kwa kuongeza ujuzi sahihi. (Ebr. 6:1; Efe. 4:13)
7. Yehova alimwezesha Eliya awe na ujasiri upitao wa kibinadamu na kumlinda asiwe na hofu. (1 Fal. 18:17, 18, 21, 40, 46) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w98-SW 1/1 uku. 31 fu. 2.] Si Kweli. Eliya alikuwa “mtu mwenye hisia kama zetu” na alipatwa na hofu na hangaiko. (Yak. 5:17; 1 Fal. 19:4)
8. Hekalu la Solomoni ni jengo mashuhuri si kwa sababu ya utukufu na fahari yake tu bali pia kwa sababu lilifananisha kimbele hekalu la kiroho la Yehova lenye utukufu mwingi zaidi. [si-SW uku. 69 fu. 26] Kweli.
9. Yaelekea majeshi ya Shamu yalipigwa kwa upofu wa akili baada ya agizo la Elisha kwa kuwa wangeweza kumwona Elisha lakini hawangeweza kutambua alikuwa nani. (2 Fal. 6:18, 19) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona si-SW uku. 71 fu. 10.] Kweli.
10. Kuweka “ushuhuda,” kunakotajwa katika 2 Wafalme 11:12, kulikuwa ishara ya ufananisho iliyoonyesha kwamba fasiri ya mfalme juu ya Sheria ya Mungu ilikuwa jambo lisiloweza kubadilishwa na ambalo lilipasa kutiiwa. [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w91-SW 2/1 uku. 31 fu. 6.] Si Kweli. Kwa kuwa mfalme alipaswa kusoma na kutumia Sheria ya Mungu katika maisha yake yote, huenda hiyo ilionyesha kwamba hata yeye hakuwa na cheo cha juu kiasi cha kutofuata Sheria ya Yehova, au Ushuhuda. (Kum. 17:18-20)
Jibu maswali yafuatayo:
11. Kupatana na 1 Yohana 2:15-17, wazazi wanaohofu Mungu wanapaswa kuwahimiza watoto wao waepuke nini wanapowaongoza kuchagua kazi ya kimwili inayofaa? [w98-SW 7/15 uku. 5 fu. 3] Wazazi wanapaswa kuwahimiza watoto wao wasifuatie umashuhuri na ufanisi katika ‘ulimwengu ambao unapitilia mbali.’
12. Ni nini linalomaanishwa kwenye 2 Samweli 18:8, andiko linalosema: “Msitu ukala watu wengi kuliko wale walioliwa na upanga”? [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w87-SW 3/15 uku. 31 fu. 2.] Yaelekea, hilo larejezea wanaume wa Absalomu waliokimbizwa, waliokuwa wakikimbia kwa woga kupitia msitu huo wenye miamba-miamba, na labda kutumbukia katika mabonde yaliyofichika, na kunaswa katika vichaka vya chini vilivyosongamana sana. (2 Sam. 18:9)
13. Ni nani leo wanaoweza kulinganishwa na watu wa ukoo wa Goliathi, Warefaimu, nao wanajitahidi kufanya nini? (2 Sam. 21:15-22) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w89-SW 1/1 uku. 20 fu. 8.] Mabingwa wa kisiasa wa ulimwengu wa Shetani waweza kulinganishwa na Warefaimu. Kupitia tawala zinazotumia mabavu, wanadhihaki vikali Yehova na kujaribu kuchokoza mashahidi wake wajitiishe. (Maana yatosha)
14. Ni kanuni gani ya Biblia yenye manufaa tunayojifunza kutoka kwenye 2 Samweli 6:6, 7? [si-SW uku. 63 fu. 30] Makusudio mema hayabadili matakwa ya Mungu.
15. Ni kanuni gani muhimu tunayoweza kujifunza kutokana na kisa kinachohusisha mtu aliyeuawa kwa sababu ya kukiuka Sabato? (Hes. 15:35) [w98-SW 9/1 uku. 20 fu. 2] Mkristo apaswa kupanga ifaavyo mambo atakayotanguliza na kuweka ibada ya Yehova mahali pa kwanza kabisa.
16. Ni kwa kufanya nini tutaweza kumwiga malkia wa Sheba, aliyesafiri kutoka mbali ili kusikia “hekima ya Sulemani”? (1 Fal. 10:1-9) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w99-SW 7/1 uku. 31 fu. 1-2.] Kwa kutafakari kielelezo na mtazamo wa akili wa Solomoni Mkubwa Zaidi, Yesu, na kwa kufuata amri yake kuhusu kufanya wanafunzi. (Mt. 12:42)
17. Kulingana na 1 Wafalme 17:3, 4, 7-9, 17-24, Eliya alionyesha imani katika Yehova katika njia gani tatu? [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w92-SW 4/1 uku. 19 fu. 5.] Eliya alionyesha imani katika Yehova kwa kumtegemea ili kumwandalia mahitaji ya maisha, kwa kufuata mielekezo Yake, na kwa kumtegemea Yeye ili atakase jina Lake.
18. Kwa nini Nabothi hakuwa akionyesha ukaidi tu alipokataa kuuza shamba lake la mizabibu kwa Ahabu? (1 Fal. 21:2, 3) [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w97-SW 8/1 uku. 13 fu. 18.] Nabothi alikuwa mwaminifu-mshikamanifu kwa Mungu na alitii takwa la Sheria ya Kimusa kwamba Mwisraeli yeyote hakupaswa kuuza mali ya urithi wa ardhi kwa umilele. (Law. 25:23-28)
19. Ni jinsi gani maneno ya 2 Wafalme 6:16 yametumika kuwatia moyo watumishi wa Yehova leo? [Usomaji wa Biblia kila juma; ona w98-SW 6/15 uku. 18 fu. 5.] Yamewatia moyo watumishi wa Mungu waendelee kutoa ushahidi licha ya jitihada za kutaka kuwanyamazisha kupitia vitisho, ogofyo, jeuri ya kimwili, vifungo vya gerezani, kambi za mateso, na hata kifo.
20. Ni katika njia gani Wakristo wa kweli leo wanapaswa kujihadhari na usimoni? [w98-SW 11/15 uku. 28 fu. 5] Wakristo wapaswa kujihadhari wasitafute mapendeleo zaidi kwa kurairai sana au kuwapa zawadi kwa wingi wale wawezao kuwapa mapendeleo zaidi. Kwa upande mwingine, wale wawezao kuwapa mapendeleo hayo wanapaswa kuepuka kupendelea wale wenye uwezo—na mara nyingi wenye hamu—ya kuwapa zawadi kwa wingi.
Toa neno au fungu la maneno yanayohitajiwa kukamilisha kila moja ya taarifa zifuatazo:
21. Kumhofu mwanadamu hakupaswi kumfanya Mkristo wa kweli ashiriki katika desturi zisizompendeza Mungu. (Mit. 29:25; Mt. 10:28) [2, w98-SW 7/15 uku. 20 fu. 5]
22. Alipokuwa akitoa ushahidi mbele za Mfalme Agripa, Paulo alitumia busara, akikazia hoja ambazo yeye na Agripa walikubaliana kwa ujumla. (Mdo. 26:2, 3, 26, 27) [7, w98-SW 9/1 uku. 31 fu. 3]
23. Kwa kuwa Mungu haonekani, huenda wengine wakahisi hana utu, lakini kujifunza Biblia mara nyingi na kwa makini zaidi kutamwezesha mtu ‘kumwona Yeye asiyeonekana.’ (Ebr. 11:27) [9, w98-SW 9/15 uku. 21 fu. 3-4]
24. Kama ionyeshwavyo na kisa cha jenerali Msiria Naamani, nyakati nyingine manufaa kubwa hupatikana kwa unyenyekevu kidogo tu. [14, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w99-SW 2/1 uku. 3 fu. 6 hadi uku. 4 fu. 1.]
25. Kama vile moyo wa Yehonadabu ulivyokuwa pamoja na Mfalme Yehu, umati mkubwa leo humkiri kwa moyo wote na kushirikiana na Yehu Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo, anayewakilishwa duniani na Wakristo watiwa-mafuta. (2 Fal. 10:15, 16) [16, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w98-SW 1/1 uku. 13 fu. 5-6.]
Chagua jibu sahihi katika kila moja ya taarifa zifuatazo:
26. Ni (Shetani; Yehova; Yoabu) aliyemchochea Daudi afanye dhambi ‘kuwahesabu Israeli.’ (2 Sam. 24:1) [4, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w92-SW 7/15 uku. 5 fu. 2.]
27. Kupatana na 1 Wafalme 8:1 na Mhubiri 1:1, Solomoni alikusanya watu ili (kujenga hekalu; kufuatia maadui wa Israeli; kumwabudu Yehova). [7, Usomaji wa Biblia kila juma; ona si-SW uku. 112 fu. 3.]
28. Kile kipindi cha miaka 20 ambacho Solomoni alijenga hekalu na nyumba yake Yerusalemu chalingana na kipindi cha marekebisho ya kimafundisho na ya kitengenezo kilichoanza mwaka wa (1919; 1923; 1931) na kilichoisha mwaka wa (1938; 1942; 1950). (1 Fal. 9:10) [8, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w92-SW 3/1 uku. 20 sanduku.]
29. Neno “mbingu” kama linavyotumiwa katika 2 Wafalme 2:11 larejezea (makao ya kiroho ya Mungu; ulimwengu wote mzima halisi; angahewa ya dunia, ambako ndege huruka na pepo huvuma). [13, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w97-SW 9/15 uku. 15 sanduku.]
30. (Herode Mkuu; Kaisari Augusto; Kaisari Tiberio) ndiye aliyeagiza usajili uliofanya Yesu azaliwe Bethlehemu badala ya Nazareti. [16, w98-SW 12/15 uku. 7 sanduku]
Patanisha maandiko yafuatayo na taarifa zilizoorodheshwa chini:
Zab. 15:4; 2 Sam. 12:28; 2 Sam. 15:18-22; 2 Fal. 3:11; Kol. 3:13
31. Ukichwa katika mpango wa kitheokrasi wa Yehova wapasa kuheshimiwa. [2 Sam. 12:28] [4, si-SW uku. 63 fu. 30]
32. Uaminifu-mshikamanifu kwa tengenezo la Yehova na wawakilishi wake lazima udumishwe. [2 Sam. 15:18-22] [4, si-SW uku. 63 fu. 30]
33. Kuthamini rehema ya Yehova kwaweza kumchochea mtu ajizuie na kufunika kasoro mbalimbali. [Kol. 3:13] [11, w98-SW 11/1 uku. 6 fu. 4]
34. Ni pendeleo kuonyesha ukaribishaji-wageni na kuhudumia kwa unyenyekevu watumishi waaminifu wa Yehova walio katika utumishi wa pekee. [2 Fal. 3:11] [13, Usomaji wa Biblia kila juma; ona w97-SW 11/1 uku. 30 fu. 8.]
35. Mtu anayemhofu Mungu hujitahidi kadiri awezavyo kutimiza aliyosema kwa kulipa madeni yake, hata ikiwa hali zisizotazamiwa zafanya iwe vigumu kuliko alivyotarajia. [Zab. 15:4] [15, w98-SW 11/15 uku. 27 fu. 1]