Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp20 Na. 1 kur. 12-13
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
  • Habari Zinazolingana
  • Mafundisho ya Yesu Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Ufalme wa Mungu Watawala
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
wp20 Na. 1 kur. 12-13
Dunia kama inavyoonekana angani na miale ya jua ikiimulika

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasali hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Ufalme wa Mungu ni nini? Unafanya nini? Na kwa nini tunapaswa kusali uje?

Yesu ni Mfalme wa Ufalme wa Mungu.

Luka 1:31-33: “Nawe utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi, na Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

Ufalme ulikuwa kichwa kikuu cha mahubiri ya Yesu.

Mathayo 9:35: “Yesu akaondoka ili kutembelea majiji na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya Ufalme na kuponya kila aina ya ugonjwa na kila aina ya udhaifu.”

Yesu aliwaeleza wanafunzi wake kuhusu ishara ambayo ingewasaidia kutambua Ufalme umekaribia kuja.

Mathayo 24:7: “Kwa maana taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali.”

Leo wanafunzi wa Yesu wanahubiri kuhusu Ufalme wa Mungu duniani kote.

Mathayo 24:14: “Na hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na ndipo ule mwisho utakapokuja.”

Ukweli kuhusu Ufalme wa Mungu

Makao. Ufalme wa Mungu ni serikali halisi iliyosimamishwa na Mungu mbinguni.​—DANIELI 2:44; MATHAYO 4:17.

Kusudi. Ufalme wa Mungu utabadili dunia iwe paradiso. Katika paradiso, wanadamu wataishi kwa amani na upatano na hawatakuwa wagonjwa wala kufa.​—ZABURI 37:11, 29.

[Picha katika ukurasa wa 13]

Watawala. Mungu alimchagua Yesu awe Mfalme mbinguni pamoja na watawala wenza 144,000, ambao wamenunuliwa kutoka duniani.​—LUKA 1:30-33; 12:32; UFUNUO 14:1, 3.

Raia. Raia wa Ufalme huo wataishi duniani, na kwa hiari watajitiisha chini ya utawala wa Yesu na kutii sheria za Ufalme. —MATHAYO 7:21.

Kwa Nini Yesu Ndiye Mfalme Anayefaa Kuwatawala Wanadamu?

  • Alipokuwa duniani Yesu alithibitisha kwamba atakuwa mtawala mwenye uwezo na upendo kwa sababu

  • Aliwahangaikia maskini.​—LUKA 14:13, 14.

  • Alichukia ufisadi na ukosefu wa haki.​—MATHAYO 21:12, 13.

  • Alidhibiti nguvu za asili.​—MARKO 4:39.

  • Aliwalisha maelfu ya watu.​—MATHAYO 14:19-21.

  • Aliwahurumia wagonjwa na aliwaponya wote waliokuwa wakiteseka.​—MATHAYO 8:16.

Aliwafufua wafu.​—YOHANA 11:43, 44.

[Picha katika ukurasa wa 13]

  • Jinsi Ufalme wa Mungu Unavyoweza Kukunufaisha

  • Unaweza kuwa na maisha yenye furaha sasa ukikubali kuwa raia wa Ufalme wa Mungu. Kwa mfano, raia wa Ufalme

  • ‘Hufuatilia amani pamoja na watu wote.’​—WAEBRANIA 12:14.

Wanafurahia amani na umoja katika familia kwa sababu wenzi wa ndoa wanapendana na kuheshimiana.​—WAEFESO 5:22, 23, 33.

Wana furaha na wanaishi maisha yenye kuridhisha kwa sababu “[wanatambua] uhitaji wao wa kiroho.”​—MATHAYO 5:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki