Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/01 kur. 3-4
  • Julisheni Jina la Yehova na Matendo Yake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Julisheni Jina la Yehova na Matendo Yake
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Lihubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Tangazeni Kotekote Sifa Bora za Yehova
    Huduma ya Ufalme—2007
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 2/01 kur. 3-4

Julisheni Jina la Yehova na Matendo Yake

1 “Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake, wajulisheni watu matendo yake. . . . Na ufurahi moyo wao wamtafutao BWANA [“Yehova,” NW].” (Zab. 105:1, 3) Mtunga-zaburi aliyeandika maneno hayo alipata shangwe kubwa kwa kuwaambia watu juu ya Yehova na “matendo” yake. Matendo gani? Bila shaka yale yanayohusiana na ufalme wa Mungu wenye utukufu na “habari njema za wokovu wake.”—Zab. 96:2, 3, NW; 145:11, 12.

2 Tukaribiapo majira ya Ukumbusho ya mwaka wa 2001, tuna sababu nyingi za kushangilia juu ya jinsi ambavyo Yehova ametutendea. Kwa nini? Bila shaka, Mlo wa Jioni wa Bwana ni mwadhimisho mkubwa zaidi kwa Wakristo wote wa kweli. Hii ndiyo pindi yenye umuhimu zaidi, kusudi zaidi, na utaratibu wenye kufuatwa zaidi kuliko pindi nyinginezo. Huo ndio wakati wa sisi sote kukumbuka yale ambayo Yehova na Yesu wamefanya ili kutuandalia njia ya wokovu. Si ajabu kwamba wakati wa majira ya Ukumbusho, sisi hutazamia kuona ongezeko la utendaji katika utumishi wa shambani tujulishapo “habari njema za wokovu”!

3 Je, Utakuwa Painia-Msaidizi? Katika mwezi wa Aprili mwaka jana, kilele cha watu 4,869 walikuwa mapainia-wasaidizi. Je, mwaka huu, twaweza kufanya Machi na Aprili iwe miezi ya pekee ya kuongeza utendaji katika huduma. Mwezi wa Machi una Jumamosi tano, na wa Aprili una Jumapili tano. Kwa kupanga mahubiri siku nzima miishoni mwa juma, wahubiri wengi wanaofanya kazi wakati wote wameona kwamba wanaweza kuwa mapainia-wasaidizi. Ili kufikia takwa la saa 50 kwa mwezi, painia-msaidizi anahitaji kuhubiri muda wa saa 12 kila juma. Fikiria kwa uangalifu ratiba zilizodokezwa katika sanduku lililoko kwenye ukurasa wa 4. Je, mojawapo ya ratiba hizo zitafaana na hali zako? Kama sivyo unaweza kutengeneza ratiba yako mwenyewe ya painia-msaidizi mwezi wa Machi na Aprili.

4 Wazee wanapaswa kuanza sasa kuchochea watu waunge mkono na wawe na shauku ya kuongeza utumishi. Mwaka jana katika kutaniko moja ambapo wazee na watumishi wa huduma wote walijiandikisha wawe mapainia-wasaidizi, wahubiri 64 kati ya 121 walifanya upainia msaidizi mwezi wa Aprili! Pia kutaniko lilifurahia kuona wahubiri sita wasiobatizwa wakianza kutoa ripoti zao mwezi wa Machi na Aprili. Kwa kweli, utakuwa wakati bora zaidi kwa watoto na wapya kuuliza wazee kama wanastahili kuanza kushiriki katika kazi ya kuhubiri hadharani.

5 Jitihada ya Ziada Huleta Baraka: Makutaniko yanayoweka miradi ya pekee na kujitahidi zaidi hupata baraka tele. Makutaniko mengine huenda yakakazia hasa kuhubiri maeneo yasiyohubiriwa kwa ukawaida, kukazia aina tofauti ya mahubiri, au kuhubiri kwa njia ya simu—njia yenye matokeo zaidi ya kufikia watu wasiokuwepo nyumbani na wakazi wasiofikiwa kwa urahisi.

6 Je, ugonjwa au uzee wapaswa kumzuia mtu asishiriki kadiri awezavyo katika utumishi? Haiwi hivyo katika visa vyote. Kwa mfano, dada mzee mwenye umri wa miaka 86 ambaye anaugua kansa alifanya upainia msaidizi mwezi wa Aprili hata ingawa miguu yake ilikuwa imevimba. Kuhubiri kwa njia ya simu kulifanya iwezekane kwake kushiriki kikamili shambani, nako kuliongeza sifa kwa Yehova. Hiyo ilikuwa na matokeo yenye kusisimua kwake na kwa kutaniko.

7 Jitayarishe Vizuri kwa Ajili ya Ukumbusho: Mwaka huu Ukumbusho utakuwa Aprili 8. Kwa kuwa siku hiyo itakuwa Jumapili, itawawezesha wengi kuhudhuria. Huenda tukawa na hudhurio kubwa kuliko wakati wowote uliopita ikiwa tutafanya sehemu yetu kwa (1) kuhudhuria sisi wenyewe na (2) kualika wengine wajiunge nasi kwenye Ukumbusho. Tualike akina nani?

8 Chunguza rekodi zako za utumishi wa shambani na kutafuta majina ya wale ambao wamependezwa na kweli kwa kiasi fulani, hata ingawa huwatembelei kwa ukawaida. Majuma mawili au matatu kabla ya Ukumbusho, jitahidi kuwatembelea wote na kuwaalika kwenye Ukumbusho. Hali zako zikiruhusu, jitolee kuwapa usafiri wale ambao wangependa kuhudhuria.

9 Makutaniko kadhaa hayatumii vikaratasi vyote vya mwaliko wa Ukumbusho. Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuhakikisha kwamba vikaratasi vya mwaliko vinapatikana mapema vya kutosha ili vigawanywe. Huenda ukataka kuchapa au kuandika kwa unadhifu wakati na mahali pa Ukumbusho sehemu ya chini ya kikaratasi hicho. Au huenda ukatia ndani kikaratasi cha kukaribisha watu kinachoonyesha mahali pa Jumba la Ufalme kama hapo ndipo Ukumbusho wenu utakapofanyiwa. Kumbuka kwamba, kwa kawaida ni mhubiri binafsi anayepaswa kumpa mwenye nyumba kikaratasi cha mwaliko wa Ukumbusho.

10 Wakumbuke Wasiotenda: Ni shangwe kuona mwanafunzi mpya anapojiweka wakfu kwa Yehova na kuonyesha wakfu wake kwa uzamisho wa maji. Ingawa hivyo, kila mwaka wengine miongoni mwetu huacha kushirikiana nasi, nao huacha kuwaambia wengine juu ya jina la Yehova na matendo yake. Tuna sababu nzuri ya kuhangaika. Ijapokuwa watu wengi wasiotenda hawajaacha kweli, huenda ikawa wameacha kuhubiri kwa sababu ya kuvunjika moyo, matatizo ya kibinafsi, au mahangaiko mengine ya maisha. (Mt. 13:20-22) Wale ambao wamedhoofika kiroho wanahitaji msaada kurudi kwenye kutaniko kabla hawajamezwa na mfumo wa Shetani. (1 Pet. 5:8) Majira haya ya Ukumbusho twataka kufanya jitihada za pekee kuwasaidia wahubiri wote wanaostahili ambao hawatendi ili warudie tena kuhubiri habari njema.

11 Mwandishi wa kutaniko apaswa kuwajulisha viongozi wa funzo la kitabu kuhusu wahubiri wowote wasiotenda walio katika vikundi vyao. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko itaongoza katika kupanga ziara za uchungaji kwa wote wasiotenda. Ikionekana kwamba mtu huyo atanufaika na funzo la Biblia, mwangalizi wa utumishi atapanga msaada utolewe, baada ya kushauriana na washiriki wengine wa halmashauri ya utumishi kuhusu mtu atakayefaa kuongoza funzo hilo. Ijapokuwa huenda isiwe lazima kuongoza funzo kwa muda mrefu, mtu aliyeombwa kuliongoza anaweza kuripoti wakati, ziara za kurudia, na funzo la Biblia.

12 Mnamo mwezi wa Aprili mwaka jana, dada aliyekuwa akihubiri nyumba hadi nyumba alimpa kijana mwanamume magazeti barabarani. Alifichua kwamba mke wake alikuwa Shahidi asiyetenda. Aliuliza mahali lilipokuwa Jumba la Ufalme na akamwalika dada huyo kuwatembelea yeye na mke wake. Tokeo likawa kwamba, wenzi hao wawili walihudhuria mkutano uliofuata na kukubali kujifunza Biblia.

13 Jitayarishe Kuongeza Utendaji! Mtunga-zaburi ambaye alitangaza kwamba twapaswa kulijulisha jina la Yehova na matendo yake aliongezea hivi: “Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi, zitafakarini ajabu zake zote. Jisifuni kwa jina lake takatifu.” (Zab. 105:2, 3) Na tutafakari jina kuu la Yehova na “ajabu zake” kwa kuongeza jitihada zetu katika huduma, tukifanya majira haya ya Ukumbusho yawe yenye kupendeza zaidi ya yote!

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

Njia Mbalimbali za Kuratibu Saa 12 kwa Juma Ili Kuwa Painia-Msaidizi

Siku Muda wa Saa

Jumatatu 1 2 − −

Jumanne 1 − 3 −

Jumatano 1 2 − 5

Alhamisi 1 − 3 −

Ijumaa 1 2 − −

Jumamosi 5 4 3 5

Jumapili 2 2 3 2

Jumla: 12 12 12 12

Je, mojawapo ya ratiba hizi itakufaa? Kama sivyo, kwa nini usitengeneze ratiba yako mwenyewe?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki