Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Februari: Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?, Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, au kitabu chochote cha zamani chenye kurasa 192 ambacho kutaniko linacho akibani. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapopata watu wenye kupendezwa kwenye ziara za kurudia, waweza kutoa maandikisho. Toa kitabu Ujuzi au broshua Anataka, ukiwa na lengo la kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Machi 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Jambo hilo lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu itakayofuata kusomwa.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa kuna wowote wanaopata ugumu wa kutimiza takwa la saa, wazee wapaswa kupanga ili usaidizi utolewe. Ili kupata madokezo, pitia barua za kila mwaka za Sosaiti S-201-SW za Oktoba 1. Ona pia fungu la 12-20 la nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1986.
◼ Mwandishi apaswa kuhakikisha kwamba ofisi inajulishwa hali ya wahubiri wote waliobatizwa ambao wamepeleka fomu za Ombi la Kujitolea Kushiriki Katika Programu ya Ujenzi wa Majumba ya Ufalme (A-25-SW). Kunapokuwa na marekebisho kuhusu hali ya mwenye kujitolea, kama vile mtu akihama au kuwekwa rasmi kuwa mtumishi wa huduma au mzee, fomu mpya zapasa kujazwa mara moja na kutumwa. Anwani ya mwenye kujitolea au namba ya simu ikibadilika, au kama hana msimamo mzuri tena kutanikoni, wazee wapaswa kujulisha ofisi upesi kwa barua.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote I —Kiarabu
Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! —Kipunjabi