Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/01 uku. 4
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 4/01 uku. 4

Matangazo

◼ Toleo la vichapo la Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapopata watu wenye kupendezwa kwenye ziara za kurudia, waweza kutoa maandikisho. Toa kitabu Ujuzi au broshua Anataka, ukiwa na lengo la kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Juni: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Julai: Broshua zozote zenye kurasa 32 zaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali? Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza, Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? na kijitabu Roho Zisizoonekana—Je! Zinatusaidia au Zinatuumiza? vyaweza kutolewa mahali panapovifaa.

◼ Kuanzia Aprili, beji za mkusanyiko wa wilaya wa 2001 za Kifaransa, Kiganda, Kiingereza, Kirundi na Kiswahili zitatiwa ndani ya upakizi wa vichapo wa kutaniko. Haitakuwa lazima kuziagiza. Beji zitapakiwa kwa mafungu yaliyo na kadi 25 ikitegemea ukubwa wa kila kutaniko. Ikiwa beji za ziada zahitajiwa na makutaniko, zapasa kuagizwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14-SW). Vifuko vya beji vya plastiki vyaweza kuagizwa kwa ajili ya yeyote kutanikoni anayevitaka.

◼ Mgawo Na. 3 na Na. 4 katika “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2001” umetolewa katika kurasa na mafungu yaliyochaguliwa kutoka katika kitabu Kutoa Sababu. Yale mafungu yanayoanza kwa sentensi iliyojongezwa ndani ndiyo yanayohesabiwa.

◼ Kampeni yetu ya kila mwaka ya maeneo ya mbali itakuwa mwezi wa Julai na Agosti. Makutaniko yatagawiwa maeneo ya kuhubiri miezi hiyo. Makutaniko yaliyo na maombi ya pekee ya eneo la mbali yanaweza kuandikia ofisi ya tawi kabla ya Mei 15, 2001. Kutaniko lolote ambalo halijagawiwa eneo la mbali linaweza kupanga kuhubiri eneo la kutaniko lisilohubiriwa mara nyingi.

◼ Ni lazima Sosaiti iwe na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kutakuwa na badiliko lolote, mwandishi anapaswa kujaza fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29-SW) na kuituma kwa Sosaiti haraka iwezekanavyo. Hiyo yatia ndani mabadiliko yoyote katika anwani ya eneo lao.

◼ Waandishi wa kutaniko wanapaswa kuweka fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205-SW) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b-SW). Fomu hizo zaweza kuombwa kupitia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14-SW). Wekeni angalau akiba ya mwaka mmoja. Chunguzeni fomu zote za ombi la painia wa kawaida ili kuhakikisha kwamba zimejazwa vizuri. Ikiwa wenye kuzijaza hawakumbuki vizuri tarehe ya ubatizo wao, wanapaswa kukadiria tarehe hiyo na kuiandika mahali.

◼ Chapa kubwa ya kitabu Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote I inatayarishwa kwa manufaa ya wale wenye tatizo la kuona. Kitabu hicho cha jalada la karatasi chenye ukubwa wa gazeti kitakuwa na kurasa 512 bila picha, na saizi ya herufi zake itakuwa kama ile ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la chapa kubwa lililo na makala mbili za funzo. Kitabu hiki kitapatikana katika Kiingereza tu kwa wakati huu. Lugha nyinginezo zitatangazwa zipatikanapo. Chaweza kuorodheshwa kwenye fomu ya ombi kama Unabii wa Isaya I-Chapa Kubwa.

◼ Iwapo wakati wowote utapanga kusafiri kwenda nchi nyingine, na utake kufahamishwa tarehe, nyakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kusanyiko la mzunguko au mkusanyiko wa wilaya, uliza ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Utapata orodha ya anwani za ofisi za tawi katika ukurasa wa mwisho wa Yearbook ya karibuni.

◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:

Jina la Mungu Litakaloendelea Milele —Kitigrinya

Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote —Kiswahili

Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini? —Kiarabu, Kichina (Sahili)

Mungu Anataka Tufanye Nini? —Kichina Sahili (Kipinyin), Kiganda, Kijaluo, Kirutoro, Kiswahili (cha Congo), Kiteso, Kizande

Mwimbieni Yehova Sifa (Nyimbo 29) —Kihindi

Serikali Itakayoleta Paradiso —Kirundi

Sikiliza Unabii wa Danieli! —Kiswahili

Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote I —Kiamhara

Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! —Kiurdu

Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani (Trakti Na. 15) —Kibari

Vichwa vya Biblia vya Mazungumzo —Kiamhara

Yehova—Yeye Ni Nani? (Trakti Na. 23) —Kiswahili

Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi —Kitigrinya

The Guidance of God—Our Way to Paradise —Kibengali, Kigujarati, Kiurdu

Watch Tower Publications Index 1997 —Kifaransa

Watch Tower Publications Index 1998 —Kifaransa

Watch Tower Publications Index 1999 —Kifaransa

◼ Kaseti Mpya za Vidio Zinazopatikana:

Noah—He Walked With God —Kiarabu, Kichina (Mandarin)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki