Toa Magazeti kwa Bidii!
1 Twaweza kutumiaje mambo yafuatayo?: (1) Kila mhubiri apaswa kuagiza magazeti ya kutosha lakini idadi inayofaa. (2) Ione kila Jumamosi kuwa Siku ya Magazeti. (3) Panga ratiba yako ya utumishi itie ndani utendaji wa magazeti kila mwezi. (4) Panga kutoa ushahidi wa vivi hivi zaidi ukitumia magazeti kuanzisha mazungumzo. (5) Wapelekee wafanyabiashara na wataalamu makala za pekee ambazo yaelekea watapendezwa nazo. (6) Andika maandishi sahihi ya magazeti uliyoachia watu, na usitawishe njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida, ukirudi kwa ukawaida na matoleo ya karibuni. (7) Tumia vizuri magazeti ya zamani ili yasirundamane. Onyesha makala za magazeti ya karibuni ambayo labda yatachochea kupendezwa.
2 Onyesho fupi la utoaji wa magazeti: “Makala hii ya Amkeni! yazungumzia kindani jambo hili.” Kisha soma sentensi moja au mbili ulizotaja mwanzoni na uendelee kusema: “Kwa kuwa yaonekana unapendezwa na jambo hili, je, ungependa kusoma makala hii na makala nyinginezo za wakati unaofaa katika toleo hili la Amkeni!? Ukipenda, nitafurahi kukuachia gazeti hili pamoja na lile linaloandamana nalo, Mnara wa Mlinzi.” Mwenye nyumba akikubali kuchukua magazeti, huenda ikafaa kusema hivi: “Kazi yetu inafanywa ulimwenguni pote na inategemezwa kwa michango ya hiari. Ukipenda kutoa mchango kidogo leo, nitaupokea kwa furaha.” Akikubali kutoa mchango mshikie bahasha ya pekee ili atie mchango wake na umshukuru na kumhakikishia kwamba mchango wake utatumiwa kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote. Akisema hana pesa usimwambie akurudishie magazeti lakini mtie moyo ayasome.
3 Ikiwa tuna bidii ya kutoa magazeti, hatupaswi kamwe kuacha kupanda mbegu za Ufalme kwa kutumia magazeti yetu. Ijapokuwa twahitaji kutumia utambuzi ili magazeti yetu yasipotezwe kwenye ‘udongo wenye miamba-miamba,’ wale wanaothamini habari njema wanafurahia kusoma magazeti na wanafurahi kutoa michango ya hiari wanapoweza.—Mr. 4:5, 6, 16, 17, linganisha Mathayo 10:42.