Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa mahali panapozifaa. Kijitabu Roho Zisizoonekana na vitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu na Maswali Ambayo Vijana Huuliza Majibu Yafanyayo Kazi vyaweza kutolewa pia katika miezi hiyo. Septemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, na Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa kwenye ziara ya kurudia, waweza kutoa andikisho. Novemba: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Ikiwa watu tayari wana vichapo hivyo, twaweza kutoa Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu au kichapo kingine chochote.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeagizwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko kuhusu ukaguzi huo baada ya kusomwa kwa ripoti ya hesabu.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza 2002 Calendar of Jehovah’s Witnesses pamoja na ombi lao la vichapo la Septemba. Kalenda zitapatikana katika Kiarabu, Kichina, Kifaransa, Kihindi, na Kiingereza.
◼ Fomu za kutosha za kutumia wakati wa mwaka wa utumishi wa 2002 zitatumwa kwa kila kutaniko. Tafadhali tumieni fomu hizo kwa busara. Zapasa zitumiwe tu kama zilivyokusudiwa.
◼ Kuanzia mwaka huu, mapainia wa kawaida walio na umri wa chini ya miaka 16 hawataweza kuhudhuria Shule ya Utumishi wa Painia isipokuwa wafikie umri huo kufikia Septemba 1 ya mwaka wanaopaswa kuhudhuria shule hiyo. Endapo mzazi wa painia huyo mchanga anastahili pia kuhudhuria darasa hilo, painia huyo mchanga atahudhuria.
◼ Kuanzia Agosti 31, 2001, hadi Septemba 1, 2001 vichapo vyote vilivyoko Betheli vitakuwa vikihesabiwa. Kwa sababu ya hesabu hiyo, hakuna maagizo yoyote ya vichapo ya kutaniko yatakayofanyiwa upakizi au yatakayochukuliwa siku hizo.
◼ Kuanzia toleo la Septemba 1, 2001, gazeti la Mnara wa Mlinzi litachapishwa katika chapa kubwa kwa Kiswahili.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Mwimbieni Yehova Sifa (Nyimbo 29) —Kitigrinya
Mungu Anataka Tufanye Nini? —Kiacholi, Kirundi
Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Unaweza Kulipataje? —Kiniue
Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote I —Kipunjabi
Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! —Kibengali
The Guidance of God—Our Way to Paradise —Kihindi