Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Septemba 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 13: Mwangalizi-msimamizi azungumza pamoja na wasikilizaji juu ya “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 1979, ukurasa wa 22-23 au toleo la Kiingereza la Mei 15, 1979, ukurasa wa 30-31.
Dak. 22: “Je, Unatimiza Huduma Yako Kikamili?”a Baada ya kuzungumzia fungu la 1-3 pamoja na wasikilizaji, toa maonyesho mawili mafupi ya utoaji wa magazeti—moja ukitumia gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15 na lingine ukitumia gazeti la Amkeni! la Septemba 22. Baada ya kuzungumzia fungu la 4, toa onyesho la utoaji uliodokezwa, na kitabu Ujuzi.
Wimbo 124 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 17
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. “Yako Kwenye Index.” Onyesha jinsi ya kupata utoaji wa toleo la mwezi huu.
Dak. 15: Tulitimiza Nini Mwaka Uliopita? Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi. Taja mambo makuu ya ripoti ya kutaniko ya mwaka wa utumishi wa 2001. Pongeza kila mtu kwa mambo mazuri yaliyotimizwa. Kazia yale ambayo kutaniko limetimiza kuhusu hudhurio la mikutano, kuwa wa kawaida katika utumishi wa shambani, na kuongoza mafunzo ya Biblia, ukionyesha madokezo yafaayo ya kufanya maendeleo. Weka miradi ya mwaka ujao inayoweza kufikiwa.
Dak. 15: Sanduku la Swali. Hotuba. Zungumzieni ratiba ya kila juma ya mikutano ya utumishi wa shambani ya kutaniko. Eleza jinsi wote wanaohudhuria wanavyoweza kuchangia kutoa maelezo yenye kujenga katika mikutano hiyo. Tia moyo kutaniko liunge mkono mipango hiyo ya utumishi.
Wimbo 129 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 24
Dak. 15: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Septemba kufikia mwisho wa juma hili.
Dak. 30: Mpende Mungu—Si Vitu vya Ulimwengu. (1 Yoh. 2:15-17) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji mkipitia tena programu ya kusanyiko la mzunguko lililofanywa mwaka wa utumishi uliopita. Alika wahubiri waeleze mambo makuu waliyojifunza na jinsi walivyoweza kuyatumia kibinafsi au wakiwa familia. (Wahubiri waweza kugawiwa sehemu hii mapema.) Zungumzieni sehemu hizi za programu: (1) “Kumpenda Mungu Hutuchochea Katika Huduma Yetu.” Upendo huo hutusaidia kukabiliana na hisia zisizofaa ambazo huenda zikatuzuia kuhubiri—kuona haya, kuhisi hatustahili na kuhofu wanadamu. (2) “Wampendao Yehova Huchukia Mabaya.” (w99-SW 10/1 28-31) Kuwa na uhusiano pamoja na Mungu hutegemea kuchukia yale anayochukia—si tu yale ambayo ni maovu kabisa bali pia maovu yasiyoonekana wazi. (3) “Fuatia Njia Izidiyo ya Upendo.” (w92-SW 7/15 27-30) Andiko la Wakorintho wa Kwanza 13:4-8 huonyesha kwa nini tunavumilia hali ya kutokamilika ya wengine, tukiepuka kuwa wenye ubinafsi na mashindano, kwa nini hatuenezi porojo zenye kudhuru, na kwa nini tunadumu tukiwa waaminifu kwa tengenezo la Mungu. (4) “Vitu Vilivyo Katika Ulimwengu—Tunavionaje?” Hatupaswi kupenda vitu vilivyo katika ulimwengu, kushindwa na tamaa za mwili, kukengeushwa na tamaa za macho yetu, au kujivunia mali zetu. (5) “Kutokuwa Sehemu ya Ulimwengu Kunatulinda.” Andiko la Wakorintho wa Pili 6:14-17 huonyesha jinsi imani, desturi na mazoea mengine yanavyoweza kutufanya tukataliwe na Mungu. Lazima tutambue na kuepuka mitego iliyobuniwa na Ibilisi. (6) “Ahadi za Mungu kwa Wale Wanaompenda.” (w86-SW 6/15 5-6) Baraka za Yehova hutuongezea furaha maishani na huboresha hali yetu ya kiroho.—1 Tim. 6:17-19.
Wimbo 133 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 1
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye safu “Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti,” toa onyesho ukitumia gazeti Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1.
Dak. 13: Naweza Kufanyaje Maendeleo Shuleni? Mzee na mke wake au mtumishi wa huduma na mke wake wanazungumza na mtoto wao anayeenda shule. Wana wasiwasi kwa sababu mtoto wao hafanyi vizuri kimasomo. Wanaongea juu ya shauri lililo katika kitabu Vijana Huuliza, sura ya 18, na kuzungumzia maendeleo ambayo mtoto wao anahitaji kufanya. Wazazi wanakazia umuhimu wa kupata elimu bora ya msingi ili kutumia uwezo wake wote katika kufuatia utumishi mtakatifu.
Dak. 20: “Je, Ni Kizuizi cha Kuhubiri?”b Kazia uhitaji wa kuwa na usawaziko katika kazi ya kimwili, ukitanguliza masilahi ya Ufalme. Alika baadhi ya vichwa vya familia katika kutaniko wasimulie jinsi ambavyo wanakabiliana na ugumu wa kuruzuku familia zao bila kuhatarisha mahitaji yao ya kiroho.
Wimbo 137 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.