Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Desemba 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Mahali ambapo video zapatikana, tia moyo kila mtu atazame video To The Ends of the Earth akijitayarisha kwa mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Desemba 24. Mahali ambapo hakuna video, zungumzieni “Kikumbusho” juma la Desemba 24.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: “Baraka Tunazopata kwa Kuthamini Upendo wa Yehova—Sehemu ya 2.”a Mnapozungumzia fungu la 2-6, alika kutaniko lisimulie mambo waliyoona walipokuwa wakiwafariji na kuwapa tumaini wale walioshuka moyo au wenye wasiwasi kwa sababu ya msiba wa hivi majuzi. Panga mapema kuwe na maonyesho ya jambo moja au mawili ya mambo hayo yaliyoonwa.
Wimbo 222 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Taja mipango ya utumishi wa shambani ya Desemba 25 na Januari 1.
Dak. 22: “Litumie Sawasawa Neno la Mungu.”b Tia ndani onyesho linalofaa eneo lenu juu ya fungu la 4. Pia, panga kuwe na onyesho lenye matokeo la jinsi ya kutia watu moyo au kuwafariji wanaosononeka kwa sababu ya matukio ya ulimwengu ya hivi karibuni. Jambo fupi lililoonwa laweza kusimuliwa. Uliza wasikilizaji waeleze kwa nini wanahisi kwamba kutumia Biblia kutafanya mahubiri yawe na matokeo zaidi.
Dak. 13: ‘Ninyi Mna Biblia Yenu Wenyewe.’ Mazungumzo na wasikilizaji yakihusu kitabu Kutoa Sababu ukurasa wa 251-252. Ikiwa watu hawataki kusikiliza kwa sababu twatumia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, tuseme nini? Panga mapema wahubiri waseme kwa maneno yao wenyewe majibu yaliyodokezwa.
Wimbo na 225 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 24
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Eleza toleo la vichapo la Januari na broshua ambazo kutaniko linazo akibani.
Dak. 10: “Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2002.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Tia moyo wote wawe na bidii kutimiza migao yao.
Dak. 25: Mahali ambapo hakuna video, zungumzieni “Kikumbusho.” Mahali ambapo video zapatikana, zungumzieni “Kuhubiri Tukitumia Video—To The Ends of the Earth.” Mazungumzo na wasikilizaji. Tia moyo wote wafikirie kwa uzito juu ya yale ambayo wanaweza kufanya ili kuhubiri habari njema katika eneo lenu, au mahali penye uhitaji mkubwa zaidi. Rejezea Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 2001, ukurasa wa 4. Mwezi wa Februari tutazungumzia video Noah—He Walked With God.
Wimbo 24 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 31
Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Desemba. Ikiwa kutaniko lenu litabadili saa za mikutano mwaka ujao, tia moyo kila mtu ahudhurie kwa ukawaida saa hizo mpya. Hakikisha kwamba watu wote wenye kupendezwa na watu wowote wasiotenda wamejua mabadiliko hayo. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, toa onyesho la jinsi ya kutoa (1) Gazeti Mnara wa Mlinzi la Desemba 15 na (2) Gazeti la Amkeni! la Desemba 22.
Dak. 15: Wapeni Wazee Ufikirio Wanaostahili. Watumishi wa huduma wawili au watatu wazungumzia Mnara wa Mlinzi, Juni 1, 1999, ukurasa wa 18-19. Wanaeleza kuhusu kazi nyingi ambazo wazee wanafanya, kutia ndani kazi ya kimwili, madaraka ya familia, na migao ya kitheokrasi. Zungumzieni njia ambazo wote wanaweza kuwatia moyo, kurahisisha mzigo wao, na kufuata mwelekezo wao. Watumishi hao wanakubali kwamba wazee wanafanya utumishi wa maana sana na wanastahili “ufikirio ambao ni zaidi kuliko ule wa kawaida.”—1 The. 5:12, 13.
Dak. 17: “Mkusanyiko wa Wilaya wa 2002 wa ‘Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii’ wa Mashahidi wa Yehova.”c Itolewe na mwandishi, akikazia fungu la 4-9. Fungu la 3 linapozungumziwa, soma barua inayojulisha mahali pa mkusanyiko ya Desemba 15, 2001. Pongeza kutaniko kwa uchangamfu kwa kufanya mipango yao ya mkusanyiko bila kukawia.
Wimbo 219 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 7
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, toa maonyesho mawili mafupi ya magazeti, moja ukitumia gazeti Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na jingine ukitumia gazeti Amkeni! la Januari 8. Panga kijana atoe moja ya maonyesho hayo.
Dak. 18: Tumia Maisha Yako kwa Njia Ifaayo Kabisa. Washiriki wa familia wazungumzia Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1998, ukurasa wa 8-9. Baba anataka familia ifuatie maisha yatakayowaletea shangwe badala ya kukata tamaa. Wanazungumzia onyo lililo katika makala hiyo linaloonyesha jinsi ya kupata furaha, wakikazia uhitaji wa kuwa wenye utambuzi, kutanguliza mambo ya maana, na kumtumaini Yehova. Wanazungumzia marekebisho yanayofaa wanayoweza kufanya wakiwa familia.
Dak. 15: Kulitunza Sana Jumba Letu la Ufalme. Hotuba itolewe na mzee. Angalieni hali ya Jumba la Ufalme. Kuna mipango gani ya kusafisha kabla ya Ukumbusho? Ni marekebisho gani yanayohitaji kufanywa kabla ya wakati huo? Eleza jinsi kutaniko linavyoweza kusaidia. Kazia uhitaji wa kuhakikisha kwamba mahali petu pa ibada panaonyesha uzuri na heshima inayostahili nyumba ya Yehova.—Zab. 84:1.
Wimbo 126 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.