Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Desemba na Januari: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa inapofaa. Februari: Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?, au kitabu kingine cha zamani cha kurasa 192 ambacho kutaniko linacho akibani. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza mabuku yaliyojalidiwa ya Watchtower na Awake! ya mwaka wa 2001 pamoja na ombi lao la vichapo la Desemba. Mabuku yaliyojalidiwa yatapatikana katika Kichina, Kifaransa na Kiingereza. Hadi mabuku yaliyojalidiwa yapatikane na upakizi ufanywe, yataonyeshwa kama “Vitatumwa Vikipatikana” katika orodha ya upakizi ya kutaniko. Mabuku yaliyojalidiwa ni bidhaa za ombi la pekee.
◼ Mialiko ya Ukumbusho ya 2002 katika lugha kuu ya kila kutaniko itatumwa. Ikiwa kuna lugha nyingine katika eneo lenu na mngependa mialiko ya lugha hizo, yapasa kuombwa bila kukawia kupitia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14-SW). Mialiko ya Ukumbusho yapatikana katika Kiarabu, Kichina (Sahili), Kifaransa, Kiganda, Kigujarati, Kihindi, Kiingereza, Kipunjabi, Kirundi, na Kiswahili. Tafadhali ombeni tu lugha zile zinazohitajiwa katika eneo lenu.
◼ Tafadhali tunawajulisha kwamba Ukumbusho wa mwaka wa 2003 utafanywa Jumatano, Aprili 16, baada ya jua kutua. Taarifa hii imetolewa mapema ili akina ndugu waweze kukodi au kufanya maagano ya lazima kwa majumba yanayopatikana mahali ambako kuna makutaniko kadhaa yanayotumia Jumba la Ufalme na inawalazimu kutafuta majengo mengine. Wazee wanapaswa kuwa na mapatano pamoja na wasimamizi wa jengo wakihakikisha kwamba hakutakuwa na usumbufu kutokana na utendaji mwingine katika jengo hilo ili mwadhimisho wa Ukumbusho uweze kuendelea kwa njia ya amani na kwa utaratibu. Kwa sababu ya umuhimu wa tukio hili, baraza la wazee linapochagua msemaji wa Ukumbusho, lapaswa kuteua mmojawapo wa wazee wenye kustahili zaidi badala ya kupokezana zamu tu au kutumia ndugu yuleyule kila mwaka. Isipokuwa tu kuwe na mzee mwenye uwezo aliye mmoja wa watiwa-mafuta anayeweza kutoa hotuba hiyo.
◼ Kuhesabiwa kwa vichapo na magazeti yote yaliyopo kwapaswa kufanywa Desemba 31, 2001 au karibu iwezekanavyo na tarehe hiyo. Hesabu hiyo ni kama ile inayofanywa kila mwezi na mratibu wa vitabu, na jumla zapasa kuandikwa kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18-SW). Jumla ya idadi ya magazeti yaliyopo inaweza kupatikana kutoka kwa watumishi wa magazeti katika kila kutaniko kwenye kikundi cha vitabu. Kila kutaniko linaloratibu litapokea nakala tatu za fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18-SW). Tafadhali tumeni nakala ya awali kwa ofisi kabla ya Januari 6. Wekeni nakala ya kaboni kwenye faili zenu. Nakala ya tatu inaweza kutumiwa ili kufanyia hesabu. Mwandishi wa kutaniko linaloratibu apaswa kusimamia kazi hiyo ya kuhesabu vichapo. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi wa kutaniko linaloratibu watatia sahihi fomu hiyo.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Mwimbieni Yehova Sifa (nyimbo 100) —Kiganda
Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele—Chapa Kubwa —Kiingereza