Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/02 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Februari 11
  • Juma Linaloanza Februari 18
  • Juma Linaloanza Februari 25
  • Juma Linaloanza Machi 4
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 2/02 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Februari 11

Wimbo 6

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Mahali ambako kuna video, tia moyo kila mtu asome Mwanzo 6:1 hadi 9:19 na kutazama video ya Noah—He Walked With God akijitayarisha kwa mazungumzo ya Mkutano wa Utumishi wa juma la Februari 25.

Dak. 20: “Lihubiri Neno la Mungu Kikamili.”a (Fungu la 1-13) Ishughulikiwe na mwangalizi-msimamizi. Mazungumzo yenye uchangamfu kuhusu yale ambayo tunataka kutimiza mwezi wa Machi na kuendelea. Kila mtu anapaswa kutumia kalenda iliyo katika nyongeza ili apange ratiba itakayofaa ya kwenda katika huduma kadiri iwezekanavyo mwezi wa Machi. Tia moyo wote wanaoweza wafanye upainia-msaidizi mwezi huo. Mnapozungumzia fungu la 7-8, omba wale waliofanya upainia-msaidizi wakati wa majira ya Ukumbusho ya mwaka jana wasimulie baraka walizopata. Tangaza kwamba fomu za kujaza maombi ya kufanya upainia-msaidizi zitapatikana baada ya mkutano huu.

Dak. 13: “Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti.” Omba wahubiri waeleze jinsi ambavyo sehemu hii katika Huduma Yetu ya Ufalme imewasaidia kujitayarisha vizuri kuunganisha makala za magazeti pamoja na matukio mabaya katika nyakati hizi za hatari. Wengine wamepata matokeo gani kwa kuwafariji watu na kuwasaidia wapate majibu ya Biblia kwa maswali yanayotatiza? Panga kuwe na maonyesho mawili mafupi yanayoonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 1 na la Amkeni! la Februari 8.

Wimbo 49 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 18

Wimbo 95

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 12: “Watu Wenye Furaha Zaidi Duniani.”b Zungumzia kifupi “Hatua Kuelekea Furaha,” katika Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1997, ukurasa wa 6.

Dak. 25: “Lihubiri Neno la Mungu Kikamili.”c (Fungu la 14-23) Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Zungumzia mipango ya pekee iliyofanywa kwenu ili watu washiriki katika utendaji zaidi mwezi wa Machi. Eleza ratiba yote ya mikutano ya utumishi wa shambani ya mwezi huo. Zingatieni kuhuisha wasiotenda na kusaidia watoto na wanafunzi wa Biblia wastahili kuwa wahubiri wasiobatizwa. Tangaza majina ya wale ambao watafanya upainia-msaidizi mwezi wa Machi, na utie moyo wengine wafikirie jambo hilo kwa sala ili wajiunge nao.

Wimbo 143 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Februari 25

Wimbo 174

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Toa maonyesho mawili mafupi ya magazeti—moja likionyesha jinsi ya kutumia Mnara wa Mlinzi Februari 15 na lingine Amkeni! Februari 22. Panga kijana atoe onyesho moja kati ya hayo mawili. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Februari.

Dak. 15: Onyesha Upendo Wako kwa Mungu. Ona broshua Rafiki ya Mungu ukurasa wa 26-27 au, mahali ambako kuna video zungumzieni “Matokeo ya Video Zinazotoa Ushahidi.” Mazungumzo na wasikilizaji. Kufikia sasa, tumechunguza video nane kwenye Mkutano wa Utumishi. Baada ya kuzungumzia kifupi mifano iliyo katika makala hiyo, omba wahubiri wasimulie mafanikio ambayo wamepata kwa kuonyesha watu video.

Dak. 15: “Je, Una ‘Moyo Mtiifu’ Kama Noa?” Ona Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 1998, ukurasa wa 29-31, au mahali ambako kuna video zungumzieni “Kila Mtu Anaweza Kujifunza Kutokana na Video ya Noah—He Walked With God.” Anza moja kwa moja mazungumzo juu ya video ya Noah pamoja na wasikilizaji, ukitumia tu maswali yaliyo kwenye sanduku lililo katika ukurasa huu. Mwezi wa Aprili tutachunguza video ya Young People Ask—How Can I Make Real Friends?

Wimbo 215 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 4

Wimbo 207

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 12: “Saidia Wengine Wawe Rafiki za Mungu.”d Tia ndani onyesho fupi la kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia broshua hii.

Dak. 12: Tumia Kitabu Ujuzi ili Kuanzisha Mafunzo. Katika mwezi wa Machi tungependa kujitahidi zaidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Simulia kifupi jambo lililoonwa linalopatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme, ya Agosti 1998 ukurasa wa 4, fungu la 8. Ikiwa mtu fulani alianzisha funzo hivi majuzi kwa kutumia kitabu Ujuzi, panga igizo lifanywe kuonyesha jinsi lilivyoanzishwa. Kumbusha kila mtu kuhusu yale “Madokezo ya Kutoa Kitabu Ujuzi,” katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002. Ukitumia kitabu hicho, toa onyesho la kutumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 katika nyongeza chini ya kichwa “Njia ya Moja kwa Moja.”

Dak. 16: “Kwa Nini Twendelee Kuhubiri?”e Malizia kwa kuhoji mhubiri mmoja au wawili ambao wameendelea kuhubiri kwa miaka mingi. Waombe waeleze ni kwa nini wameendelea katika kazi hii na jinsi ambavyo imewafaidi.

Wimbo 223 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

e Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki