Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/02 uku. 8
  • Je, Kutaniko Lenu Lina Eneo Kubwa Mno?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Kutaniko Lenu Lina Eneo Kubwa Mno?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Watu Wasipopatikana Nyumbani
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Je, Una Eneo la Kibinafsi?
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Je, Utanufaika kwa Kuwa na Eneo la Kibinafsi?
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 5/02 uku. 8

Je, Kutaniko Lenu Lina Eneo Kubwa Mno?

1 Kuanzia majiji ya Yudea hadi sehemu za mashambani za Galilaya, Yesu alihubiri sana kotekote katika eneo kubwa la Israeli ya kale. (Mr. 1:38, 39; Luka 23:5) Sisi pia lazima tuhubiri habari njema kwa watu wengi iwezekanavyo. (Mr. 13:10) Hata hivyo, jambo hilo laweza kuwa gumu. Kwa nini?

2 Maeneo ya makutaniko mengi ya Afrika Mashariki ni sehemu za mashambani, yakiwa na ukubwa wa mamia ya kilometa za mraba. Huenda makutaniko mengine yakahubiri maeneo ya majiji makubwa-makubwa, wakitafuta watu wanaoweza kusikiliza habari njema. Twaweza kufanya nini ili kusaidia watu wanaoishi katika maeneo makubwa mno kujifunza kweli kuhusu Yehova, Yesu, na Ufalme?

3 Panga Vizuri: Mwangalizi wa utumishi na mtumishi wa eneo wanahitaji kupanga jinsi kutaniko linavyoweza kuwa na matokeo bora. Labda mwaweza kupanga mwe na Jumamosi za pekee ili watu wengi waweze kuhubiri siku nzima. Mnapohubiri maeneo ya mbali, pangeni mhubiri kwa muda mrefu ikiwezekana, mbebe chakula cha mchana. Mnaweza kukutana kwa ajili ya utumishi mapema kuliko kawaida ili mwe na wakati wa kusafiri kwenye eneo au kufanya mkutano wa utumishi wa shambani karibu na eneo litakalohubiriwa. Pangeni vikundi vidogo-vidogo ili watu wawe na eneo la kutosha. Pangeni kuhubiri mashambani wakati hali ya hewa na barabara ni nzuri.

4 Wale wanaohubiri majijini au mijini wanaweza kuokoa wakati ikiwa watakuwa na mipango ya kuwa na eneo la kutosha. Panga maeneo ili kikundi cha utumishi kiwe na eneo la kutosha kuhubiriwa asubuhi nzima au alasiri nzima.

5 Hakikisha kwamba unachukua vichapo vya kutosha. Ikiwa eneo halihubiriwi kwa ukawaida, huenda ikafaa kuacha trakti au gazeti la zamani mahali ambapo hakuna watu nyumbani. Ikiwa trakti yenye kichwa Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? inapatikana katika lugha yenu, mwachie kila mtu unayekutana naye na uiache kwenye nyumba ambazo wenyewe hawako.

6 Shirikiana Kabisa: Kuhubiri eneo kubwa hutaka ushirikiano wa kila mtu kutanikoni. Ikiwa ni lazima watu wasafiri mbali, wale wanaosafiri pamoja wanaweza kuchangia gharama za petroli. Unapaswa kutumia utambuzi unapopata wenye nyumba walio tayari kuongea. Jitahidi kufikia watu wote katika eneo, na uwafikirie wale wanaokungojea katika kikundi chenu. Ikiwa ungependa kuendeleza mazungumzo pamoja na mtu anayependezwa, unaweza kupanga ili wale wengine katika kikundi waendelee kuhubiri.

7 Fanya mipango hususa ya kufuatia watu wote wanaopendezwa. Mbali na kujua mahali wanakoishi, jaribu kujua jinsi utakavyoweza kupata nyumba ya mtu mwenye kupendezwa utakaporudi. Kwa mfano, ikiwa barabara za mashambani hazina majina au nyumba hazina namba, chora vizuri ramani au fafanua jinsi ya kumpata mwenye kupendezwa utakapomrudia.

8 Ni pendeleo letu kutii maagizo haya ya Yesu: “Katika jiji lolote lile au kijiji chochote kile mwingiamo, tafuteni kabisa ni nani humo anayestahili”! (Mt. 10:11) Kwa kweli Yehova atabariki jitihada zako unapojitoa kwa hiari kufanya kazi hii yenye kuthawabisha zaidi!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki