Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/02 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 12
  • Juma Linaloanza Agosti 19
  • Juma Linaloanza Agosti 26
  • Juma Linaloanza Septemba 2
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 8/02 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Agosti 12

Wimbo 76

Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 15 na Amkeni! la Julai 22. Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti ya kujibu kizuia-mazungumzo “Mbona ninyi watu mnatembelea watu mara nyingi mno?”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 20.

Dak. 20: “Weka Miradi ya Kiroho.”a Mnapozungumzia fungu la 5, tia ndani maelezo yenye kutia moyo kuhusu upainia wa kawaida na wa pekee na utumishi wa Betheli kutoka katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 114-116.

Dak. 12: Mambo yaliyoonwa. Omba kutaniko lisimulie mambo ambayo wameona walipokuwa wakitumia trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? Je, mafunzo yoyote ya Biblia yameanzishwa? Ikiwa ndivyo, eleza yalianzishwa jinsi gani au uigize jambo moja au mawili yaliyoonwa. Zungumzieni sanduku “Fursa za Kugawanya Trakti” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 2002, ukurasa wa 3 na 4.

Wimbo 123 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 19

Wimbo 182

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Zungumzieni “Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee.” Tangaza tarehe ya kusanyiko la pekee litakalofuata, na uwasihi wote wafike mapema na kusikiliza kwa makini programu yote. Tia moyo wahubiri waalike watu wenye kupendezwa na mafunzo ya Biblia.

Dak. 15: Ni Nini Kinachowazuia? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji na onyesho. Katika huduma yetu tunakutana na watu ambao hawapendi kuzungumza juu ya imani zao. Hilo laweza kutuzuia tusiwaeleze ujumbe wa Ufalme. Tukitambua sababu inayomfanya mtu asitake kuzungumza, huenda jambo hilo likatusaidia tutayarishe utangulizi ambao utamvuta mtu huyo kuongea. Zungumzia jinsi tunavyoweza kurekebisha utoaji wetu tunapokutana na watu wa hali zifuatazo: (1) Wale wasiopendezwa na dini, hata na dini yao wenyewe. (2) Wale wanaoshikilia desturi za kidini za familia yao na mababu zao wa zamani. (3) Wale wasiopenda kuzungumza juu ya imani zao kwa sababu hawajui Maandiko ya kuunga mkono imani hizo. (4) Wale wanaotubagua kwa sababu ya kusikia mambo yasiyo ya kweli kutuhusu kutoka kwa wapinzani. Rekebisha orodha hiyo ilingane na eneo lenu, ukizingatia maoni ambayo sisi hupata kwa kawaida. Tia ndani onyesho fupi kuonyesha jinsi ya kumvuta mtu kwenye mazungumzo ya Kimaandiko.

Dak. 18: “Onyesha Uaminifu wa Kikristo Mtu wa Ukoo Anapotengwa na Ushirika.”b(Fungu la 1-8) Ishughulikiwe na mzee anayestahili, akitumia maswali yaliyopo. Mwombe ndugu anayejua kusoma vizuri asome kila fungu.

Wimbo 136 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 26

Wimbo 189

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga painia wa kawaida au msaidizi atoe onyesho la kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 na mhubiri atoe onyesho la Amkeni! la Agosti 8. Tia moyo wahubiri wote watumie andiko wanapohubiri.

Dak. 17: “Uwe Mwasiliani! ”c Kwa kumalizia, tia moyo wahubiri wachunguze sura yenye kichwa “Jinsi ya Kuboresha Stadi za Mazungumzo” katika kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ukurasa wa 62-65.

Dak. 18: “Onyesha Uaminifu wa Kikristo Mtu wa Ukoo Anapotengwa na Ushirika.”d (Fungu la 9-14) Ishughulikiwe na mzee anayestahili, akitumia maswali yaliyopo. Mwombe ndugu anayejua kusoma vizuri asome kila fungu.

Wimbo 125 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 2

Wimbo 84

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Agosti. Zungumzia kifupi makala “Soma Pamoja na Watoto Wako” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 1999, ukurasa wa 25.

Dak. 20: Jitayarishe Kabla ya Kwenda. Mazungumzo na onyesho. Kuwa na mpango mzuri huboresha huduma yetu. Kwa hiyo, panga mapema: (1) Kuchukua vichapo vinavyohitajiwa. (2) Hakikisha una karatasi za kutosha za rekodi ya nyumba kwa nyumba na kalamu au penseli. (3) Ikiwa wahitaji namna ya kusafiri, fanya mipango ya usafiri. (4) Fikiria ziara za kurudia unazopanga kufanya. (5) Tayarisha kile utakachosema. Ikiwa utaongoza mkutano wa utumishi wa shambani, uwe na eneo la kutosha. Zungumza pamoja na wasikilizaji njia moja au mbili ambazo kitabu Ufunuo chaweza kutolewa katika huduma wakati wa Septemba. Toa onyesho moja kati ya utoaji mbalimbali unaoonyeshwa, na utumie andiko katika mazungumzo.—Ona madokezo yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 1998, ukurasa wa 8.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Au omba kutaniko lisimulie mambo waliyoona walipokuwa wanafanya mahubiri yasiyo rasmi, labda walipokuwa wakiwahubiria watu katika maegesho ya magari, wakisafiri kwa gari la umma, kwenye bustani, na madukani, kwenye vituo vya basi, na mahali pengine pa umma. Igiza jambo moja au mawili yaliyoonwa.

Wimbo 99 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki