Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/02 uku. 1
  • Julisha Ukweli Kuhusu Yesu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Julisha Ukweli Kuhusu Yesu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Yohana 14:6—“Mimi ndiye Njia na Kweli na Uzima”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • “Njia na Kweli na Uzima”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
  • Ujumbe Ambao Ni Lazima Tuutangaze
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kwa Nini Tumfuate “Kristo”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 11/02 uku. 1

Julisha Ukweli Kuhusu Yesu

1 Wakristo watiwa-mafuta, wakisaidiwa na kondoo wengine, “[wana] kazi ya kutoa ushahidi kumhusu Yesu.” (Ufu. 12:17) Hii ni kazi muhimu, kwa kuwa wokovu utapatikana tu kupitia yeye.—Yoh. 17:3; Mdo. 4:12.

2 ‘Ndiye Njia, Kweli, na Uhai’: “Mimi ndiyo njia na kweli na uhai. Hakuna ajaye kwa Baba ila kupitia mimi.” (Yoh. 14:6) Tunaweza kumfikia Mungu kwa sala na kuwa na uhusiano mzuri Naye kupitia Yesu tu, ambaye ndiye ile “njia.” (Yoh. 15:16) Yesu ndiye “kweli” kwa kuwa alitimiza unabii mbalimbali na mambo mengine yaliyomo katika Maandiko ya Kiebrania. (Yoh. 1:17; Kol. 2:16, 17) Kwa kweli, kusudi kuu la unabii wa kweli ni kujulisha zaidi daraka kuu la Yesu katika kutimizwa kwa kusudi la Mungu. (Ufu. 19:10) Zaidi ya hayo, Yesu ni “uhai.” Ili kupata zawadi ya uhai wa milele, lazima watu wote wadhihirishe imani katika dhabihu yake ya fidia.—Yoh. 3:16, 36; Ebr. 2:9.

3 Ndiye Kichwa na Mfalme Anayetawala: Pia lazima watu watambue mamlaka kuu zaidi ambayo Yehova amempa Mwanaye. Yesu amewekwa kuwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, ‘na mataifa watamtii.’ (Mwa. 49:10) Kwa kuongezea, Yehova amemweka awe Kichwa cha kutaniko. (Efe. 1:22, 23) Twahitaji kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia waelewe jinsi Yesu anavyoliongoza kutaniko na kumtumia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” kuandaa ‘chakula cha kiroho kwa wakati ufaao.’—Mt. 24:45-47.

4 Kuhani wa Cheo cha Juu Mwenye Rehema: Kwa kuwa Yesu alipatwa na majaribu na kuteseka alipokuwa mwanadamu, yeye “aweza kuja kusaidia wale wanaotiwa kwenye jaribu.” (Ebr. 2:17, 18) Wanadamu wasiokamilika hufurahi sana kujua kwamba Yesu huwahurumia kwa sababu ya udhaifu wao na kuwaombea kwa fadhili! (Rom. 8:34) Kupitia dhabihu ya Yesu na huduma zake akiwa Kuhani wa Cheo cha Juu, twaweza kumfikia Yehova “kwa uhuru wa usemi” ili tuweze kupokea “msaada katika wakati ufaao.”—Ebr. 4:15, 16.

5 Jitihada zetu za kuwajulisha wengine kweli kuhusu Yesu na ziwachochee wamtii na kumtumikia pamoja nasi.—Yoh. 14:15, 21.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki