Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Mamilioni ya watu huamini kwamba ‘watakatifu’ wana nguvu ya pekee na kwamba inafaa kuomba kupitia kwao. Wafikirije? [Ngoja ajibu.] Ona vile Yesu alivyosema. [Soma Yohana 14:6.] Hilo hufanya wengi wajiulize kama inafaa kusali kupitia ‘watakatifu.’ Toleo hili la Mnara wa Mlinzi lazungumzia habari hiyo muhimu.”
Amkeni! Sept. 22
“Watu wengi leo wanahangaishwa na ugaidi, kutia ndani matumizi ya silaha za kibiolojia. Je, wafikiri kwamba serikali za kibinadamu zaweza kukomesha ugaidi katika ulimwengu huu? [Ngoja ajibu.] Biblia huonyesha kile ambacho Mungu anakusudia kufanya. [Soma Ezekieli 34:28.] Gazeti hili la Amkeni! lachunguza baadhi ya masuala yanayohusika.”
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Watu wengi wamejiuliza kama kutakuwako na wakati ambapo matatizo yote tunayoona kama vile vita, uhalifu, na vitendo vya ugaidi vitakoma kabisa. Wafikirije? [Ngoja ajibu.] Biblia yatoa uhakikisho huu wenye kufariji. [Soma Zaburi 37:10, 11.] Gazeti hili laeleza sababu gani Mungu hajakomesha uovu na mateso yanayotokana nao.”
Amkeni! Okt. 8
“Inaonekana kwamba leo kuna ongezeko kubwa zaidi la idadi ya familia zenye mzazi mmoja. Biblia yaonyesha kwamba Muumba wetu anawahurumia. [Soma Zaburi 146:9.] Toleo hili la Amkeni! laonyesha jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kuwasaidia wazazi kulea watoto wao kwa mafanikio.”