Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Ningependa kusikia maoni yako kuhusu kinachosemwa hapa. [Soma Kumbukumbu la Torati 32:4.] Umewahi kujiuliza ni kwa nini kuna mateso na uovu mwingi ulimwenguni ikiwa Mungu ni mweza-yote na mwenye haki? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza ni kwa nini Mungu ameacha uovu uendelee hadi siku zetu.”
Amkeni! Sept.
“Wengi wetu tunatamani kuwa na afya nzuri na maisha marefu. Unafikiri kwamba kuwa na mtazamo mzuri kunaweza kuboresha afya yetu? [Mruhusu ajibu. Kisha msomee Methali 17:22.] Makala hii inazungumzia kuhusu sababu zinazofanya liwe jambo muhimu kusitawisha mtazamo mzuri.” Onyesha makala inayoanzia ukurasa wa 26.
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Je, umewahi kusema, ‘Laiti ningalifanya mambo kwa njia tofauti!’? [Mruhusu ajibu.] Hebu ona maelezo haya kuhusu kwa nini mara nyingine sote tunafanya maamuzi tunayojutia baadaye. [Soma Yeremia 10:23.] Gazeti hili linaonyesha jinsi mashauri mazuri yanayopatikana katika Biblia yanatusaidia tufanye maamuzi mazuri.”
Amkeni! Okt.
“Je, unafikiri kwamba hali ni hatari zaidi wakati huu kwa watoto kuliko ilivyokuwa zamani? [Mruhusu ajibu.] Watu wengi wanahisi kwamba tunaishi katika nyakati zinazofafanuliwa hapa. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Gazeti hili linatoa mashauri yanayofaa kuhusu jinsi wazazi wanavyoweza kuwalinda watoto wao dhidi ya watu wanaowatendea watoto vibaya kingono.”