Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
Taja tukio la karibuni linalowahangaisha watu. Kisha uliza, “Je, unafikiri mstari huu wa Biblia unaeleza vizuri kuhusu nyakati tunamoishi? [Soma 2 Timotheo 3:1, kisha umruhusu ajibu.] Makala hii inaonyesha uthibitisho kwamba tunaishi katika siku za mwisho na kile tunachopaswa kufanya.”
Amkeni! Sept.
“Wengi wana maoni kwamba sisi tuliumbwa. Wengine nao huhisi kwamba tulitokea kupitia mageuzi. Je, wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi dokezo hili linavyotusaidia tufikie mkataa unaofaa. [Soma Ayubu 12:7, 8.] Toleo hili la pekee la Amkeni! linazungumzia kile tunachojifunza kutokana na hekima na ubuni unaodhihirika katika vitu vya asili.”
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Wataalamu wanajaribu kuondoa magonjwa na kutuongezea muda tunaoweza kuishi. Unafikiri itawezekana mwishowe kuishi milele? [Mruhusu ajibu.] Ona ni kwa nini tunatamani kuishi muda mrefu. [Soma Mhubiri 3:11.] Gazeti hili linaeleza ni kwa nini Mungu alituumba tukiwa na tamaa ya kuishi milele.”
Amkeni! Okt.
“Karibu kila mtu hufurahia kutazama televisheni. Lakini unafikiri tunapaswa kuteua kile tunachotazama? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Methali 13:20.] Gazeti hili linazungumzia jinsi televisheni inavyotuathiri na linatupatia madokezo kuhusu jinsi tunavyoweza kudhibiti utazamaji wetu.”