Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Mamilioni ya watu husema maneno haya yanayojulikana sana katika sala zao. [Soma Mathayo 6:10.] Unafikiri maisha yangekuwaje ikiwa mapenzi ya Mungu yangetimizwa kikamili duniani? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linafafanua ile Sala ya Bwana, kutia ndani sehemu ambayo tumesoma sasa hivi.”
Amkeni! Sept. 22
“Watu wengi wanahangaishwa na tatizo linalozidi kuongezeka la vijana kunywa pombe kupita kiasi. Je, wewe pia umeona hivyo? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Methali 20:1.] Vijana wanaokunywa kupita kiasi wanakabili hatari nyingi. Makala hii ina habari zinazoweza kuwasaidia kushinda vishawishi vya kunywa pombe kupita kiasi.”
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Sote tunatamani kuona uhalifu, jeuri, na vita vikikomeshwa. Je, unafikiri tutaona maneno haya yakitimizwa? [Soma Zaburi 37:11. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi ahadi hiyo inavyohusiana na kusudi la Mungu la awali kwa wanadamu na jinsi tunavyoweza kufaidika.”
Amkeni! Okt. 8
“Je, haisikitishi kwamba kila mwaka mamilioni ya wasichana ambao hawajaolewa hupata mimba? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia hatua wanazoweza kuchukua ili kukabiliana na magumu ya kuwa mama wakiwa vijana. Pia linaonyesha jinsi wazazi wanavyoweza kuwasaidia watoto wao kuepuka tatizo hili.” Soma 2 Timotheo 3:15.