Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Katika ulimwengu wa leo, watu fulani wanahisi kwamba wamenaswa katika ndoa isiyo na upendo. Watu hao wanaweza kupata wapi msaada? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatuhakikishia kwamba kanuni za Mungu zinaweza kutusaidia. [Soma Isaya 48:17, 18.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi huchanganua kanuni za Biblia zinazoweza kuimarisha ndoa.”
Amkeni! Sept. 22
“Sisi hushangazwa na uwezo wa wanyama wa kuwasiliana. Lakini, je, unajua kwamba wanadamu wana sifa za pekee? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Zaburi 65:2.] Tofauti na wanyama, sisi hutamani kuwasiliana na Mungu. Gazeti hili linaeleza jinsi tunavyoweza kuwa na mawasiliano mazuri kati yetu wenyewe na pamoja na Mungu.”
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Je, umewahi kujiuliza, ‘Ikiwa Mungu ni mwenye upendo na ana nguvu zote, mbona hawasaidii wale wanaoteseka?’ [Mruhusu ajibu.] Hivi karibuni atakomesha matatizo yote. [Soma Isaya 65:17.] Kwa sasa, Mungu hatazami tu bila kujali huku tunapoteseka, kama vile gazeti hili linavyoonyesha.”
Amkeni! Okt. 8
“Je, umesikia kwamba wakulima wengi wanashindwa kutegemea kilimo ili kujiruzuku? [Mruhusu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia tatizo hilo pamoja na ahadi ya Biblia ya wakati ujao ulio bora. [Soma Zaburi 72:16.] Nitakaporudi, nitakueleza jinsi Mungu atakavyotimiza jambo hilo.”