Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Unafikiri tunaweza kupata wapi mashauri yenye kutegemeka tunapokabili maamuzi muhimu? [Mruhusu ajibu. Soma Methali 3:5, 6.] Makala hii inakazia hekima inayotoka kwa Mungu ya kufikiria matokeo kabla ya kufanya maamuzi.” Onyesha makala iliyo kwenye ukurasa wa 8.
Amkeni! Sept.
“Je, unafikiri Mungu alikusudia wanadamu wateseke kwa sababu ya upungufu wa chakula ambao umeenea duniani leo? [Mruhusu ajibu.] Ona jinsi anavyokusudia kutatua tatizo hilo. ” [Soma Zaburi 72:16.] Makala hii inaeleza jinsi Mungu atakavyorudisha Paradiso duniani.” Onyesha makala iliyo kwenye ukurasa wa 7.
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Katika nyakati hizi zenye msukosuko, watu wengi wanahangaikia wakati ujao. Ni nini kinachokusaidia kuwa na mtazamo mzuri? [Mruhusu ajibu.] Angalia ahadi hii ya Biblia. [Soma Isaya 65:17.] Gazeti hili linaeleza sababu nzuri za kuwa na matarajio mazuri kuhusu wakati ujao.”
Amkeni! Okt.
“Intaneti ni muhimu sana, lakini pia ina hatari fulani kwa watoto. Unafikiri tunaweza kuwalindaje watoto? [Mruhusu ajibu.] Tafadhali ona wazo hili. [Soma na ufafanue Methali 18:1.] Hii ni mojawapo ya kanuni sita za Biblia ambazo zinazungumziwa katika makala hii za kuwasaidia wazazi wawalinde watoto wao.” Onyesha makala iliyo kwenye ukurasa wa 8.