Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Ago. 15
“Tungependa kupata maoni yako kuhusu kile ambacho Yesu alisema. [Soma Mathayo 5:5.] Ahadi hii itakapotimizwa unafikiri hali duniani zitakuwa kama zilivyo sasa? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha kupitia Biblia jinsi Yesu atakavyobadilisha dunia. Pia linaeleza kuhusu wale watakaoishi duniani.”
Amkeni! Ago.
“Unafikiri tutawaona tena wapendwa wetu waliokufa? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi anayotoa Yesu kuhusu wafu. [Soma Yohana 5:28, 29.] Makala hii inaeleza kupitia Biblia kile kinachotupata tunapokufa.” Zungumzia makala inayoanza kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Watu wengi leo wametamaushwa na dini. Unafikiri kuwa mwanadini kunasaidia mtu awe bora zaidi? [Mruhusu ajibu.] Chunguza Biblia ilitabiri watu watatafuta nini katika dini siku hizi za mwisho.” [Soma 2 Timotheo 4:3, 4.] Gazeti hili linaeleza jinsi ibada ya kweli inavyomletea Mungu heshima na inavyotufaidi.”
Amkeni! Sept.
“Watu wengi hushangaa kama kuamini Mungu kunapatana na sayansi. Unaonaje? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Waebrania 3:4.] Toleo hili la pekee la Amkeni! linachunguza uthibitisho ambao umewafanya wanasayansi wengine kuamini kuna Muumba.”