Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Ago.15
“Baada ya kifo cha mpendwa, watu wengi hujiuliza ni jambo gani ambalo hutukia mtu anapokufa. Unafikiri tunaweza kufahamu kifo ni nini? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza yale ambayo Biblia inasema kuhusu hali ya wafu. Pia, linazungumzia ahadi ya Mungu ya kuwafufua wapendwa wetu.” Soma Yohana 5:28, 29.
Amkeni! Ago. 22
“Unajua kwamba watu wengi sana wameajiriwa katika biashara ya utalii kuliko katika kazi nyingine yoyote ulimwenguni? [Mruhusu ajibu.] Kusitawi kwa utalii kumeleta faida na hasara. Gazeti hili linazungumzia faida na hasara za biashara ya utalii leo. Pia, linawapa watu ambao hutembelea nchi mbalimbali mapendekezo mazuri.”
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Katika ulimwengu wa leo, watu wengi huzungumzia sifa ya uaminifu lakini hawaionyeshi. Hali ingekuwa bora ikiwa watu wengi zaidi wangekuwa kama rafiki huyu anayezungumziwa hapa, sivyo? [Soma Methali 17:17, kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia manufaa za kuwa waaminifu kwa familia na marafiki wetu.”
Amkeni! Sept. 8
“Huenda umestaajabia ushirikiano uliopo kati ya viumbe. [Taja mfano mmoja katika makala.] Inasikitisha sana kuona kwamba wanadamu hawashirikiani, sivyo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza jinsi Mungu atakavyoleta amani na upatano duniani hivi karibuni.” Soma Isaya 11:9.