Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Je, unakubali kwamba kutii amri hii ya Yesu kunaweza kuongeza furaha katika familia? [Soma Yohana 13:34. Mruhusu ajibu.] Makala hii inaonyesha jinsi mafundisho na mfano wa Yesu unavyomhusu kila mshiriki wa familia.” Onyesha makala iliyo katika ukurasa wa 16 na 17.
Amkeni! Ago.
“Je, unafikiri serikali za wanadamu zitakomesha tatizo la kuongezeka kwa joto duniani? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Yeremia 10:23.] Utafurahia makala hii. Inaonyesha jinsi Mungu atakavyosuluhisha matatizo yanayoikumba dunia.”
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Watu wengi wanajua maneno ya Yesu katika Mathayo 6:9. [Soma.] Hata hivyo, wengi wanaona ni vigumu kumkaribia Mungu akiwa Baba. Unafikiri tunaweza kumkaribia Mungu jinsi gani? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha sifa mbalimbali za Baba yetu wa mbinguni na jinsi tunavyoweza kumjua vizuri.”
Amkeni! Sept.
“Kwa karne nyingi, kumekuwa na ubishi mwingi kuhusu uhai baada ya kifo. Maoni yako ni nini? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Ayubu aliamini. [Soma Ayubu 14:14, 15.] Makala hizi zinaonyesha maoni ya Biblia kuhusu uhai baada ya kifo.”