Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Ago. 15
“Wewe unaonaje? Tunapaswa kuwa waaminifu kwa nani hasa? [Ngoja jibu.] Makala hii inakazia uaminifu kwa Mungu wa kweli. [Onyesha ukurasa wa 5, na usome 2 Samweli 22:26.] Je, unajua kwamba uaminifu kwa Mungu unaweza kuwazuia watu wasiwatendee wengine bila upendo? Nina uhakika kwamba utafurahia kusoma juu ya jambo hilo.”
Amkeni! Ago. 22
“Je, umewahi kufikiri kwamba uchafuzi wa dunia umezidi kiasi cha kwamba hauwezi kukomeshwa? [Ngoja jibu.] Jambo moja linalosababisha uchafuzi ni kwamba watu huwa na zoea la kutupatupa vitu. Yesu aliwafundisha wafuasi wake wasiharibu mali ovyoovyo. [Soma Yohana 6:12.] Gazeti hili linaonyesha jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kuwasaidia watu wasiwe na mwelekeo wa kutupa vitu ovyoovyo.”
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Je, umetambua kwamba katika sehemu nyingi majirani hawajuani kama walivyojuana zamani? [Ngoja jibu.] Yesu alitaja kanuni moja inayoweza kumsaidia mtu kuwa jirani mzuri. [Soma Mathayo 7:12.] Gazeti hili linaonyesha jinsi tunavyoweza kuwa majirani bora na kuwatia wengine moyo kufanya vivyo hivyo.”
Amkeni! Sept. 8
“Siku hizi watu wengi wanahangaikia jinsi maisha yao yatakavyokuwa. [Soma Mhubiri 9:11.] Mwongozo unaofaa unapatikana wapi? [Ngoja jibu.] Watu fulani huamini kwamba namba fulani zinaweza kutabiri wakati ujao. Je, hiyo ndiyo njia ya kujua jinsi maisha yako yatakavyokuwa? Unaweza kupata wapi habari zenye kutegemeka kuhusu wakati ujao? Gazeti hili la Amkeni! linajibu maswali hayo.”