Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Ago. 15
“Watu wengi wanapenda kujifanyia sifa nzuri. Wengine hata hujiuliza watakumbukwaje wanapokufa. Je, umewahi kufikiria jambo hilo? [Ngoja jibu. Kisha usome Mhubiri 7:1.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi tunavyoweza kujifanyia sifa nzuri mbele ya wanadamu na Mungu.”
Amkeni! Ago. 22
“Ikiwa wewe au mshiriki wa familia yako amewahi kudhulumiwa, unajua jinsi jambo hilo linavyoumiza. [Ngoja maelezo.] Toleo hili la Amkeni! lina madokezo yatakayowasaidia wale wanaodhulumiwa. Pia linaeleza ahadi ya Mungu kuhusu wakati ambapo maisha hayatakuwa kamwe na matatizo kama hayo.” Soma Mika 4:4.
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Watu wengi wanaona kwamba dini tofauti ni njia mbalimbali zinazoongoza mahali pamoja. Wengine wanaamini kwamba kuna dini moja tu ya kweli. Je, umefikiria hilo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linazungumzia mfano mmoja wa kale ambao unajibu swali hilo.” Zungumzia Mathayo 13:24-30.
Amkeni! Sept. 8
“Watu wengi leo ni watumwa wa mitindo. Wengine hudhani kwamba mavazi na sura yanakaziwa kupita kiasi. Maoni yako ni nini? [Ngoja jibu.] Gazeti hili la Amkeni! linaeleza maoni yanayofaa kuhusu mitindo.” Soma Wakolosai 3:12.