Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
“Leo, watu hutafuta mashauri kuhusu ndoa na jinsi ya kuelea watoto kutoka katika vyanzo mbalimbali. Wewe unafikiri ni wapi tunapoweza kupata mashauri bora? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia baadhi ya mashauri yenye hekima kuhusu maisha ya familia yanayotolewa na Muumba wa wanadamu.” Someni Zaburi 32:8.
Amkeni! Ago. 22
“Unaonaje, je, ni muhimu akina baba wajihusishe katika maisha ya watoto wao? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia tatizo linalozidi kuongezeka la akina baba kutojihusisha katika maisha ya watoto wao. Pia linaeleza jinsi akina baba wanavyoweza kufanikisha maisha ya watoto wao.” Someni Methali 13:1.
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Sisi sote tunataka kuwa na furaha. Je, unafikiri mambo yanayotajwa hapa kwa kweli yanaweza kuleta furaha? [Someni Mathayo 5:4a, 6a, 10a. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza maana ya maneno hayo yaliyo katika yale Mahubiri ya Mlimani yanayojulikana sana, na pia mambo mengine yanayohitajiwa ili tuwe na furaha.”
Amkeni! Sept. 8
“Inakadiriwa kwamba mtu mmoja kati ya kila watu wanne atapata ugonjwa wa akili wakati fulani maishani mwake. Wengi wetu tunajua mtu fulani aliye na ugonjwa huo. [Fungua makala.] Makala hii inatoa mapendekezo mazuri kuhusu mambo tunayoweza kufanya ikiwa mtu fulani tunayempenda ana ugonjwa huo.”