Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Novemba 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili tofauti, moja la kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15 na jingine la Amkeni! Oktoba 22. Katika onyesho moja, eleza jinsi kazi yetu ya ulimwenguni pote inavyotegemezwa.—Ona Mnara wa Mlinzi ukurasa wa 2, au Amkeni! ukurasa wa 5.
Dak. 15: Watu Waliounga Mkono Ibada ya Kweli—Zamani za Kale na Leo. Hotuba inayotegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2002, ukurasa wa 26-30.
Dak. 20: “Msaidie Mwangalizi Wenu wa Funzo la Kitabu la Kutaniko.”a Itolewe na mzee ambaye ni Mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko. Mnapozungumzia fungu la 3, tia ndani maelezo ya kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 70. Pongeza kutaniko kwa njia hususa ambazo limeunga mkono mpango wa funzo la kitabu, na kwa fadhili ueleze sehemu zozote ambazo zahitaji kufanyiwa maendeleo.
Wimbo 114 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Zungumzia sanduku “Habari Nzuri Sana ya Kusoma!”
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee anayestahili.
Dak. 25: “Vichwa vya Familia—Dumisheni Ratiba Nzuri ya Kiroho.” Baada ya utangulizi mfupi unaotegemea fungu la 1-3, zungumzia fungu la 4-13 pamoja na wasikilizaji. Wakati ukiruhusu soma fungu la 7, 8, 11, na 12. Hoji mzazi mmoja au wawili. Ni nini ambacho kimesaidia familia yao iwe na ratiba nzuri ya utendaji wa kiroho? Imebidi wafanye jitihada gani? Wamenufaikaje? Malizia kwa maelezo mafupi yanayotegemea fungu la 14.
Wimbo 31 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wenzi wa ndoa wanaohubiri pamoja shambani wanaonyesha jinsi ya kutumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 ya kutoa magazeti ya Novemba 1 na Novemba 8. Mume anatoa gazeti la Mnara wa Mlinzi, na mke wake anatoa Amkeni!
Dak. 15: “Julisha Ukweli Kuhusu Yesu.”b Tia ndani maelezo ya kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 278. Tia moyo wote wabebe kitabu hicho kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo kwa ajili ya sehemu “Shule Inayotuzoeza Kufanya Kazi Muhimu Zaidi Maishani.”
Dak. 20: “Pendezwa na ‘Mayatima.’” Anza kwa utangulizi wa dakika tatu kuhusu jinsi Yehova anavyowaona mayatima, ukitegemea fungu la 1 na kichapo Insight, Buku la 1, ukurasa wa 816. Zungumzieni mafungu yaliyobaki ya makala hiyo kwa maswali na majibu. Taja njia zinazofaa ambazo wengine wanaweza kuwasaidia na kuwatia moyo. Mnapozungumzia fungu la 3-4, tia ndani maelezo mafupi kutoka gazeti la Amkeni! la Oktoba 8, 1995, ukurasa wa 8-9.
Wimbo 142 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 2
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Novemba. Pitia kifupi utoaji unaoweza kutumiwa unapotoa kitabu Mtu Mkuu Zaidi.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Juni 1998, ukurasa wa 8.
Dak. 12: Mahitaji ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 25: “Shule Inayotuzoeza Kufanya Kazi Muhimu Zaidi Maishani.” Mazungumzo na wasikilizaji yaongozwe na mwangalizi wa shule. Chochea akina ndugu watazamie kwa hamu programu mpya ya shule ambayo itaanza Januari. Kazia mambo mbalimbali yaliyotajwa katika “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2003,” katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2002. Eleza matakwa ya kujiunga na shule, kama yanavyoonyeshwa katika kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 282, na uwatie moyo wale ambao bado hawajajiandikisha wafanye hivyo kama wanastahili.
Wimbo 127 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.