Matangazo
◼ Januari: Kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya 1988 chenye kurasa 192 chaweza kutolewa. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani vyenye kurasa 192 yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Februari: Kitabu kipya Mkaribie Yehova. Makutaniko ambayo bado hayana kitabu hiki yanaweza kutumia kitabu Creation au Ufunuo Upeo Wao. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee yapaswa kufanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu waliopendezwa, jitahidi kuwaachia kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli na kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa ikiwa watu hao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka.
◼ Kuanzia Februari, na kabla ya Machi 2, kichwa kipya cha hotuba ya waangalizi wa mzunguko kitakuwa “Kukombolewa Kutokana na Ulimwengu Wenye Giza.”
◼ Makutaniko yapaswa kufanya mipango ya kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu Jumatano, Aprili 16, baada ya jua kutua. Ingawa hotuba yaweza kuanza mapema, kupitishwa kwa mifano hakupaswi kuanza mpaka jua litue. Chunguzeni vyanzo vya habari vya kwenu ili mjue wakati ambapo jua litatua katika eneo lenu. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba moja la Ufalme, labda kutaniko moja au makutaniko zaidi yanaweza kutumia jengo jingine jioni hiyo. Inapowezekana, twadokeza kuwe na angalau dakika 40 hivi katikati ya vipindi ili wote wanufaike kikamili na pindi hiyo. Hali za msongamano na maegesho ya magari zapasa kufikiriwa, kutia ndani kusafirisha watu. Baraza la wazee lapaswa kuamua ni mipango gani itafaa kutaniko lenu.
◼ Kuanzia na toleo hili, orodha ya vichapo vipya vinavyopatikana haitachapishwa tena katika Huduma Yetu ya Ufalme. “Tangazo kwa Makutaniko Yote” lenye habari hii litaendelea kutumwa kwa kila kutaniko kila mwezi. Mnakumbushwa kuwa, “Tangazo kwa Makutaniko Yote” likipokewa, mnapaswa kutangaza kwenye Mkutano wa Utumishi utakaofuata vichapo ambavyo huenda kutaniko lenu linavihitaji. Kisha tangazo laweza kuwekwa kwenye ubao wa matangazo. Baada ya hapo, mtumishi wa vitabu anapaswa kuliweka kwenye faili yake.