Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/03 uku. 3
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwahubiria Watu Wanaozungumza Lugha ya Kigeni
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Dumisha Hali Nzuri ya Kiroho Unapotumikia Kwenye Eneo la Kigeni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 1/03 uku. 3

Sanduku La Swali

◼ Kikundi kinachosema lugha ya kigeni kinapaswa kuanzishwa wakati gani?

Eneo la kutaniko linapokuwa na watu wengi wenye kuongea lugha ya kigeni, wazee wanapaswa kufanya yale wanayoweza ili kupanga kazi ya kuhubiri katika lugha hiyo. (km 2/98 uku. 3-4) Huenda ikawa kwamba watu wanaosema lugha ya kigeni wametapakaa kote katika maeneo ya makutaniko mawili au zaidi katika ujirani. Ikiwa hivyo, mwangalizi au waangalizi wa mzunguko watatoa mwelekezo unaohitajiwa, wakisaidia makutaniko yanayohusika yashirikiane katika kazi ya kuhubiri. Mara kwa mara, hotuba ya watu wote au Funzo la Mnara wa Mlinzi laweza kupangwa ili kuona ni watu wangapi wanaohudhuria mikutano ya lugha hiyo ya kigeni.

Kikundi cha lugha ya kigeni chaweza kuanzishwa wakati matakwa yafuatayo yanapotimizwa: (1) Kuna wahubiri au watu wenye kupendezwa ambao wanaelewa habari njema katika lugha ya kigeni. (2) Kuna mzee au mtumishi wa huduma anayestahili ambaye anaweza kuongoza angalau mkutano mmoja kila juma. (3) Baraza la wazee liko tayari kutegemeza kikundi hicho. Matakwa hayo yanapotimizwa, wazee wanapaswa kujulisha ofisi ya tawi ili kikundi hicho kitambuliwe rasmi na maagizo zaidi yatolewe.

Vikundi vingi huanza kwa kufanya Funzo la Kitabu la Kutaniko kila juma. Baadaye, wazee wanaweza kukubali kuongeza mikutano mingine, kama vile Hotuba ya Watu Wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi. Hotuba Namba 2, 3, na 4 za Shule ya Huduma ya Kitheokrasi zaweza kutolewa katika darasa tofauti ikiwa kuna mzee au mtumishi wa huduma anayeifahamu lugha hiyo vizuri na ambaye anaweza kutoa mashauri. Lakini, kikundi hicho kitajiunga na kutaniko kusikiliza hotuba ya sifa ya usemi, hotuba ya maagizo, mambo makuu ya usomaji wa Biblia, na Mkutano wa Utumishi. Pia kikundi hicho kinaweza kuwa na mikutano yao ya utumishi wa shambani.

Wote katika kikundi hicho watashirikiana sana na baraza la wazee. Wazee wanapaswa kutoa mwelekezo na kuchukua hatua ya kutunza mahitaji ya kikundi hicho. Mwangalizi wa mzunguko anapotembelea kutaniko linalotegemeza kikundi hicho, atapanga pia kuhubiri pamoja na kikundi hicho ili kukijenga kiroho. Kwa baraka za Yehova, huenda kikundi hicho cha lugha ya kigeni kikawa kutaniko baada ya muda fulani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki