Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Februari: Kitabu kipya Mkaribie Yehova kitatolewa. Makutaniko ambayo bado hayana kitabu hiki yanaweza kutumia kitabu Creation au Upeo wa Ufunuo. Machi: Toa kitabu Ujuzi na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, na waliohudhuria Ukumbusho au mikutano mingine ya kitheokrasi lakini ambao hawashirikiani kwa ukawaida na kutaniko, jitahidi kuwaachia kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa ikiwa watu hao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko mnamo Machi 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Baada ya ukaguzi kufanywa, tangazieni kutaniko baada ya kusoma ripoti ya hesabu. Soma barua zozote za shukrani za michango ambayo kutaniko limetoa kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote na michango mingineyo ya tengenezo.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa kuna wowote wanaoshindwa kutimiza takwa la saa, wazee wapaswa kupanga ili kuwasaidia. Madokezo yapatikana katika barua za kila mwaka za S-201. Pia angalieni fungu la 12-20 la nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986.
◼ Kichwa cha hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ya 2003 kitakuwa “Je, Saa ya Hukumu ya Babiloni Imefika?” Ona tangazo kama hilo kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2002.
◼ Kwa kuwa mpango wa kuandikisha magazeti uliondolewa, makutaniko yanapaswa kuwapa wahubiri magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yanapopatikana. Jambo hili litawawezesha wahubiri kupata magazeti yao na pia kuwa na nafasi ya kuyasoma kabla ya kuyatumia katika utumishi wa shambani.
◼ Wanafunzi wa darasa la 12 la Kenya la Shule ya Mazoezi ya Kihuduma walihitimu Novemba 3, 2002. Wanafunzi hao 24 walitoka Ethiopia, Kenya, Sudan, Tanzania, na Uganda.