Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Februari 24, 2003. Mwangalizi wa shule atashughulikia pitio la dakika 30 linalotegemea habari iliyozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa juma la kuanzia Januari 6 hadi Februari 24, 2003. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejezo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Kweli au Si Kweli: Siri ya kusoma kwa usahihi ni kuhakikisha kwamba kile unachosoma kinasikika kuwa sahihi, hata kama kinatofautiana kidogo na kile kilichoandikwa. Eleza. [be uku. 83]
2. Jaza Nafasi Zilizopo: Ili kusoma kwa usahihi, lazima mtu ․․․․․․․․, ․․․․․․․․, ․․․․․․․․ na afanye hivyo kwa sauti. [be uku. 85]
3. Kwa nini ni jambo la maana kusema kwa njia inayoeleweka wazi? (1 Kor. 14:8, 9) [be uku. 86]
4. Ni yapi baadhi ya mambo ambayo hufanya usemi usiwe dhahiri, na twaweza kufanya nini ili tuseme kwa njia inayoeleweka wazi zaidi? [be uku. 87-88]
5. Ni maneno gani yaliyotumiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika miezi miwili iliyopita ambayo unahitaji kujizoeza kuyatamka kwa usahihi? [be uku. 92]
HOTUBA NA. 1
6. Kweli au Si Kweli: Macho yetu yanaweza kutusaidia kusikiliza. Eleza. [be uku. 14]
7. Jaza Nafasi Zilizopo:․․․․․․․․, ․․․․․․․․, na ․․․․․․․․ hutumika kama ishara za wakati kutoka kwa Mungu. [si uku. 279 fu. 7]
8. Jaza Nafasi Zilizopo: Katika Biblia, usemi “siku” waweza kumaanisha kipindi cha muda wa saa ․․․․․․․․, saa ․․․․․․․․, miaka ․․․․․․․․, au ․․․․․․․․, ikitegemea muktadha. [si uku. 279 fu. 8]
9. Mifano ya Hana, Marko, na Eliya yaweza kutusaidiaje kushinda kivunja-moyo kwa mafanikio? Twaweza kutumiaje mifano hiyo kuwasaidia wengine? [w01 2/1 uku. 20-23]
10. Kuelewa baadhi ya michezo ya zamani ya riadha kunafunuaje maana ya mistari kadhaa ya Biblia? Habari hiyo yapaswa kuathirije maisha yetu? [w01 1/1 uku. 28-31]
USOMAJI WA BIBLIA KILA JUMA
11. Kweli au Si Kweli: Kwa kuwa Ufalme wa Mungu ulisimamishwa mbinguni mwaka wa 1914, haifai tena kusali, “Acha ufalme wako uje.” (Mt. 6:10) Eleza. [be uku. 279; w96 6/1 uku. 31]
12. Kweli au Si Kweli: Maneno ya Yesu kwenye Mathayo 11:24 humaanisha kwamba wale ambao Yehova aliwaharibu kwa moto katika Sodoma na Gomora watafufuliwa. Eleza.
13. Chagua Jibu Sahihi: Mtumwa mwaminifu na mwenye busara anayetajwa na Yesu kwenye Mathayo 24:45-47 ni (a) Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova; (b) Wakristo wote watiwa-mafuta wakiwa kikundi waliopo duniani.; (c) Yesu Kristo mwenyewe. Mtumwa huyo huandalia ‘watumishi wa nyumbani,’ chakula cha kiroho kwa wakati unaofaa ambao wanawakilisha (a) watiwa-mafuta wakiwa mmoja-mmoja; (b) kondoo wengine; (c) wasomaji wote wa vichapo vya Kikristo. Bwana-mkubwa alimweka mtumwa huyo kusimamia mali zake zote mwaka wa (a) 1914; (b) 33 W.K.; (c) 1919.
14. Chagua Jibu Sahihi: Wavu unaozungumziwa katika mfano wa Yesu kwenye Mathayo 13:47-50 umetia ndani kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta na (a) Ufalme wa Mungu wa Kimesiya; (b) waandamani wao, wale kondoo wengine; (c) Jumuiya ya Wakristo.
15. Kulingana na maneno ya Yesu kwenye Mathayo 5:24, ufanyeje ukiona kwamba umemuudhi mwabudu mwenzako? [g96 2/8 uku. 26-27]