Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • be funzo 3 uku. 89-uku. 92 fu. 5
  • Matamshi Mazuri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matamshi Mazuri
  • Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Tulitumie Jina la Mungu Ikiwa Hatujui Linavyopaswa Kutamkwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Jina la Mungu—Maana Yalo na Linavyotamkwa
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Je, Ni “Yehova” au Ni “Yahweh”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Nufaika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1996—Sehemu ya 3
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
be funzo 3 uku. 89-uku. 92 fu. 5

SOMO LA 3

Matamshi Mazuri

Unahitaji kufanya nini?

Tamka kila neno vizuri. Kunatia ndani (1) kutamka maneno kwa kutumia sauti zinazofaa, (2) kukazia silabi inayofaa au zinazofaa na, (3) katika lugha nyingi, kufuata alama za matamshi.

Kwa Nini Ni Muhimu?

Matamshi mazuri hufanya ujumbe wetu uheshimiwe. Yanafanya mtu asikilize ujumbe wetu badala ya kufikiria jinsi tunavyotamka maneno vibaya.

SI WAKRISTO wote wamesoma sana elimu ya kilimwengu. Hata mtume Petro na mtume Yohana walitajwa kuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.” (Mdo. 4:13) Lakini, ni muhimu kuepuka kukengeusha akili za watu kutoka kwenye kweli ya Biblia kwa kutamka maneno vibaya.

Mambo ya Kufikiria. Hakuna kanuni fulani hususa za matamshi zinazoweza kutumiwa na lugha zote. Lugha nyingi huandikwa kwa herufi za alfabeti. Mbali na alfabeti ya Kilatini, kuna alfabeti za Kiarabu, Kiebrania, Kigiriki, na Kirusi. Kichina huandikwa kwa herufi zenye sehemu kadhaa badala ya alfabeti. Kwa kawaida herufi hizo husimamia neno au sehemu ya neno. Ingawa Kijapani na Kikorea zinatumia herufi za Kichina, herufi zao hutamkwa kwa njia tofauti kabisa na huenda hata zisiwe na maana moja.

Katika lugha zinazotumia alfabeti, matamshi mazuri humaanisha kutaja kila herufi au herufi kadhaa kwa sauti inayotakikana. Ikiwa lugha kama hiyo ina kanuni za wazi za kufuata, kama vile Kigiriki, Kihispania, na Kizulu, haiwi vigumu kutamka maneno vizuri. Lakini, maneno ya lugha za kigeni yanaweza kuingiza katika lugha nyingine matamshi ya lugha hizo za kigeni. Basi, inakuwa kwamba kila herufi au herufi kadhaa zinaweza kutamkwa kwa njia nyingi au nyakati nyingine hata zisitamkwe kamwe. Huenda ikawa lazima kukumbuka matamshi kama hayo na kuyatumia mara nyingi unapoongea. Katika Kichina ni lazima mtu akariri moyoni matamshi ya maelfu ya herufi. Katika lugha nyinginezo, ubadilifu wa sauti hubadili maana ya neno. Mtu anaweza kueleweka vibaya asipozingatia jambo hilo.

Ikiwa lugha fulani imefanyizwa kwa silabi, ni vizuri kuweka mkazo unaotakikana kwenye silabi inayofaa. Lugha nyingi za aina hiyo zina njia za kawaida za kutia mkazo. Kama neno linapaswa kutamkwa kwa njia tofauti, alama ya matamshi inaweza kuwekwa kwenye neno hilo. Hiyo hufanya iwe rahisi kutamka maneno. Lakini, inakuwa vigumu kutamka maneno kama hakuna utaratibu maalumu wa kufuata. Katika hali kama hizo ni lazima ukariri moyoni jinsi ya kutamka kila neno vizuri.

Kuna lugha ambazo hutumia sana alama za matamshi. Baadhi ya alama hizo huonyeshwa juu ya herufi au chini yake. Ufuatao ni mfano wa herufi zenye alama za matamshi: ā, ō, é, ù, ĩ, ũ, ḥ, ị, ụ. Nyakati nyingine alama hizi za matamshi huandikwa na nyakati nyingine haziandikwi na katika hali hiyo msomaji mwenyewe huzitia kulingana na muktadha wa neno analosoma. Ikiwa alama za matamshi hazijaonyeshwa, msomaji anahitaji kujitayarisha vizuri sana ikiwa ana mgawo wa kusoma mbele ya watu.

Kuna mambo yanayohusu matamshi ambayo tunapaswa kuepuka. Kutamka maneno kupita kiasi kunaweza kufanya ionekane unajifanya, au hata kujionyesha. Ndivyo ilivyo na kutumia matamshi ambayo kwa ujumla hayatumiwi tena. Msemaji atakuwa akijielekezea tu fikira akifanya hivyo. Kwa upande mwingine, tusipite kiasi kwa kuongea na kutamka maneno kwa uzembe. Baadhi ya mambo hayo tayari yametajwa katika somo lenye kichwa “Kusema kwa Njia Inayoeleweka Wazi.”

Maneno fulani ya lugha moja yanaweza kutamkwa tofauti katika nchi tofauti-tofauti, au hata yatamkwe tofauti katika sehemu mbalimbali za nchi ileile moja. Mtu wa nchi nyingine anaweza kusema lugha ileile moja kwa matamshi tofauti. Kamusi zinaweza kuorodhesha njia mbalimbali zinazokubalika za kutamka neno. Ikiwa mtu hakupata elimu ya kilimwengu au lugha anayosema si yake ya asili, anaweza kufaidika sana akiwasikiliza kwa makini wale wanaozungumza lugha hiyo vizuri na kujaribu kutamka maneno jinsi wanavyotamka. Sisi Mashahidi wa Yehova tunataka kuzungumza kwa njia inayotukuza ujumbe wetu na kwa njia ambayo watu katika eneo letu wanatuelewa kwa urahisi.

Katika mazungumzo ya kawaida, inafaa kutumia maneno ambayo unafahamu vizuri. Kwa kawaida matamshi huwa si tatizo unapozungumza. Lakini, unaposoma kwa sauti unaweza kupata maneno ambayo kwa kawaida hutumii katika mazungumzo yako. Na Mashahidi wa Yehova husoma sana kwa sauti. Sisi husomea watu Biblia tunapohubiri. Ndugu wengine hupewa migawo ya kusoma mafungu wakati wa Funzo la Mnara wa Mlinzi au kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko. Ni muhimu tusome kwa usahihi na tusikengeushe akili za watu kutoka kwenye ujumbe huo kwa kutamka maneno vibaya.

Je, unashindwa kutamka majina fulani katika Biblia? Katika Kiswahili, kwa ujumla ni silabi ya pili kutoka mwisho ndiyo inapaswa kutamkwa kwa mkazo.

Njia za Kufanya Maendeleo. Watu wengi hawajui kwamba wana tatizo la matamshi. Mwangalizi wa shule akikutajia mambo fulani kuhusu matamshi ambayo unahitaji kurekebisha, thamini fadhili yake. Baada ya kutambua tatizo, unawezaje kufanya maendeleo?

Kwanza, unapokuwa na mgawo wa kusoma kwa sauti, chunguza kamusi ikiwa kamusi za lugha yenu zina miongozo ya jinsi ya kutamka maneno. Tafuta maneno usiyoyafahamu. Kama hujazoea kutumia kamusi, fungua kurasa za kwanza zenye maelezo kuhusu alama zinazotumika katika kamusi hiyo, au mwombe mtu akufafanulie alama hizo. Kamusi za lugha nyinginezo huonyesha jinsi ya kutamka maneno. Kamusi hizo huonyesha sauti unazopaswa kutumia unapotamka vokali fulani na konsonanti fulani. Nyakati nyingine kuna maneno ambayo yanaweza kutamkwa kwa njia tofauti-tofauti ikitegemea muktadha. Rudia kutaja kwa sauti mara kadhaa neno lile unalolitafuta kabla ya kufunga kamusi.

Njia ya pili inayoweza kuboresha matamshi yako ni kusoma mbele ya mtu mwingine, mtu ambaye hutamka maneno vizuri, na umwambie akukosoe unapokosea.

Njia ya tatu ya kuboresha matamshi ni kusikiliza kwa makini wasemaji wazuri. Ikiwa kuna kaseti za vichapo vyetu, zitumie. Unaposikiliza, chunguza maneno yanayotamkwa kwa njia tofauti na jinsi ambavyo wewe ungeyatamka. Uyaandike kisha ufanye mazoezi ya kuyatamka. Baada ya muda, hutakuwa ukitamka maneno vibaya, na hiyo itakusaidia sana uwe msemaji bora.

JINSI YA KUBORESHA MATAMSHI

  • Omba mtu ambaye husoma vizuri akusikilize na kukushauri.

  • Ona jinsi wasemaji wazuri wanavyotamka maneno; linganisha na jinsi unavyotamka maneno.

  • Jifunze kutumia kamusi.

MAZOEZI: Chunguza jinsi neno lolote usilolifahamu vizuri linavyotamkwa unaposoma Zaburi 83 au sehemu fulani ya Biblia ambayo unaona ni ngumu kusoma. Omba mashauri ya mtu anayejua lugha hiyo vizuri. Chunguza ni silabi zipi zinazopaswa kukaziwa katika majina unaposoma mistari hiyo; soma kwa sauti kila jina unalopata. Kisha soma sehemu hiyo yote kwa sauti.

Nahitaji kufanya mazoezi ya kutamka vizuri maneno haya

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․ ․․․․․․․․․․․․․․․․․․․․

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki