Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, na waliohudhuria Ukumbusho au mikutano mingine ya kitheokrasi lakini ambao hawashirikiani kwa ukawaida na kutaniko, jitahidi kuwaachia kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa ikiwa watu hao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Toa kitabu Ujuzi au broshua Anataka. Ikiwa wenye nyumba tayari wana vichapo hivyo, tumia broshua nyingine zinazofaa ambazo ziko kutanikoni. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai–Wewe Waweza Kulipataje?, Roho za Wafu, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” na kijitabu Roho Zisizoonekana.
◼ Kuanzia Juni, beji za kusanyiko la wilaya la 2003 zitatiwa ndani ya upakizi wa vichapo wa kutaniko. Hamtahitaji kuziagiza. Beji zitapakiwa kwa mafungu ya kadi 25 ikitegemea ukubwa wa kutaniko. Ikiwa kutaniko linahitaji beji zaidi, zapasa kuagizwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Vifuko vya beji vya plastiki vyaweza kuagizwa kwa ajili ya yeyote kutanikoni anayevitaka.
◼ Ni lazima ofisi ya tawi iwe na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kutakuwa na badiliko lolote, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko yapaswa kujaza Fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29) na kuituma kwa ofisi ya tawi haraka iwezekanavyo. Fomu hiyo yapasa kutumwa ikiwa kuna mabadiliko yoyote katika namba ya simu ya eneo lao.
◼ Waandishi wa kutaniko wanapaswa kuwa na fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b). Fomu hizo zaweza kuagizwa kupitia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Wekeni angalau akiba ya mwaka mmoja. Chunguzeni fomu zote za ombi la painia wa kawaida ili kuhakikisha kwamba zimejazwa vizuri. Ikiwa wenye kuzijaza hawakumbuki vizuri tarehe waliyobatizwa, wanapaswa kukadiria tarehe hiyo na kuiandika mahali.
◼ Iwapo wakati wowote utapanga kwenda nchi nyingine, na utake kufahamishwa tarehe, wakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kusanyiko la mzunguko au la wilaya, uliza ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Utapata orodha ya anwani za ofisi ya tawi katika ukurasa wa mwisho wa Yearbook au kitabu kingine chochote cha karibuni cha Sosaiti.
◼ Kampeni yetu ya kila mwaka ya maeneo yaliyo mbali itakuwa Julai 1 hadi Septemba 30, 2003. Makutaniko au vikundi vya wahubiri wanaotaka kushiriki wanapaswa kuomba eneo hususa lisilogawiwa mtu kutoka kwenye orodha iliyotumwa kwenye makutaniko. Tarehe ya mwisho ya kufanya hivyo ni Mei 20, 2003. Makutaniko ambayo hayamalizi maeneo yao kwa ukawaida yanaweza kupanga kuhubiri maeneo yasiyohubiriwa mara nyingi katika kipindi hicho. Hakuna haja ya kuandikia ofisi ya tawi ili kuomba utumikie kama painia wa pekee wa muda katika kipindi hicho kwa sababu ni wachache tu wanaopendekezwa na mwangalizi wa mzunguko. Ikiwa unataka kuwa painia wa pekee wa muda, tafadhali wasiliana na mwangalizi wa mzunguko kupitia Halmashauri ya Utumishi ya kutaniko lenu.
◼ Jina sahihi la Jumba la Ufalme lililowekwa wakfu huko Uganda ni Kyoga wala si Kyoka kama ilivyoonyeshwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari.