Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/03 uku. 4
  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Vichwa vidogo
  • HOTUBA NA. 1
  • USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 4/03 uku. 4

Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Aprili 28, 2003. Mwangalizi wa shule atashughulikia pitio la dakika 30 linalotegemea habari iliyozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa juma la kuanzia Machi 3 hadi Aprili 28, 2003. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Ni mambo gani yanayoweza kusababisha ukosefu wa ufasaha? [be uku. 93]

2. Kweli au Si Kweli: Twapaswa kuepuka kutua, kwa kuwa kufanya hivyo kwaweza kufanya akili za watu zitangetange na kuwapa fursa ya kutukatiza. Eleza.

3. Kwa nini mtu anayehutubia watu au kusoma mbele ya watu anapaswa kukazia maana kwa njia inayofaa? (Neh. 8:8) [be uku. 101]

4. Mtu anawezaje kujifunza kukazia maana kwa njia inayofaa? [be uku. 102-103]

5. Ni mawazo gani makuu yanayopaswa kukaziwa mtu anaposoma kichapo kwa sauti kwenye funzo la Biblia au kwenye mkutano wa kutaniko? [be uku. 105]

HOTUBA NA. 1

6. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kuwazoeza watoto wao “wapate kusikia na kujifunza” kwenye mikutano ya Kikristo? (Kum. 31:12) [be uku. 16]

7. Paradiso ya kiroho ni nini? [w01 3/1 uku. 8-10]

8. Mithali 8:1-3 yaonyeshaje kwamba hekima ya Mungu inapatikana kwa wote, na kulingana na Wakolosai 2:3, yaweza kupatikana wapi? [w01 3/15 uku. 25, 28]

9. Twaweza kutangazaje jina la Mungu? (Yoh. 17:6) [be uku. 273-275]

10. Ni mambo gani muhimu ambayo watu wanahitaji kujua kuhusu “habari njema ya ufalme”? (Mt. 24:14) [be uku. 279-280]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. (a) Katika karne ya kwanza, “kitu chenye kuchukiza” kilichotajwa kwenye Marko 13:14 kilikuwa nini? (b) Ni nini maana ya maneno “kimesimama ambapo hakipaswi”?

12. Gospeli ya Luka inathibitishaje kwamba Yesu alikuwa mrithi wa kiasili wa kiti cha ufalme cha Daudi? (Luka 3:23-38) [w92 10/1 uku. 9 fu. 3]

13. Maneno ya Yesu kwenye Luka 12:2 yanamaanisha nini?

14. Kwa nini itikio la malaika katika mfano wa Yesu wa sarafu iliyopotea ni lenye kusifika? (Luka 15:10) Mfano wao wapaswa kuwa na matokeo gani kwetu?

15. Ni maagano gani mawili yanayotajwa kwenye Luka 22:29?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki