Kuthamini Rehema za Mungu
1 Kabla ya kuwa Mkristo, mtume Paulo alipinga vikali kuenea kwa Ukristo. Hata hivyo, alionyeshwa rehema kwa sababu alitenda kwa kutojua. Yehova alimwonyesha Paulo fadhili isiyostahiliwa, akampa mgawo wa kuhubiri. Aliuthamini sana mgawo huo. (Mdo. 26:9-18; 1 Tim. 1:12-14) Kuthamini rehema za Yehova kulimchochea Paulo ajitahidi kabisa kutimiza huduma yake.—2 Kor. 12:15.
2 Mungu ametuonyesha rehema sisi pia kwa kutupa huduma. (2 Kor. 4:1) Sawa na Paulo, sisi pia tunaweza kuthamini rehema ambazo tumeonyeshwa kwa kujitahidi kuwasaidia wengine wafanye maendeleo ya kiroho. Njia moja ya kufanya hivyo ni kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia.
3 Kuanzisha Mafunzo ya Biblia: Njia moja ya kuanzisha mafunzo ya Biblia ni kuwapelekea watu magazeti kwa ukawaida. Tunapowatembelea kwa ukawaida watu hao, tunapata kujua vizuri zaidi mahangaiko yao. Mwishowe, makala katika gazeti moja inaweza kutumiwa kuanzisha funzo la Biblia katika broshua Anataka. Katika ziara za baadaye, huenda ikawezekana kuendeleza mazungumzo katika broshua Anataka unapompelekea magazeti.
4 Sala na Jitihada Zahitajiwa: Sala pamoja na jitihada nyingi zitaboresha kazi yetu ya kuhubiri. Dada mmoja painia aliyekuwa na funzo moja la Biblia alimwomba Yehova ambariki apate mafunzo zaidi. Pia alitenda kupatana na sala zake. Alichunguza huduma yake na kugundua kwamba hakuwa akiwatajia watu mpango wa kujifunza Biblia alipokuwa akifanya ziara za kurudia. Alianza kufanya hivyo na muda si muda akapata mafunzo mengine mawili.
5 Tuna pendeleo kubwa la kushiriki katika kuhubiri “habari njema ya fadhili isiyostahiliwa ya Mungu.” (Mdo. 20:24) Kuthamini rehema za Mungu na kutuchochee kuwa wenye bidii katika kuwasaidia wengine wafaidike na fadhili isiyostahiliwa ya Yehova.