Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Julai 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4, panga kuwe na maonyesho mawili ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 15 na Amkeni! la Juni 22 yanayoonyesha jinsi yanavyoweza kutolewa katika eneo la kutaniko lenu. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Mhubiri amweleza mwenye nyumba mpango wa kutoa michango naye mwenye nyumba afurahia kutoa mchango.
Dak. 15: Ibada ya Yehova Inathawabishaje Maisha Yetu? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Ibada ya kweli ni muhimu kwa maisha yenye furaha na kusudi. (1) Hutusaidia tukabiliane na matatizo na mahangaiko ya maisha. (Flp. 4:6, 7) (2) Hutusaidia kusitawisha sifa zinazompendeza Mungu. (2 Pet. 1:5-8) (3) Hutusaidia tutumie wakati na mali zetu kwa njia ya maana. (1 Tim. 6:17-19) (4) Hutupa tumaini hakika la wakati ujao. (2 Pet. 3:13) (5) Hutuwezesha kustawisha uhusiano wa karibu na Yehova. (Yak. 4:8) Eleza jinsi hali ni tofauti kwa wale ambao hawamjui au kumtumikia Yehova.
Dak. 20: “Kuthamini Rehema za Mungu.”a Mnapozungumzia fungu la 3, toa madokezo ya kuanza kumpelekea mtu magazeti kwa ukawaida, yanayopatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1998, ukurasa wa 12. Mwulize mhubiri mmoja au wawili wenye ustadi njia ambazo wameona zikiwa na matokeo katika kuanzisha mafunzo ya Biblia. Watie moyo wote waweke mradi wa kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia.—om uku. 91.
Wimbo 176 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya Hesabu.
Dak. 10 “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tangaza tarehe za kusanyiko la mzunguko linalofuata ikiwa inajulikana. Ikiwa kutaniko litakuwa linahudhuria kusanyiko miezi michache inayofuata, taja kwamba wale wanaotaka kubatizwa wanapaswa kumjulisha mwangalizi-msimamizi. Watie moyo wote wajitahidi sana kualika mafunzo ya Biblia na kuhudhuria vipindi vyote.
Dak. 25: Iga Ujasiri Wao wa Kuhubiri. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Mwabudu Mungu, ukurasa wa 170-171. Waombe wasikilizaji wajibu maswali yaliyo kwenye fungu la 7 na watie ndani maandiko yaliyomo wanapotoa maelezo. Soma maandiko yaliyoteuliwa. Kazia somo tunaloweza kujifunza kutokana na masimulizi hayo na jinsi yanavyotusaidia tuwe na maoni yanayofaa katika mgawo wetu wa kuhubiri.
Wimbo 201 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Julai. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4, panga kuwe na maonyesho mawili ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1 na Amkeni! la Julai 8. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika onyesho moja, mhubiri anafanya hivyo katika mahubiri yasiyo rasmi.
Dak. 15: Kikumbusho na mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Mahubiri ya Vikundi Huleta Shangwe.”b Mnapozungumzia fungu la 3, tia ndani maelezo kutoka katika Sanduku la Swali la Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2001. Mhoji kifupi mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko. Mwulize kuhusu mipango ya utumishi wa shambani ambayo amefanyia kikundi chake cha funzo na jinsi kikundi hicho hunufaika kuhubiri pamoja.
Wimbo 36 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja toleo la vichapo la mwezi huu. Toa onyesho moja au mawili mafupi yanayoweza kutumiwa. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: “Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali.”c Tumia maswali yaliyopo. Mnapozungumzia fungu la 3 ikifaa, onyesha kifupi jinsi ya kuhubiri katika lugha ya kigeni inayosemwa katika eneo lenu ambayo hakuna kutaniko linaloitumia.
Dak. 15: Vijana Wanamsifu Yehova! Hotuba inayotia ndani mazungumzo pamoja na wasikilizaji na mahojiano. Sisi hufurahia kusikia vijana wakitoa maelezo yaliyotayarishwa vizuri mikutanoni. Juhudi zao na maendeleo yao katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi yanafurahisha sana. Wanaonyesha imani ya kweli wanaposhiriki ifaavyo katika huduma. Mwenendo wao humheshimu Yehova. (yb88 uku. 53-54) Maendeleo yao ya kiroho ndiyo msingi wa mapendeleo yao ya utumishi siku zijazo. Wahoji kifupi vijana wawili au watatu Wakristo ambao hushiriki kwa kawaida katika utendaji mbalimbali wa kutaniko. Wapongeze kwa shauku vijana katika kutaniko kwa ajili ya jitihada zao za kumsifu Yehova.
Wimbo 49 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.