Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Septemba: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, na Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Watolee watu wanaopendezwa broshua Anataka, na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Novemba: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Iwapo watu tayari wana vichapo hivyo, kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli au kitabu cha zamani chaweza kutolewa. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Vitabu vifuatavyo vinaweza kutumiwa pia: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.
◼ Kuanzia Septemba 1, 2003, nchi ya Uganda itakuwa na Ofisi ya Tawi.
◼ Ofisi ya tawi haishughulikii maagizo ya vichapo ya mhubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi msimamizi anapaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla ya agizo la kutaniko kutumwa kwenye ofisi ya tawi ili wote ambao wanataka kuagiza kichapo fulani waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali shughulikieni ifaavyo bidhaa za kuagizwa kipekee.
◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyo kwenye ukurasa wa 21-23 wa toleo la Mnara wa Mlinzi, la Aprili 15, 1991, kuhusu kuwatembelea watu waliotengwa na ushirika au waliojitenga, ambao huenda wakaonyesha mwelekeo wa kutaka kurudishwa.
◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ya mwaka wa 2004 itatolewa Jumapili, Aprili 18. Kichwa cha hotuba na muhtasari wa hotuba hiyo zitatangazwa baadaye. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwishoni mwa juma hilo, yatapanga hotuba ya pekee itolewe juma linalofuata. Hotuba ya pekee haipaswi kutolewa kabla ya Aprili 18, 2004 katika kutaniko lolote lile.