Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Oktoba 27, 2003. Mwangalizi wa shule atashughulikia pitio la dakika 30 linalotegemea habari iliyozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa juma la kuanzia Septemba 1 hadi Oktoba 27, 2003. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Ni nini kinachomaanishwa na shauri linalopatikana kwenye 1 Timotheo 2:9 kuhusu kujipamba kwa “mavazi yenye mpangilio mzuri,” na hilo laweza kuwa na matokeo gani tunapotoa hotuba jukwaani na tunapokuwa katika huduma ya shambani? [be uku. 132 fu. 4-5]
2. Kanuni za Biblia katika 1 Yohana 2:15-17; Waefeso 2:2; na Waroma 15:3 zinapasa kuathirije mavazi na mapambo yetu? [be uku. 133 fu. 2-4]
3. Kwa nini utulivu ni muhimu, na mtu anawezaje kuwa mtulivu anapotoa hotuba jukwaani au anapohubiri? [be uku. 135 sanduku; uku. 136 fu. 6, sanduku]
4. Akiwa “shahidi mwaminifu na wa kweli,” Yesu alituwekeaje kielelezo cha kutumia Biblia katika huduma? (Ufu. 3:14) [be uku. 143 fu. 2-3]
5. Twawezaje kuwa stadi zaidi katika kutumia Biblia? (Tito 1:9) [be uku. 144 fu. 1, sanduku]
HOTUBA NA. 1
6. Funzo linahusisha nini, na ni zipi baadhi ya faida za kujifunza Neno la Mungu kwa ukawaida? [be uku. 27 fu. 3; uku. 32 fu. 3]
7. Kulingana na Yakobo 1:5, 6, ni muhimu tufanye nini tunapokabili uamuzi mzito? [w01 9/1 uku. 28 fu. 4]
8. Tarehe za msingi ni nini, na kwa nini ni muhimu sana? [si uku. 282 fu. 27]
9. “Yeye asingiziaye ni mpumbavu” kwa njia gani? (Mit. 10:18) [w01 9/15 uku. 25 fu. 3]
10. Wanadamu watapataje kuthamini kwa ukamili zaidi maoni ya Yehova juu ya wakati katika ulimwengu mpya? [si uku. 283 fu. 32]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Kweli au Si Kweli: Kwenye 1 Wakorintho 2:9, mtume Paulo anazungumzia mambo ambayo Yehova amewatayarishia watu wake waaminifu kuwa urithi. Eleza. [ip-2 uku. 366, sanduku]
12. Ni vishawishi gani vinavyozungumziwa kwenye 1 Wakorintho 10:13, na Yehova ‘hufanyaje njia ya kutokea’? [w91 10/1 uku. 10-11 fu. 11-14]
13. Mfano wa Yesu wa kujitoa husaidiaje Wakristo? (2 Kor. 8:9) [w92 1/15 uku. 16 fu. 10]
14. Sheria ‘imekuwaje mfunzi ikiongoza kwa Kristo’? (Gal. 3:24) [w02 6/1 uku. 15 fu. 11]
15. “Mambo ya msingi ya ulimwengu” ambayo ni lazima tujihadhari nayo ili tusipotoshwe ni yapi? (Kol. 2:8)