Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Watolee watu wanaopendezwa broshua Anataka, na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Novemba: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Iwapo watu tayari wana vichapo hivyo, broshua Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele? au kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli au kichapo cha zamani chaweza kutolewa. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Vitabu vifuatavyo vinaweza kutumiwa pia: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Januari: Kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1988 ambacho huenda kutaniko likawa nacho akibani. Ikiwa kutaniko halina toleo lolote kati ya hayo, tafadhali ulizeni makutaniko yoyote ya karibu kama yana vichapo vyovyote vya ziada ambavyo mnaweza kutumia. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.
◼ Tunafurahi kutangaza kwamba maandiko ya mwaka ya 2004 yatapatikana katika Kiingereza na Kiswahili na makutaniko yanayohitaji kupata andiko la mwaka kutoka katika ofisi ya tawi yanaweza kuagiza. Yana ukubwa wa milimeta 1000 kwa milimeta 350 nayo yatachapwa kwenye karatasi ngumu ya rangi ya mchanga kwa maandishi ya rangi ya bluu.
◼ Nyongeza iliyo katika toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme ni “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2004” na yapasa kuwekwa ili kutumiwa mwaka wote wa 2004.
◼ Ikiwa saa za mkutano za kutaniko lenu zitabadilika Januari 1, mwandishi wa kutaniko apaswa kujulisha Sosaiti mabadiliko hayo kwa kutuma fomu ya Habari Kuhusu Mikutano ya Kutaniko na fomu ya Ombi la Vikaratasi vya Ukaribishaji (S-5). Ikiwa vikaratasi vipya vya ukaribishaji vyahitajiwa vyaweza kuagizwa kwenye fomu hiyohiyo. Vikaratasi vya ukaribishaji vyapaswa kuagizwa angalau majuma 12 kabla ya wakati ambapo vinahitajiwa.