Ratiba Ya Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi Ya 2004
Maagizo
Katika mwaka wa 2004, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaongozwa kulingana na mipango ifuatayo.
VICHAPO VITAKAVYOTUMIWA: Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya [bi12], Mnara wa Mlinzi [w], Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi [be], “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” [si], na Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko [rs].
Shule inapaswa kuanza KWA WAKATI, kwa wimbo, sala, na maneno ya kuwakaribisha wasikilizaji, kisha utaratibu huu unapaswa kufuatwa:
SIFA YA USEMI: Dakika 5. Mwangalizi wa shule, mshauri msaidizi, au mzee mwingine anayestahili atazungumzia sifa moja ya usemi akitumia kitabu cha Shule ya Huduma. (Katika makutaniko yenye wazee wachache, mtumishi wa huduma anayestahili anaweza kutoa hotuba hiyo.) Kama maagizo mengine hayajatolewa, masanduku yaliyo kwenye kurasa ambazo hotuba imetolewa yanapaswa kutiwa ndani. Mazoezi yanayotiwa ndani ya kila somo hayapaswi kushughulikiwa. Mazoezi hayo yamekusudiwa hasa kutumiwa na wanafunzi na pia kutoa ushauri faraghani.
HOTUBA NA. 1: Dakika 10. Hotuba hii inapaswa kutolewa na mzee au mtumishi wa huduma, na habari zitatolewa katika Mnara wa Mlinzi, Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, au “Kila Andiko Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa.” Hotuba hii ya maagizo inapaswa kutolewa kwa dakika kumi bila kuuliza maswali ya kurudia. Lengo la hotuba hii linapaswa kuwa kuzungumzia habari zote zilizoteuliwa, kuonyesha jinsi habari hizo zinavyoweza kutumiwa maishani, na kukazia mambo ambayo yatanufaisha kutaniko. Kichwa cha hotuba kilichoandikwa kwenye ratiba chapaswa kutumiwa. Ndugu wanaogawiwa hotuba hiyo wanatarajiwa kumaliza kwa wakati. Ushauri unaweza kutolewa faraghani inapohitajika.
MAMBO MAKUU YA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 10. Mzee au mtumishi wa huduma anayestahili, anapaswa kutumia dakika sita za kwanza kuonyesha jinsi habari hiyo inavyohusu kutaniko lenu. Anaweza kutoa maelezo kuhusu sehemu yoyote ya usomaji wa Biblia wa juma hilo. Maelezo hayo hayapasi kuwa tu muhtasari wa usomaji huo wa Biblia. Lengo kuu ni kuwasaidia wasikilizaji waelewe ni kwa nini habari hiyo ni yenye faida na jinsi inavyowafaidi. Msemaji anapaswa kuwa mwangalifu asipitishe zile dakika sita alizopewa atoe maelezo yake. Anapaswa kutumia dakika nne zilizobaki kuwapa wasikilizaji nafasi watoe maelezo mafupi (yasiyozidi nusu dakika) kuhusu mambo yaliyowapendeza katika usomaji wa Biblia na jinsi walivyofaidika. Kisha mwangalizi wa shule atawaruhusu wanafunzi watakaotoa hotuba katika shule ya pili au ya tatu kuondoka.
HOTUBA NA. 2: Dakika 4. Ndugu anapaswa kugawiwa usomaji huu. Kwa kawaida sehemu fulani ya Biblia itasomwa. Mara moja kwa mwezi, sehemu fulani katika Mnara wa Mlinzi itasomwa. Mwanafunzi anapaswa kusoma habari aliyogawiwa bila kutoa utangulizi wala maneno ya kumalizia. Sehemu zilizoratibiwa kusomwa hazitakuwa zenye urefu mmoja kila juma, lakini sehemu zote zinapaswa kusomwa kwa dakika nne au chini ya dakika nne. Mwangalizi wa shule anapaswa kuchunguza habari kabla ya kumgawia yeyote, ili kuhakikisha kwamba habari inafaa umri na uwezo wa mwanafunzi. Mwangalizi wa shule atapendezwa hasa kuwasaidia wanafunzi kusoma kwa njia yenye kueleweka, kwa ufasaha, kukazia maana kwa njia inayofaa, kuwa na ubadilifu wa sauti, kutua kwa njia inayofaa, na kusoma kama unavyoongea kwa kawaida.
HOTUBA NA. 3: Dakika 5. Dada atagawiwa hotuba hii. Wanafunzi wanaogawiwa hotuba hii watachagua kikao au wataonyeshwa kikao watakachotumia katika orodha ya vikao iliyo kwenye ukurasa wa 82 katika kitabu cha Shule ya Huduma. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa katika ratiba na kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani katika eneo la kutaniko lenu. Iwapo vichapo vya kutumiwa havijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti wa habari hiyo katika vichapo vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Wanafunzi wapya wanapaswa kugawiwa hotuba zinazoonyesha vichapo vya kutumia. Mwangalizi wa shule atapendezwa hasa kuona jinsi mwanafunzi anavyofafanua habari hiyo na jinsi anavyomsaidia mwenye nyumba kuelewa maana ya Maandiko na kuelewa mambo makuu. Wanafunzi wanaogawiwa hotuba hiyo wanapaswa kujua kusoma. Mwangalizi wa shule atateua msaidizi mmoja.
HOTUBA NA. 4: Dakika 5. Mwanafunzi anapaswa kuzungumzia kichwa kilichoonyeshwa katika ratiba. Kama vichapo vya kutumiwa havijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hii katika vichapo vilivyotolewa na mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Ndugu anapogawiwa hotuba hii, anaweza kuitayarisha ili ifae wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Dada anapogawiwa hotuba hii, inapaswa kutolewa jinsi Hotuba Na. 3 inavyotolewa. Mwangalizi wa shule anaweza kumpa ndugu hotuba Na. 4 anapoona inafaa kufanya hivyo. Tafadhali ona kwamba habari zenye nyota zapaswa kugawiwa akina ndugu na kutolewa kama hotuba.
WAKATI: Hotuba na maelezo ya mshauri hayapaswi kamwe kupita wakati uliowekwa. Wanafunzi wanaotoa hotuba Na. 2 hadi 4 wanapaswa kukatizwa kwa busara muda wao unapokwisha. Ndugu wanaotoa hotuba ya sifa ya usemi, Hotuba Na. 1, au mambo makuu ya usomaji wa Biblia, wanapaswa kushauriwa faraghani wakipitisha wakati uliowekwa. Wote wanapaswa kufuata wakati vizuri. Programu nzima: Dakika 45, mbali na wimbo na sala.
USHAURI: Dakika 1. Mwangalizi wa shule atatumia muda usiozidi dakika moja kutoa maelezo yanayojenga kuhusu sehemu ya hotuba inayostahili kusifiwa. Lengo lake si kupongeza tu, bali pia kuonyesha ni kwa nini jambo fulani katika hotuba lilikuwa zuri. Kulingana na uhitaji wa kila mwanafunzi, ushauri unaweza kutolewa faraghani baada ya mkutano au wakati mwingine ili kumsaidia kufanya maendeleo.
MSHAURI MSAIDIZI: Ikiwa kuna mzee mwenye uwezo mbali na mwangalizi wa shule, baraza la wazee linaweza kumteua na kumweka kuwa mshauri msaidizi. Ikiwa kuna wazee wengi katika kutaniko, basi mzee tofauti anayestahili anaweza kushughulikia mgawo huo kila mwaka. Daraka la mshauri msaidizi litakuwa kuwashauri faraghani akina ndugu wanaoshughulikia Hotuba Na. 1 na mambo makuu ya usomaji wa Biblia, wanapohitaji ushauri. Si lazima awashauri wazee wenzake au watumishi wa huduma kila mara wanapotoa hotuba hizo. Utaratibu huo utafuatwa katika mwaka wa 2004 na huenda mabadiliko fulani yakafanywa baadaye.
FOMU YA MASHAURI: Imo katika kitabu cha shule.
PITIO LA MASWALI NA MAJIBU: Dakika 30. Kila baada ya miezi miwili, mwangalizi wa shule ataongoza pitio la maswali na majibu. Sehemu hiyo itafanywa baada ya hotuba ya sifa ya usemi na mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama ilivyoorodheshwa hapa juu. Pitio hilo litahusisha habari zilizozungumziwa katika shule katika miezi miwili iliyotangulia, kutia ndani juma la pitio.
RATIBA
Jan. 5 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 1-5 Wimbo 154
Sifa ya Usemi: Kuonyesha Wasikilizaji Jinsi ya Kutumia Habari (be uku. 157 ¶1-5)
Na. 1: Kutayarisha Muhtasari (be uku. 39-42)
Na. 2: Mwanzo 2:7-25
Na. 3: Je, “Agano Jipya” Linaelekeza Kwenye Paradiso ya Kidunia ya Wakati Ujao au Hiyo Imo Katika “Agano la Kale” Tu? (rs uku. 257 ¶1–uku. 258 ¶1)
Na. 4: aMambo Tunayoweza Kujifunza Kutokana na Mifano ya Biblia ya Watu Waliotenda Dhambi kwa Kutofanya Yale Waliyopaswa Kufanya
Jan. 12 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 6-10 Wimbo 215
Sifa ya Usemi: Kuwaonyesha Wasikilizaji Jinsi ya Kutumia Habari (be uku. 158 ¶ 1-3)
Na.1: Usafi—Unamaanisha Nini Hasa? (w02 2/1 uku. 4-7)
Na. 2: Mwanzo 8:1-17
Na. 3: Kwa Nini Ni Vibaya Kusema Uwongo?
Na. 4: Kwa Nini “Paradiso” Inayotajwa Katika Luka 23:43 Haiwezi Kuwa Hadesi au Mbinguni (rs uku. 258 ¶2–uku. 259 ¶2)
Jan. 19 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 11-16 Wimbo 218
Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Kuona Faida ya Ujumbe Wetu (be uku. 159 ¶1-4)
Na. 1: Kanuni za Kimungu Zaweza Kukufaidi (w02 2/15 uku. 4-7)
Na. 2: Mwanzo 13:1-18
Na. 3: Ni Jambo Gani Linaloonyesha Kwamba Paradiso Inayotajwa Katika Luka 23:43 ni ya Kidunia? (rs uku. 259 ¶3–uku. 260 ¶4)
Na. 4: Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Huwaeleza Wengine Kuhusu Tumaini Lao?
Jan. 26 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 17-20 Wimbo 106
Sifa ya Usemi: Kutumia Maneno Yanayofaa (be uku. 160 ¶1-3)
Na. 1: Hisia-Mwenzi Hutusaidia Kudhihirisha Fadhili na Huruma (w02 4/15 uku. 24-27)
Na. 2: w02 1/1 uku. 10-11 ¶9-11
Na. 3: Maneno ya Yesu Yanayotajwa Katika Luka 13:24 Yanamaanisha Nini?
Na. 4: Yeyote Kati Yetu Anaweza Kujipatiaje Maarifa na Hekima ya Kweli? (rs uku. 83 ¶2–uku. 84 ¶1)
Feb. 2 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 21-24 Wimbo 64
Sifa ya Usemi: Lugha Inayoeleweka kwa Urahisi (be uku. 161 ¶1-4)
Na. 1: Kutayarisha Migawo ya Shule (be uku. 43 ¶1–uku. 44 ¶3)
Na. 2: Mwanzo 21:1-21
Na. 3: Ni Nini Iliyo Asili ya Falsafa za Kibinadamu? (rs uku. 84 ¶2–uku. 85 ¶2)
Na. 4: bKwa Nini Uchumba Unapaswa Kuonwa Kuwa Jambo Nzito?
Feb. 9 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 25-28 Wimbo 9
Sifa ya Usemi: Kutumia Semi Tofauti-Tofauti na Sahihi (be uku. 161 ¶5–uku. 162 ¶4)
Na. 1: Kutayarisha Ukifikiria Kichwa Kikuu na Kikao (be p. 44 ¶4–uku. 46 ¶2)
Na. 2: Mwanzo 28:1-15
Na. 3: Jinsi ya Kupata Amani ya Akili Katika Ulimwengu Huu Wenye Taabu
Na. 4: Kwa Nini Ni Ithibati ya Kufikiri Wazi Kujifunza Mafundisho ya Yesu Kristo Badala ya Falsafa za Kibinadamu? (rs uku. 85 ¶3–uku. 86 ¶2)
Feb. 16 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 29-31 Wimbo 160
Sifa ya Usemi: Maneno Yanayoonyesha Mkazo, Hisia, na Yanayovutia (be uku. 163 ¶1–uku. 164 ¶2)
Na. 1: Wanyoofu Huongozwa na Uaminifu-Maadili (w02 5/15 uku. 24-28)
Na. 2: w02 2/1 uku. 15-16 ¶6-10
Na. 3: Ni Sala za Nani Ambazo Mungu Anapenda Kusikia? (rs uku. 276 ¶1–uku. 277 ¶1)
Na. 4: Kwa Nini Wema wa Adili Ni Sifa Muhimu kwa Wakristo?
Feb. 23 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 32-35 Wimbo 1
Sifa ya Usemi: Usemi Unaopatana na Kanuni za Sarufi (be uku. 164 ¶3–uku. 165 ¶1)
Pitio la Maswali na Majibu
Mac. 1 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 36-39 Wimbo 49
Sifa ya Usemi: Kutumia Muhtasari (be uku. 166 ¶1–uku. 167 ¶2)
Na. 1: Kutayarisha Hotuba kwa Ajili ya Kutaniko (be uku. 47 ¶1–uku. 49 ¶1)
Na. 2: Mwanzo 37:12-28
Na. 3: Kwa Nini Ni Lazima Imani Yetu Iambatane na Uvumilivu?
Na. 4: cNi Nini Kingeweza Kufanya Sala za Mtu Zisikubalike kwa Mungu? (rs uku. 277 ¶2–uku. 278 ¶1)
Mac. 8 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 40-42 Wimbo 205
Sifa ya Usemi: Kupanga Mambo Unayotaka Kuzungumzia (be uku. 167 ¶3–uku. 168 ¶2)
Na. 1: Kutayarisha Mkutano wa Utumishi na Hotuba Nyingine (be uku. 49 ¶2–uku. 51 ¶1)
Na. 2: Mwanzo 42:1-20
Na. 3: Jinsi ya Kusitawisha Uhusiano wa Karibu na Yehova
Na. 4: dNi Mambo Gani Yanayofaa ya Kutolea Sala? (rs uku. 278 ¶2-9)
Mac. 15 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 43-46 Wimbo 67
Sifa ya Usemi: Fanya Muhtasari Wako Uwe Rahisi (be uku. 168 ¶3–uku. 169 ¶6)
Na. 1: Yehova Hubariki Jitihada Yenye Bidii Wakati Gani? (w02 8/1 uku. 29-31)
Na. 2: Mwanzo 43:1-18
Na. 3: eMtu Akisema, ‘Sali Pamoja na Mimi Kwanza, Ndipo Unipe Ujumbe Wako’ (rs uku. 279 ¶1-2)
Na. 4: Tunawezaje Kujifanyia Marafiki Kupitia Mali Zisizo za Uadilifu?
Mac. 22 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 47-50 Wimbo 187
Sifa ya Usemi: Habari Inayofuatana Vizuri (be uku. 170 ¶1–uku. 171 ¶2)
Na. 1: Kwa Nini Yehova Alikubali Dhabihu ya Abeli na Kukataa ya Kaini? (w02 8/1 uku. 28)
Na. 2: Mwanzo 47:1-17
Na. 3: Ni Baadhi ya Unabii Gani Wenye Kutokeza wa Biblia Ambao Bado Utatimizwa? (rs uku. 362 ¶2–uku. 363 ¶4)
Na. 4: Kwa Nini Kumwogopa Yehova Ndio Mwanzo wa Hekima?
Mac. 29 Usomaji wa Biblia: Kutoka 1-6 Wimbo 52
Sifa ya Usemi: Kufuatanisha Habari Vizuri (be uku. 171 ¶3–uku. 172 ¶6)
Na. 1: Uwezo wa Kufikiri Unaweza Kukulindaje? (w02 8/15 uku. 21-24)
Na. 2: w02 2/15 uku. 19-20 ¶7-11
Na. 3: Yehova Huonaje Kiburi?
Na. 4: Kwa Nini Imewapasa Wakristo Wapendezwe Sana na Mabashiri ya Biblia? (rs uku. 363 ¶5–uku. 364 ¶3)
Apr. 5 Usomaji wa Biblia: Kutoka 7-10 Wimbo 61
Sifa ya Usemi: Kutumia Habari Zinazohusika Pekee (be uku. 173 ¶1-4)
Na. 1: Kutayarisha Hotuba za Watu Wote (be uku. 52 ¶1–uku. 54 ¶1)
Na. 2: Kutoka 8:1-19
Na. 3: fMtu Akisema, ‘Ninyi Mnatia Mkazo Mwingi Mno Juu ya Unabii’ (rs uku. 364 ¶4-5)
Na. 4: Kwa Nini Tumaini Ni Kama “Nanga ya Nafsi”?
Apr. 12 Usomaji wa Biblia: Kutoka 11-14 Wimbo 87
Sifa ya Usemi: Kutoa Hotuba Bila Kutazama Sana Maandishi (be uku. 174 ¶1–uku. 175 ¶4)
Na. 1: Maamuzi ya Msemaji (be uku. 54 ¶2-4; uku. 55, sanduku)
Na. 2: Kutoka 12:1-16
Na. 3: Kwa Nini Tuwe Tayari Kukubali Nidhamu ya Yehova?
Na. 4: Fundisho la Tohara (Purgatori) Linategemea Nini? (rs uku. uku. 316 ¶1-6)
Apr. 19 Usomaji wa Biblia: Kutoka 15-18 Wimbo 171
Sifa ya Usemi: Kuepuka Mitego ya Kutoa Habari Bila Kutazama Sana Maandishi (be uku. 175 ¶5–uku. 177 ¶1)
Na. 1: Tuyaoneje Majaribu? (w02 9/1 uku. 29-31)
Na. 2: w02 3/1 uku. 15-16 ¶8-11
Na. 3: Je, Adhabu Zaidi kwa Sababu ya Dhambi Inatozwa Baada ya Mtu Kufa? (rs uku. 317 ¶2-6)
Na. 4: gKwa Nini Ndoa Inapaswa Kuwa Muungano wa Maisha?
Apr. 26 Usomaji wa Biblia: Kutoka 19-22 Wimbo 59
Sifa ya Usemi: Wengine Wanapotaka Majibu (be uku. 177 ¶2–uku. 178 ¶2)
Pitio la Maswali na Majibu
Mei 3 Usomaji wa Biblia: Kutoka 23-26 Wimbo 13
Sifa ya Usemi: Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi (be uku. 179-180)
Na. 1: Sitawisha Ustadi wa Kufundisha (be uku. 56 ¶1–uku. 57 ¶2)
Na. 2: Kutoka 23:1-17
Na. 3: Yehova Anaweza Kumsaidiaje Mtu Aache Mazoea Mabaya?
Na. 4: Jamii Mbalimbali Zilitoka Wapi? (rs uku. 95 ¶1-4)
Mei 10 Usomaji wa Biblia: Kutoka 27-29 Wimbo 28
Sifa ya Usemi: Ubora wa Sauti (be uku. 181 ¶1-4)
Na. 1: ‘Pambanua Mambo’ (be uku. 57 ¶3–uku. 58 ¶2)
Na. 2: Kutoka 28:29-43
Na. 3: Ikiwa Kulikuwako Jamaa Moja Tu, Ni Wapi Kaini Alikopata Mke Wake? (rs uku. 96 ¶1-3)
Na. 4: Kwa Nini Ni Vibaya Kuwabagua Watu?
Mei 17 Usomaji wa Biblia: Kutoka 30-33 Wimbo 93
Sifa ya Usemi: Pumua Vizuri (be uku. 181 ¶5–uku. 184 ¶1; uku. 182, sanduku)
Na. 1: Watie Moyo Wasikilizaji Wafikiri (be uku. 58 ¶3–p. 59 ¶3)
Na. 2: Kutoka 30:1-21
Na. 3: Kwa Nini Tuwe Wenye Tabia-Pole?
Na. 4: Kwa Nini Jamii Zina Tabia Mbalimbali? (rs uku. 96 ¶4–p. 97 ¶3)
Mei 24 Usomaji wa Biblia: Kutoka 34-37 Wimbo 86
Sifa ya Usemi: Kutuliza Mkazo wa Misuli (be uku. 184 ¶2–uku. 185 ¶2; uku. 184, sanduku)
Na. 1: Onyesha Jinsi Habari Inavyotumika na Weka Mfano Mzuri (be uku. 60 ¶1–uku. 61 ¶3)
Na. 2: Kutoka 36:1-18
Na. 3: Je, Wanadamu Wote Ni Watoto wa Mungu? (rs uku. 98 ¶1-5)
Na. 4: Kwa Nini Tuwe Waaminifu Katika Mambo Madogo?
Mei 31 Usomaji wa Biblia: Kutoka 38-40 Wimbo 202
Sifa ya Usemi: Kupendezwa na Wengine (be uku. 186 ¶1-4)
Na. 1: Jinsi ya Kuboresha Stadi za Mazungumzo (be uku. 62 ¶1–uku. 64 ¶1)
Na. 2: w02 5/1 uku. 19-20 ¶3-6
Na. 3: Kulielewa Andiko la 1 Yohana 3:19, 20 Kunawezaje Kumfariji Mtu?
Na. 4: Je, Watu wa Jamii Zote Watapata Kuungana Kweli Kweli Wakiwa Ndugu na Dada? (rs p. 99 ¶1-4)
Juni 7 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 1-5 Wimbo 123
Sifa ya Usemi: Kusikiliza kwa Makini (be uku. 187 ¶1-5)
Na. 1: Jinsi ya Kuendeleza Mazungumzo (be uku. 64 ¶2–uku. 65 ¶4)
Na. 2: Mambo ya Walawi 3:1-17
Na. 3: Kifo cha Yesu Kristo Kilikuwaje Tofauti na Kile cha Wengine Waliokufa kwa Sababu ya Imani? (rs uku. 346 ¶3—uku. 347 ¶2)
Na. 4: Kuna Ubaya Gani Kujihusisha Kidogo Tu na Mambo ya Mizungu?
Juni 14 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 6-9 Wimbo 121
Sifa ya Usemi: Kuwasaidia Wengine Wafanye Maendeleo (be uku. 187 ¶6–uku. 188 ¶3)
Na. 1: Kufahamu Maoni ya Anayeuliza Swali (be uku. 66 ¶1–uku. 68 ¶1)
Na. 2: Mambo ya Walawi 7:1-19
Na. 3: Tunawezaje Kujifunza Kuchukia Yaliyo Mabaya?
Na. 4: Kwa Nini Ilikuwa Lazima Ukombozi Uandaliwe kwa Njia Hiyo? (rs uku. 347 ¶4-6)
Juni 21 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 10-13 Wimbo 183
Sifa ya Usemi: Kutoa Msaada Unaofaa (be uku. 188 ¶4–uku. 189 ¶4)
Na. 1: Jua Jinsi Unavyopaswa Kujibu (be uku. 68 ¶2–uku. 70 ¶3)
Na. 2: Mambo ya Walawi 11:1-25
Na. 3: Kwa Nini Mungu Hakuamuru Tu Kwamba Wale Wote Ambao Wangemtii Wangeweza Kuishi Milele? (rs uku. 348¶1—uku. 349 ¶1)
Na. 4: Maoni ya Yehova Kuhusu Kusema Uwongo
Juni 28 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 14-16 Wimbo 216
Sifa ya Usemi: Kuwaheshimu Wengine (be uku. 190 ¶1-4)
Pitio la Maswali na Majibu
Julai 5 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 17-20 Wimbo 54
Sifa ya Usemi: Salamu Zenye Heshima (be uku. 191 ¶1–uku. 192 ¶1)
Na. 1: Kuandika Barua (be uku. 71-73)
Na. 2: Mambo ya Walawi 17:1-16
Na. 3: Litumaini Tengenezo la Yehova
Na. 4: Ustahili wa Dhabihu ya Yesu Ulitumiwa kwa Akina Nani Kwanza, na kwa Lengo Gani? (rs uku. 349 ¶2-3)
Julai 12 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 21-24 Wimbo 138
Sifa ya Usemi: Kutoa Hotuba kwa Njia ya Heshima (be uku. 192 ¶2–uku. 193 ¶2)
Na. 1: Uwe Mwenye Maendeleo (be uku. 74 ¶1–uku. 75 ¶3)
Na. 2: Mambo ya Walawi 22:1-16
Na. 3: Ni Nani Wengine Wakati Wetu Wanaonufaika na Dhabihu ya Yesu? (rs uku. 349 ¶4–uku. 350 ¶2)
Na. 4: Je, Yehova Alikuwa Mungu wa Kikabila wa Wayahudi?
Julai 19 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 25-27 Wimbo 7
Sifa ya Usemi: Kuzungumza kwa Usadikisho (be uku. 194 ¶1–uku. 195 ¶2)
Na. 1: Tumia Zawadi Yako (be uku. 75 ¶4–uku. 77 ¶2)
Na. 2: Mambo ya Walawi 25:1-19
Na. 3: Jinsi Ugaidi Utakavyokoma
Na. 4: Ni Baraka Gani za Wakati Ujao Zitakazofurahiwa Kama Matokeo ya Ukombozi? (rs uku. 350 ¶3–uku. 351 ¶2)
Julai 26 Usomaji wa Biblia: Hesabu 1-3 Wimbo 30
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuonyesha Usadikisho (be uku. 195 ¶3–uku. 196 ¶4)
Na. 1: Je, Wakristo Wanapaswa Kuwa na Wivu? (w02 10/15 uku. 28-31)
Na. 2: w02 6/15 uku. 18-19 ¶6-9
Na. 3: Ni Nini Linalotakwa Kwetu Ili Tunufaike na Dhabihu ya Yesu? (rs uku. 351 ¶3-6)
Na. 4: Je, Ni Vibaya Kuomboleza Kifo cha Mpendwa Wetu?
Ago. 2 Usomaji wa Biblia: Hesabu 4-6 Wimbo 128
Sifa ya Usemi: Uwe Mwenye Busara Lakini Thabiti (be uku. 197 ¶1-3)
Na. 1: Tunawezaje Kuishi Maisha Yanayompendeza Yehova? (w02 11/15 uku. 20-23)
Na. 2: Hesabu 6:1-17
Na. 3: Biblia Inawezaje Kuwasaidia Watu Waache Kuchukiana?
Na. 4: Uandalizi wa Ukombozi Umepasa Uwe na Matokeo Gani juu ya Jinsi Tunavyotumia Maisha Zetu? (rs uku. 352 ¶1-3)
Ago. 9 Usomaji wa Biblia: Hesabu 7-9 Wimbo 35
Sifa ya Usemi: Kutumia Busara Unapohubiri (be uku. 197 ¶4–uku. 198 ¶5)
Na. 1: Je, Inawezekana Kuwa na Jamii Isiyo na Ubaguzi? (w02 1/1 uku. 4-7)
Na. 2: Hesabu 8:1-19
Na. 3: Mtume Paulo Aliposema Kwamba Wakristo ‘Wangedakwa’ Wakawe Pamoja na Bwana, Alikuwa Akizungumza juu ya Nini? (rs uku. 113 ¶1-2)
Na. 4: Mpinga-Kristo Ni Nani?
Ago. 16 Usomaji wa Biblia: Hesabu 10-13 Wimbo 203
Sifa ya Usemi: Maneno Yafaayo Wakati Ufaao (be uku. 199 ¶1-4)
Na. 1 : Mtumaini Yehova—Mungu Aliye Halisi (w02 1/15 uku. 5-7)
Na. 2: Hesabu 12:1-16
Na. 3: Je, Kisasi cha Yehova Kinapatana na Upendo Wake?
Na. 4: Je, Kristo Atatokea kwa Jinsi ya Kuonekana na Macho juu ya Wingu Kisha Awachukue Wakristo Waaminifu Katika Mbingu Huku Ulimwengu Ukiwa Unatazama? (rs uku. 114 ¶1-3)
Ago. 23 Usomaji wa Biblia: Hesabu 14-16 Wimbo 207
Sifa ya Usemi: Kutumia Busara Katika Familia na Ukiwa na Wakristo Wenzako (be uku. 200 ¶1-4)
Na. 1 : Ndugu Waliositawisha Mitazamo Tofauti (w02 1/15 uku. 21-23)
Na. 2: w02 7/15 uku. 23-24 ¶15-19
Na. 3: Je, Inawezekana kwa Wakristo Kuchukuliwa Kupelekwa Mbinguni Wakiwa na Miili Yao ya Asili? (rs p. 115 ¶1-2)
Na. 4: hKwa Nini Wakristo Hawapaswi Kucheza Michezo ya Video Yenye Jeuri?
Ago. 30 Usomaji wa Biblia: Hesabu 17-21 Wimbo 150
Sifa ya Usemi: Uwe Mwenye Kujenga na Kutia Moyo (be uku. 202 ¶1–uku. 203 ¶2)
Pitio la Maswali na Majibu
Sept. 6 Usomaji wa Biblia: Hesabu 22-25 Wimbo 22
Sifa ya Usemi: Uwe Mwenye Kutia Moyo (be uku. 203 ¶3–uku. 204 ¶1)
Na. 1: Kwa Nini Ulimwengu Huo wa Kale Uliangamia? (w02 3/1 uku. 5-7)
Na. 2: Hesabu 22:1-19
Na. 3: Je, Wakristo Waaminifu Watachukuliwa Kwenda Mbinguni kwa Siri Bila Kufa? (rs p. 115 ¶3–uku. 116 ¶3)
Na. 4: iKwa Nini Wazazi Wakristo Wanapaswa Kuwasomea Watoto Wao?
Sept. 13 Usomaji wa Biblia: Hesabu 26-29 Wimbo 71
Sifa ya Usemi: Unapozungumza na Waamini Wenzako (be uku. 204 ¶2–uku. 205 ¶4)
Na. 1: Jinsi Ulemavu Utakavyokoma (w02 5/1 uku. 4-7)
Na. 2: Hesabu 29:1-19
Na. 3: Ni Himaya Gani Itakayokuwapo kwa Wakristo wa Kweli Wakati wa Dhiki Kubwa? (rs uku. 116 ¶4–uku. 117 ¶3)
Na. 4: Ahadi za Mungu Zimekuwaje Ndiyo kwa Njia ya Yesu Kristo?
Sept. 20 Usomaji wa Biblia: Hesabu 30-32 Wimbo 51
Sifa ya Usemi: Kurudia Ili Kukazia Mambo (be uku. 206 ¶1-4)
Na. 1: Panda kwa Uadilifu, Vuna Fadhili-Upendo za Mungu (w02 7/15 uku. 28-31)
Na. 2: Hesabu 30:1-16
Na. 3: Kwa Nini Wakristo Fulani Wanachukuliwa Kwenda Mbinguni Wakawe Pamoja na Kristo? (rs uku. 117 ¶5-8)
Na. 4: jKwa Nini Tuepuke Kabisa Ponografia?
Sept. 27 Usomaji wa Biblia: Hesabu 33-36 Wimbo 100
Sifa ya Usemi: Kurudia Ili Kukazia Mambo Unapokuwa Katika Huduma ya Shambani na Unapotoa Hotuba (be uku. 207 ¶1–uku. 208 ¶4)
Na. 1: Watakatifu wa Kweli Wanaweza Kukusaidiaje? (w02 9/15 uku. 4-7)
Na. 2: w02 8/1 uku. 18-19 ¶15-19
Na. 3: k‘Je, Unaitikadi Katika Kuchukuliwa Kimwili Kutoka Duniani?’ (rs uku. 117 ¶9–uku. 118 ¶1)
Na. 4: Kwa Nini Tuepuke Michezo Hatari Yenye Kusisimua?
Okt. 4 Usomaji wa Biblia Kumbukumbu la Torati 1-3 Wimbo 191
Sifa ya Usemi: Kufafanua Kichwa Kikuu (be uku. 209 ¶1-3)
Na. 1: Ujuzi Sahihi Kumhusu Mungu Hutufariji (w02 10/1 uku. 5-7)
Na. 2: Kumbukumbu la Torati 1:1-18
Na. 3: Inamaanisha Nini Kuufanya Ukweli Uwe Mali Yako Mwenyewe?
Na. 4: Je, Hisia ya Kigeni ya Kuwa Mwenye Kuzoelea Sana Watu Wapya Wanaojulikana na Mahali Papya Kabisa Huthibitisha Kuzaliwa Upya Katika Mwili Mwingine Kuwa Uhakika? (rs uku. 154 ¶2–uku. 156 ¶2)
Okt. 11 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 4-6 Wimbo 181
Sifa ya Usemi: Kutumia Kichwa Kikuu Kinachofaa (be uku. 210 ¶1–uku. 211 ¶1; uku. 211, sanduku)
Na. 1: Kuhesabu Kurudi Nyuma Kuanzia 537 K.W.K. Mpaka 997 K.W.K. (si uku. 285 ¶5-7)
Na. 2: Kumbukumbu la Torati 4:1-14
Na. 3: Kwa Nini Simulizi la Yohana 9:1, 2 Halithibitishi Kuzaliwa Upya Katika Mwili Mwingine? (rs uku. 156 ¶3–p. 157 ¶3)
Na. 4: “Kukaza Akili juu ya Roho” Kunahusisha Nini?
Okt. 18 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 7-10 Wimbo 78
Sifa ya Usemi: Kukazia Mambo Makuu (be uku. 212 ¶1–uku. 213 ¶1)
Na. 1: Kuhesabu Kurudi Nyuma Kuanzia 997 K.W.K. Mpaka 2370 K.W.K. (si uku. 285-286 ¶8-11)
Na. 2: w02 8/15 uku. 15-16 ¶3-6
Na. 3: Kuna Tofauti Kadiri Gani Kati ya Kuzaliwa Upya Katika Mwili Mwingine na Tumaini Linalotolewa Katika Biblia (rs uku. 157 ¶4–uku. 158 ¶1)
Na. 4: lMaoni ya Yehova Kuhusu Waasi-Imani
Okt. 25 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 11-13 Wimbo 57
Sifa ya Usemi: Usitumie Mambo Makuu Mengi Mno (be uku. 213 ¶2–uku. 214 ¶5)
Pitio la Maswali na Majibu
Nov. 1 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 14-18 Wimbo 26
Sifa ya Usemi: Utangulizi Unaoamsha Upendezi (be uku. 215 ¶1–uku. 216 ¶5)
Na. 1: Kuhesabu Kurudi Nyuma Kuanzia 2370 K.W.K. Mpaka 4026 K.W.K. (si uku. 286-287 ¶12-15)
Na. 2: Kumbukumbu la Torati 14:1-23
Na. 3: aMtu Akisema, ‘Mimi Naitikadi Kuna Kuzaliwa Upya Katika Mwili Mwingine’ (rs uku. 158 ¶2-4)
Na. 4: Kwa Nini Wakristo Waishi Maisha Sahili?
Nov. 8 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 19-22 Wimbo 182
Sifa ya Usemi: Jinsi ya Kuvuta Usikivu wa Watu Unapokuwa Katika Utumishi wa Shambani (be p. 217 ¶1-4)
Na. 1: Ukaaji wa Kidunia wa Yesu (si uku. 287 ¶16, 291 ¶17)
Na. 2: Kumbukumbu la Torati 21:1-17
Na. 3: Kwa Nini Kuna Dini Nyingi Sana? (rs uku. 67 ¶1–p. 68 ¶2)
Na. 4: Mifano Iliyomo Katika Biblia Inaweza Kutusaidiaje Kukabiliana na Kivunja-Moyo?
Nov. 15 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 23-27 Wimbo 162
Sifa ya Usemi: Taja Hususa Habari Utakayozungumzia Unapotoa Utangulizi (be uku. 217 ¶5–uku. 219 ¶2)
Na. 1: Mambo ya Wakati wa Huduma ya Yesu (si uku. 291 ¶18-19)
Na. 2: Kumbukumbu la Torati 24:1-16
Na. 3: Jinsi ya Kuwatambua Wale Wanaoungwa Mkono na Mungu
Na. 4: Je, Ni Kweli Kwamba Kuna Wema Katika Dini Zote? (rs uku. 68 ¶3-5)
Nov. 22 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 28-31 Wimbo 32
Sifa ya Usemi: Umalizio Mzuri (be uku. 220 ¶1-3)
Na. 1: Kuhesabu Miaka Katika Nyakati za Kimitume (si uku. 291-292 ¶20-23)
Na. 2: Kumbukumbu la Torati 29:1-18
Na. 3: Je, Inafaa Mtu Kuacha Dini ya Wazazi Wake? (rs uku. 69 ¶1-3)
Na. 4: Kwa Nini Wakristo Wanapaswa Kuwa na Kiasi?
Nov. 29 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 32-34 Wimbo 41
Sifa ya Usemi: Kumbuka Mambo Haya (be uku. 221 ¶1-5)
Na. 1: Safari ya Pili ya Umishonari ya Paulo (si uku. 292-293 ¶24-25)
Na. 2: w02 10/15 uku. 11 ¶10-13
Na. 3: Njia Ambazo Tunaweza Kulitakasa Jina la Mungu
Na. 4: Maoni ya Biblia Ni Nini juu ya Kuchangamana na Dini Nyingine? (rs uku. 70 ¶1–uku. 71 ¶2)
Des. 6 Usomaji wa Biblia: Yoshua 1-5 Wimbo 40
Sifa ya Usemi: Katika Huduma ya Shambani (be uku. 221 ¶6–uku. 222 ¶6)
Na. 1: Safari ya Tatu ya Umishonari ya Paulo na Miaka ya Kumalizia, 56-100 W.K. (si uku. 293 ¶26-30)
Na. 2: Yoshua 4:1-14
Na. 3: Je, Kuwa Upande wa Dini Iliyofanywa Tengenezo Ni kwa Lazima? (rs uku. 71 ¶3–uku. 72 ¶2)
Na. 4: Je, Krismasi Ni Sherehe ya Kikristo?
Des. 13 Usomaji wa Biblia: Yoshua 6-8 Wimbo 213
Sifa ya Usemi: Kusema Mambo Yaliyo Sahihi (be uku. 223 ¶1-5)
Na. 1: Kuomba Msamaha Ni Njia Bora ya Kufanya Amani (w02 11/1 uku. 4-7)
Na. 2: Yoshua 6:10-23
Na. 3: Kwa Nini Tuendelee Kuhubiri Nyumba kwa Nyumba?
No. 4: Je, Kupenda Jirani Ndilo Jambo la Maana? (rs p. 72 ¶4)
Des. 20 Usomaji wa Biblia: Yoshua 9-11 Wimbo 135
Sifa ya Usemi: ‘Kushika kwa Imara Neno la Uaminifu’ (be uku. 224 ¶1-4)
Na. 1: Itieni Mikono Yenu Nguvu (w02 12/1 uku. 30-31)
Na. 2: w02 11/15 uku. 18-19 ¶19-23
Na. 3: Je, Kuwa na Uhusiano wa Kibinafsi Pamoja na Mungu Ni Jambo la Maana Kweli Kweli? (rs p. 72 ¶5–uku. 73 ¶1)
Na. 4: bInamaanisha Nini Kuwa Mwenye Kufanya Amani?
Des. 27 Usomaji wa Biblia: Yoshua 12-15 Wimbo 210
Sifa ya Usemi: Kuchunguza Usahihi wa Habari Unayozungumzia (be uku. 225 ¶1-3)
Pitio la Maswali na Majibu
[Maelezo ya Chini]
a Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
b Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
c Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
d Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
e Wakati ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.
f Wakati ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.
g Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
h Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
i Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
j Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
k Wakati ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.
l Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.
a Wakati ukiruhusu, zungumzia jinsi ya kushughulikia maoni na vipingamizi vya kawaida katika eneo lenu.
b Sehemu hii igawiwe akina ndugu peke yao.