Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Oktoba 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Watie moyo wote watumie maswali yaliyo katika ukurasa wa 1 kupitia mambo waliyoandika wanapojitayarishia mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu programu ya Kusanyiko la “Mtukuzeni Mungu” katika Mkutano wa Utumishi juma lijalo. Ukitumia mapendekezo yaliyo katika ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili halisi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15 na Amkeni! la Septemba 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe pamoja, hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika onyesho moja, mhubiri aonyeshe jinsi ya kufanya ziara ya kurudia kwa mtu ambaye hupelekewa magazeti kwa ukawaida. Mhubiri huyo aweka msingi kwa ajili ya ziara inayofuata kwa kumwonyesha sanduku “Katika Toleo Linalofuata.”—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1998, uku. 12, fu. 7-8.
Dak. 20: “Mtumikieni Yehova kwa Kushangilia.”a (Wote wanapaswa kuwa na nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002 kwa ajili ya mazungumzo haya.) Baada ya kuzungumzia fungu la 4, taja kwamba katika mwezi wa Novemba tutatoa broshua Anataka na kitabu Ujuzi. Taja kifupi mapendekezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002. Kisha kuwe na onyesho ambapo wahubiri wanajitayarisha kwa ajili ya utumishi kwa kuigiza pendekezo lililozungumziwa. Watie wote moyo wajitayarishe kwa ajili ya huduma.
Dak. 15: Kuongoza Mafunzo ya Biblia Huleta Baraka. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Simulia mambo machache yaliyoonwa kutoka katika vichapo vyetu yanayohusu mafunzo ya Biblia yanayofanya maendeleo. (w00 3/1 uku. 6; yb98 uku. 55-60) Waombe wasikilizaji waeleze mambo tunayojifunza kutokana na mambo hayo yaliyoonwa na jinsi tunavyofaidika kwa kuongoza mafunzo ya Biblia.
Wimbo 172 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 20
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 40: “Makusanyiko ya Wilaya na ya Kimataifa Yametuchochea Kumtukuza Mungu!” Ishughulikiwe na mzee. Baada ya utangulizi usiozidi dakika moja, kuwe na mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu programu ya kusanyiko kwa kutumia maswali yaliyo katika makala. Panga wakati vizuri ili maswali yote yazungumziwe, huenda baadhi ya maswali yakahitaji jibu moja tu. Wakati uliowekwa hautoshi maandiko yote yaliyotajwa kusomwa; yametiwa ndani ili kufanya iwe rahisi kupata majibu. Maelezo yanapaswa kukazia faida za mambo waliyojifunza.
Wimbo 112 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 27
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Oktoba. Watie wote moyo wapitie mambo waliyoandika katika programu ya kusanyiko la pekee la mwaka wa utumishi uliopita, wakijitayarishia Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo. Ukitumia mapendekezo yaliyo katika ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili yanayoonyesha jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, na Amkeni! la Oktoba 8. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe pamoja, hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika onyesho moja, onyesha jinsi ya kushughulikia kizuia mazungumzo, “Mimi Sipendezwi.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. 16.
Dak. 20: Tumia Upanga wa Roho. (Efe. 6:17) Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 143-144. Waombe wasikilizaji wajibu maswali haya: (1) Kwa nini sisi hutumia Biblia tunapojibu maswali? (2) Jina Mashahidi wa Yehova linaonyesha nini kutuhusu? (3) Yesu aliweka mfano gani, nasi tunaweza kumwigaje? (4) Katika eneo lenu, ni njia zipi zenye matokeo zinazoweza kutumiwa kuanzisha mazungumzo ya Biblia? (5) Kwa nini ni vizuri kusoma Biblia moja kwa moja inapowezekana? (6) Wazee wanawezaje kuwatia moyo wengine waitumie Biblia vizuri? Panga kuwe na onyesho lililotayarishwa vizuri kwa kutegemea mazoezi yaliyo katika ukurasa wa 144 ambapo mhubiri mwenye uwezo anatumia angalau andiko moja kujibu swali. Watie wote moyo wajiwekee mradi wa kuitumia Biblia kila wakati wanapotoa ushahidi.
Dak. 13: Mambo ya kwenu yaliyoonwa. Waombe wasikilizaji wasimulie mambo waliyojionea walipokuwa wakihudhuria kusanyiko la wilaya au walipokuwa wakihubiri kazini, shuleni, au kwingineko.
Wimbo 52 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 3
Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 13: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 25: Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora. (1 Tim. 6:18) Kwa kutumia maswali yaliyo hapa, mzee aongoza mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu programu ya kusanyiko la pekee lililofanywa katika mwaka wa utumishi uliopita. Omba kutaniko lisimulie jinsi wametumia mambo waliyojifunza. (Watu mbalimbali wanaweza kugawiwa sehemu fulani mapema.) Kazia sehemu zifuatazo za programu: (1) “Kazi Zilizo Bora Hunufaisha Sana.” (Mhu. 2:11) Kwa nini watumishi wa Mungu hufanya kazi bora zinazotajwa katika Neno la Mungu badala ya kazi za ubatili za ulimwengu huu? (2) “Iweni Matajiri Machoni pa Mungu.” (Mt. 6:20) Watu fulani ‘wamewekaje hazina mbinguni,’ nao wamefaidikaje? (3) “Boresha Huduma Yako kwa Kuwa na Funzo la Biblia.” (om uku. 91) Ni nini kinachoweza kutusaidia kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia? (4) “Kazi Zilizo Bora Wakati Huu wa Mavuno.” (Mt. 13:37-39) Wakristo wa kwanza waliweka mfano gani wa kazi zilizo bora, na kazi ya Ufalme imepanukaje leo? (5) “Kazi Zilizo Bora na Zimtukuze Yehova.” (Mt. 5:14-16) Watu fulani ‘wameachaje nuru yao iangaze’? (6) “Kuwapongeza Vijana kwa Kazi Zilizo Bora za Kumsifu Yehova.” (Zab. 148:12, 13) Vijana Wakristo katika mzunguko wetu wanamsifuje Yehova? (7) “Endeleeni Kufanya Kazi Zilizo Bora na Kupata Baraka za Yehova.” (Met. 10:22) Tunapojishughulisha na kazi zilizo bora, tunaweza kupata baraka gani tukiwa mtu mmojammoja, tukiwa familia, tukiwa kutaniko, na tukiwa tengenezo la ulimwenguni pote?
Wimbo 180 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.