Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Novemba 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 panga kuwe na maonyesho mawili yanayofaa eneo lenu ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15 na Amkeni! la Oktoba 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika onyesho moja mhubiri aeleza jinsi kazi yetu ya ulimwenguni pote inavyogharimiwa, kisha mwenye nyumba atoa mchango papo hapo.—Ona Mnara wa Mlinzi, uku. wa 2, au Amkeni! uku. wa 5.
Dak. 15: “Iweni Tayari.”a Waombe wasikilizaji waeleze kile kinachowasaidia kuepuka mahangaiko na vikengeusha-fikira vya mfumo huu wa mambo visiwapotezee wakati ambao wangetumia katika shughuli za kiroho.
Dak. 20: Unachaguaje Mashirika Yako? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Mwabudu Mungu, ukurasa wa 48-49. Ukitumia maswali na maandiko katika fungu la 13, waombe wasikilizaji waeleze kanuni za Biblia zinazopaswa kutuongoza kuchagua mashirika yetu.
Wimbo 127 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 17
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Wahoji wahubiri wawili au watatu ambao wamekuwa na mambo yaliyoonwa yenye kupendeza walipotumia toleo la sasa la vichapo. Huenda wengine wameanzisha mafunzo ya Biblia.
Dak. 15: Sitawisha Roho ya Kutoa. Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2003, ukurasa wa 27-30. Gazeti hilo lisipopatikana tumia gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2002, ukurasa wa 26-30.
Dak. 18: “Pongezi Hutia Moyo.”b Tia ndani maelezo kutoka kitabu Furaha ya Familia, ukurasa wa 49-50, fungu la 21. Waombe wasikilizaji waeleze kifupi jinsi walivyotiwa moyo walipopongezwa na wengine.
Wimbo 58 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 24
Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 panga kuwe na maonyesho mawili ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1 na Amkeni! la Novemba 8. Andiko tofauti na lile lililotajwa kwenye ukurasa wa 4 linaweza kutumiwa. Katika kila onyesho magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika onyesho moja magazeti yatolewe katika gari la umma au mahali pengine panapofaa katika eneo lenu. Eleza jinsi kazi yetu ya ulimwenguni pote inavyogharimiwa na mwenye nyumba asema kwamba angependa kutoa mchango.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.
Dak. 23: “Kujenga Uhusiano wa Karibu Pamoja na Yehova.”c Tumia maswali yaliyo kwenye makala. Waombe wasikilizaji watoe maelezo juu ya maandiko. Panga mapema mhubiri mmoja au wawili waeleze kilichowasaidia kuboresha funzo lao la kibinafsi la Biblia.
Wimbo 202 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Novemba. Taja toleo la vichapo la Desemba. Pitia kwa ufupi dokezo moja au mawili ya kutoa toleo hilo. Eleza jinsi wahubiri wanavyoweza kutumia Watch Tower Publications Index kupata madokezo mengine.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2001, uku. wa 2.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: Sifa za Kustahili Kuwafundisha Wengine. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1, 2000, ukurasa wa 16-17, fungu la 9-13. Lengo letu kuu katika huduma ni kufundisha kwa ustadi. Tutafanikiwa kuwasaidia watu wenye mfano wa kondoo tukiwaeleza ujumbe wa Ufalme kwa njia inayoeleweka na yenye kuchochea. Zungumzia maswali yafuatayo: (1) Kuna tofauti gani kati ya kuhubiri na kufundisha? (jv 572, fu. la 4) (2) Kwa nini wengine huogopa kuongoza funzo la Biblia? (3) Tunawezaje kuboresha uwezo wetu wa kufundisha? (4) Tunawezaje kuhakikisha kwamba mwanafunzi wetu anaelewa anayojifunza? (5) Tunapaswa kumsaidia mwanafunzi kufikia lengo gani?
Wimbo 70 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa maelezo yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.