Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Januari: Kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1988 ambacho huenda kutaniko likawa nacho na pia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Ikiwa kutaniko halina toleo lolote kati ya hayo, ulizeni makutaniko yoyote ya karibu kama yana vichapo vyovyote vya zamani vya ziada ambavyo mnaweza kutumia. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Februari: Mkaribie Yehova. Ikiwa hamna kitabu hicho, mnaweza kutoa kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! au Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Jitihada za pekee zitafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Ikiwa watu tayari wana kichapo hicho, kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! kinaweza kutolewa. Aprili: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, tia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho au matukio mengine ya kitheokrasi lakini ambao hawashirikiani na tengenezo. Jitahidi kutoa kitabu Mwabudu Mungu. Jitahidi sana kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa ikiwa watu fulani tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka.
◼ Kuanzia juma la Machi 15, 2004, tutajifunza kitabu Mkaribie Yehova katika Funzo la Kitabu la Kutaniko.
◼ Kuanzia Februari, na si baada ya Machi 7, hotuba mpya ya watu wote kwa waangalizi wa mzunguko itakuwa “Wewe Unapenda Viwango vya Nani?”
◼ Makutaniko yanapaswa kufanya mipango inayofaa ya kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu siku ya Jumapili, Aprili 4, baada ya jua kushuka. Ingawa hotuba inaweza kuanza mapema, mifano haipaswi kupitishwa mpaka baada ya jua kushuka. Angalieni vyanzo vya habari vya kwenu ili kujua wakati jua linaposhuka katika eneo lenu. Kwa kuwa hakuna mikutano mingine itakayofanywa siku hiyo isipokuwa mkutano wa utumishi wa shambani, marekebisho yanayofaa yanapaswa kufanywa ili Funzo la Mnara wa Mlinzi lifanywe wakati mwingine. Waangalizi wa mzunguko watahitaji kurekebisha ratiba yao ya mikutano kwa ajili ya juma hilo kulingana na hali. Ingawa ni vizuri kila kutaniko kuwa na Ukumbusho wake lenyewe, huenda hilo lisiwezekane wakati wote. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba moja la Ufalme, labda kutaniko moja au zaidi yanaweza kutumia mahali pengine jioni hiyo. Inapowezekana, tunapendekeza muda wa angalau dakika 40 kati ya programu ili wote wafaidike kikamili kutokana na pindi hiyo. Hali za magari na maegesho zinapaswa kufikiriwa pia, kutia ndani kushukisha na kubeba abiria. Baraza la wazee linapaswa kuamua mipango inayofaa zaidi kwao.