Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/04 uku. 5
  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 2/04 uku. 5

Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Februari 23, 2004. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa kuanzia juma la Januari 5 hadi Februari 23, 2004. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba wasikilizaji wanaelewa waziwazi jinsi ya kutumia habari inayotolewa na kwamba inawafaidi kwelikweli? [be uku. 158 fu. la 1-3]

2. Kwa nini tunapaswa kuchagua maneno kwa uangalifu? [be uku. 160 fu. 1 na sanduku la pili]

3. Ni jambo gani kuu linalohusu usemi mzuri ambalo linakaziwa katika 1 Wakorintho 14:9, na tunawezaje kutumia kanuni hiyo tunapowafundisha wengine? [be uku. 161 fu. 1-4]

4. Andiko la Mathayo 5:3-12 na Marko 10:17-21 yanaonyesha jambo gani bora la pekee kuhusu ufundishaji wa Yesu ambalo tunaweza kuiga? [be uku. 162 fu. 4]

5. Katika utumishi wetu au tunapotoa maelezo mikutanoni, kwa nini tunapaswa kujitahidi kutumia maneno yanayoonyesha mkazo, hisia, na yanayovutia? (Mt. 23:37, 38) [be uku. 163 fu. 3–uku. 164 fu. 1]

HOTUBA NA. 1

6. Kichwa kikuu cha hotuba ni nini, nacho kinawezaje kutusaidia kuchagua na kupanga habari kwa ajili ya hotuba? [be uku. 39 fu. 6–uku. 40 fu. 1]

7. (a) Kuwa safi kiroho kunamaanisha nini, na kwa nini usafi wa kiroho ni muhimu kuliko usafi wa aina nyingine? (b) Wakristo wanawezaje kukataa mambo yasiyo safi kiadili ambayo ni ya kawaida sana ulimwenguni? [w02 2/1 uku. 5-6]

8. Ni kanuni zipi zilizo muhimu zaidi? [w02 2/15 uku. 5 fu.1, 4, 6]

9. Hisia-mwenzi ni nini, na Yesu alionyeshaje sifa hiyo? [w02 4/15 uku. 25 fu. 4-5]

10. Andiko la Methali 11:11 linahusuje makutaniko ya watu wa Yehova? [w02 5/15 uku. 27 fu. 1-3]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. “Mti wa uzima” unaotajwa katika Mwanzo 2:9 unawakilisha nini?

12. Kwa nini mke wa Loti alipoteza uhai wake? (Mwa. 19:26) [w90 4/15 uku. 18 fu. 10]

13. Katika tamasha ya kiunabii ya Mwanzo sura ya 24, ni nani anayefananishwa na (a) Abrahamu, (b) Isaka, (c) Eliezeri, mtumishi wa Abrahamu (d) ngamia kumi, na (e) Rebeka?

14. Je, Mungu aliamuru kimbele mambo ambayo yangewapata Yakobo na Esau? (Mwa. 25:23)

15. Kwa nini jitihada yenye bidii ya Raheli, iliyobarikiwa na Yehova, ni mfano mzuri? (Mwa. 30:1-8) [w02 8/1 uku. 29-30]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki