Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/04 kur. 3-5
  • Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • ‘Lihubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Tangazeni Kotekote Sifa Bora za Yehova
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 2/04 kur. 3-5

Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za Yehova

1 Hakuna anayeweza kulinganishwa na Mungu wetu mkuu, Yehova! Daudi aliandika hivi: “Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi, Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea; hakuna wa kulinganishwa nawe.” (Zab. 40:5) Kazi za ajabu za Yehova zinatia ndani kuumbwa kwa ulimwengu, Ufalme wa Kimasihi, matendo ya fadhili zenye upendo kuelekea watu wake, na kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. (Zab. 17:7, 8; 139:14; Dan. 2:44; Mt. 24:14) Kumpenda Yehova na kuthamini yote ambayo amefanya hutuchochea kuwaambia wengine kumhusu. (Zab. 145:5-7) Katika miezi ya Machi, Aprili, na Mei, tutakuwa na nafasi ya kufanya hivyo kwa ukamili zaidi.

2 Ukiwa Painia-Msaidizi: Je, unaweza kupanga ratiba yako ili utumie muda wa saa 50 katika huduma kwa mwezi mmoja au zaidi katika miezi hii ya utendaji wa pekee? Hutajuta kwa sababu ya marekebisho yoyote utakayofanya katika ratiba yako. (Efe. 5:16) Wengi wameona kwamba kufanya upainia msaidizi huwasaidia waboreshe huduma yao. Wao huwa watulivu zaidi wanapohubiri nao hutumia Biblia zaidi. Kutumia wakati mwingi katika huduma hufanya iwe rahisi kuendelea kuwasaidia watu wowote wanaopendezwa, na wengine ambao hawakuwa na funzo la Biblia walianzisha funzo walipokuwa wakifanya upainia msaidizi. Upainia msaidizi ni utendaji wenye shangwe, kwa sababu tunajitoa kwa ajili ya wengine.—Mdo. 20:35.

3 Usiamue haraka kwamba hali zako hazikuruhusu kufanya upainia msaidizi. Mzee mmoja aliyefanya upainia msaidizi mwaka jana ana watoto wawili na kazi ya wakati wote. Ndugu huyo mwenye shughuli nyingi aliwezaje kutimiza hilo? Kwa kuwa yeye hufanya kazi katikati ya juma, alipanga kuhubiri kwa muda mrefu kwenye miisho-juma, akianza na mahubiri ya barabarani saa moja asubuhi siku za Jumamosi. Wengine katika kutaniko ambao pia walikuwa na hali kama hizo walifanya upainia, nao wakaungana mkono na kutiana moyo. Katika kutaniko lingine, dada mmoja mwenye umri wa miaka 99 aliamua kufanya upainia katika mwezi wa Mei baada ya binti yake kumwomba ajiunge naye. Wengine kutanikoni walimsaidia dada huyo mzee kwenda nyumba kwa nyumba na kwenye mafunzo ya Biblia kwa kusukuma kiti chake cha magurudumu. Pia alihubiri kwa kutumia simu, barabarani, na kuandika barua. Anasadiki kwamba hakufanya hivyo kwa nguvu zake mwenyewe bali tu kwa msaada wa Yehova.—Isa. 40:29-31.

4 Jaribu kutayarisha ratiba inayofaa hali zako. Ratiba zilizo katika toleo hili zinaweza kukusaidia. Je, wewe hufanya kazi wakati wote au huenda shuleni? Huenda ratiba inayohusisha hasa miisho-juma ikakufaa zaidi. Ikiwa una matatizo ya afya na nguvu zako hazikuruhusu kuhubiri kwa saa nyingi, ratiba inayohusisha kuhubiri kwa muda mfupi kila siku huenda ikakufaa zaidi. Ongea na wengine kuhusu tamaa yako ya kufanya upainia msaidizi. Labda wao pia wataweka mradi huo.

5 Njia Ambazo Vijana Wanaweza Kushiriki: Yehova hufurahi vijana wanapotangaza kazi zake za ajabu. (Zab. 71:17; Mt. 21:16) Ikiwa wewe ni kijana na umebatizwa, labda unaweza kufanya upainia msaidizi wakati wa likizo ya shule. Ikiwa huwezi kufanya upainia msaidizi, je, unaweza kuweka miradi hususa ya kuongeza utumishi wako na kuboresha huduma yako wakati wa miezi hiyo? Ikiwa unashiriki katika huduma pamoja na wazazi wako lakini wewe si mhubiri, sasa ungekuwa wakati unaofaa kujaribu kufikia mradi huo. Si lazima ufikiri kwamba unapaswa kuwa stadi wa kujibu maswali ya Biblia au kwamba unapaswa kujua mambo mengi kama watu wazima waliobatizwa. Je, unaelewa mafundisho ya msingi ya Biblia? Je, unashika viwango vya maadili vya Biblia? Je, unataka kutambuliwa kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova? Basi ongea na wazazi wako kuhusu jambo hilo. Wanaweza kupanga wazee waone kama unatimiza matakwa hayo.—Ona kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 98-99.

6 Kuwasaidia Wengine Kuhubiri: Wanafunzi wa Biblia wenye maendeleo wanaweza kustahili kuwa wahubiri katika miezi inayokuja ya utendaji wa pekee. Ikiwa una funzo la Biblia anayefanya maendeleo, tafuta msaada kutoka kwa mwangalizi wa funzo lako la kitabu au mwangalizi wa utumishi. Mmoja wao anaweza kuhudhuria au kujiunga nawe katika funzo hilo ili kuchanganua maendeleo ya mwanafunzi huyo. Mwanafunzi huyo akistahili na akiwa na tamaa ya kuwa mhubiri, mwangalizi-msimamizi anaweza kupanga wazee wawili wakutane na wewe na mwanafunzi huyo. (Ona Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1988, ukurasa wa 17.) Mwanafunzi anapokubaliwa, anza mara moja kumzoeza katika huduma.

7 Waangalizi wa funzo la kitabu wanapaswa kukazia uangalifu wahubiri wowote wasiotenda au wasio wa kawaida katika kikundi chao. Waalike waende pamoja nawe katika huduma. Ikiwa wamekuwa wasiotenda kwa muda mrefu, inafaa kwanza wazee wawili waongee nao ili waone ikiwa wanastahili. (Ona Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme, Novemba 2000.) Huenda bidii ya kutaniko katika miezi hiyo ya utendaji wa pekee itawachochea wawe wa kawaida tena katika huduma.

8 Jitayarishe Sasa kwa Ajili ya Utendaji Ulioongezeka: Wazee, anzeni sasa kuwachochea wahubiri kutanikoni wawe na hamu ya kufanya upainia msaidizi. Mnaweza kufanya hivyo kwa maelezo yenu yenye kujenga na mfano wenu mwema. (1 Pet. 5:3) Ni wangapi waliofanya upainia msaidizi wakati uliopita? Je, wengi zaidi wanaweza kufanya mwaka huu? Waangalizi wa funzo la kitabu na wasaidizi wao wanapaswa kutafuta njia ya kuwatia wote moyo katika kikundi ili waongeze utendaji wao. Waangalizi wa utumishi wanaweza kupanga mikutano ya ziada ya utumishi wa shambani. Julisheni kutaniko mapema mipango hiyo. Hakikisheni kwamba wahubiri wenye uzoefu wamegawiwa kuongoza na kwamba mikutano ya utumishi inaanza na kumalizika kwa wakati. (Ona Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme, Septemba 2001.) Pia mwangalizi wa utumishi anapaswa kupanga kuwe na eneo, magazeti, na vichapo vya kutosha.

9 Mwaka jana wazee wa kutaniko moja walianza mapema na kwa hamu kuwatia moyo wahubiri wafanye upainia msaidizi, huku baadhi yao wakifanya upainia msaidizi. Walipanga mikutano ya ziada ya utumishi wa shambani—mmoja saa 11:30 alfajiri kwa ajili ya mahubiri ya barabarani, mwingine saa 9 mchana kwa ajili ya wale wanaotoka shuleni, na wa tatu saa 12 jioni kwa ajili ya wale wanaotoka kazini. Zaidi ya hayo, mikutano mitatu ya utumishi wa shambani ilipangwa siku za Jumamosi. Kutaniko liliitikia kwa kuwa na wahubiri 66 waliojiandikisha kuwa mapainia-wasaidizi mwezi wa Aprili!

10 Kwa nini usitenge wakati katika funzo la familia lijalo ili kuweka miradi ya miezi ijayo? Kukiwa na ushirikiano na mipango mizuri, wengine au wote katika familia wanaweza kufanya upainia msaidizi. Ikiwa hilo haliwezekani, wekeni miradi ya kuongeza utendaji wenu kwa kurefusha vipindi vyenu vya kawaida vya kuhubiri au kwa kuhubiri katika pindi za ziada. Salini mkiwa familia kuhusu jambo hilo. Iweni na hakika kwamba Yehova atabariki jitihada zenu.—1 Yoh. 3:22.

11 Kazi ya Ajabu Zaidi ya Mungu: Upendo mkuu zaidi ambao Yehova alionyesha ni kutoa zawadi ya Mwana wake kwa ajili yetu. (1 Yoh. 4:9, 10) Dhabihu ya fidia ndiyo msingi halali wa kuwakomboa wanadamu kutokana na dhambi na kifo. (Rom. 3:23, 24) Damu ya Yesu iliyomwagwa ilihalalisha agano jipya, na kufanya iwezekane kwa wanadamu wasio wakamilifu kufanywa wana wa Mungu, wakiwa na tumaini la kutawala katika Ufalme wa mbinguni. (Yer. 31:31-34; Marko 14:24) Jambo muhimu zaidi ni kwamba maisha ya Yesu ya utii mkamilifu yalilitukuza jina la Yehova. (Kum. 32:4; Met. 27:11) Siku ya Jumapili, Aprili 4, baada ya jua kutua, Ukumbusho wa kifo cha Yesu utaadhimishwa ulimwenguni pote.

12 Mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana hutukuza kazi za ajabu za Yehova. Hotuba hutuchochea tuthamini yale ambayo Yehova alifanya kwa kutoa fidia. Watu wenye kupendezwa wataweza kuona kazi nyingine za ajabu za Mungu. Wataona umoja na upendo ambao Yehova amewafundisha watu wake kuonyesha. (Efe. 4:16, 22-24; Yak. 3:17, 18) Kuhudhuria pindi hiyo ya pekee kwaweza kuwa na kubadili sana maoni ya mtu, kwa hiyo tunataka watu wengi iwezekanavyo wahudhurie.—2 Kor. 5:14, 15.

13 Kuwaalika Wengine: Anza kwa kuandika orodha ya wale unaopanga kualika. Orodha yako inapaswa kutia ndani washiriki wa familia yako wasioamini, majirani, watu unaofahamu kazini au shuleni, wanafunzi wa Biblia wa sasa au wa zamani, na marudio yako yote. Waangalizi wa funzo la kitabu wanapaswa kutia katika orodha yao wahubiri wowote wasiotenda.

14 Tumia mialiko ya Ukumbusho iliyochapwa, na uandike vizuri saa na mahali pa Ukumbusho. Au unaweza kutumia mwaliko ulio kwenye ukurasa wa mwisho wa gazeti la Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 2004 au Amkeni! la Machi 22, 2004. Wakumbushe wote ulioalika kwa kuwatembelea au kuwapigia simu kadiri Aprili 4 inavyokaribia.

15 Kwenye Ukumbusho: Jaribu kufika mapema siku ya Ukumbusho. Wakaribishe wapya kwa kuwasalimu kwa uchangamfu. (Rom. 12:13) Una daraka la pekee kwa wale unaowaalika. Wasalimu kwa uchangamfu, na uwajulishe kwa wengine kutanikoni. Labda unaweza kuwasaidia wapate kiti karibu nawe. Na ikiwa kuna yeyote ambaye hana Biblia au kitabu cha wimbo, shiriki pamoja naye au upange mtu mwingine ashiriki pamoja naye. Baada ya mwadhimisho, uwe karibu ili kujibu maswali ambayo huenda wakawa nayo. Ikiwa wengine wamefika kwa mara ya kwanza, waulize kama wangependa kujifunza Neno la Mungu na makusudi yake. Jitolee kujifunza Biblia nyumbani pamoja nao.

16 Endelea Kuwasaidia Wale Watakaohudhuria: Majuma yanayofuata Ukumbusho, huenda wale waliohudhuria wakahitaji msaada. Wanatia ndani wale ambao hapo wakati mmoja walikuwa wakihudhuria mikutano kwa ukawaida lakini sasa hawashirikiani sana na kutaniko. Wazee watakuwa macho kuona kwamba watu hao hawapuuzwi, nao watajaribu kujua kwa nini waliacha kufanya maendeleo ya kiroho. Waonyeshe uharaka wa nyakati hizi. (1 Pet. 4:7) Wasaidie wote waone faida za kutii himizo la Kimaandiko la kukutana na watu wa Mungu kwa ukawaida.—Ebr. 10:24, 25.

17 Kazi za Yehova ni za ajabu sana kwetu hivi kwamba hatuwezi kuzielewa kikamili hata tukiishi milele. (Ayu. 42:2, 3; Mhu. 3:11) Kwa hiyo, hatutakosa kamwe mambo ya kumsifia. Katika majira haya ya Ukumbusho tunaweza kuonyesha uthamini kwa ajili ya kazi za ajabu za Yehova kwa kufanya jitihada ya pekee kupanua huduma yetu.

[Maswali ya Funzo]

1. Baadhi ya kazi za ajabu za Yehova unazothamini hasa ni gani?

2. Tunafaidikaje kibinafsi tunapofanya upainia msaidizi?

3. Wengine wamewezaje kufanya upainia msaidizi hata katika hali ngumu?

4. Ni mambo gani tunayoweza kufikiria tunapotayarisha ratiba ya kufanya upainia msaidizi?

5. Vijana wanaweza kuweka miradi gani katika miezi ya Machi, Aprili, na Mei?

6. Tunaweza kuwasaidiaje wanafunzi wa Biblia wawe wahubiri wa habari njema?

7. Wahubiri wasio wa kawaida au wasiotenda wanaweza kusaidiwaje?

8, 9. Wazee wanaweza kufanya nini ili kuchochea hamu kwa ajili ya utendaji wa pekee?

10. Familia zinaweza kujitayarishaje kuongeza utendaji wao?

11. (a) Dhabihu ya Kristo ilitimiza mambo gani ya ajabu? (b) Ukumbusho wa kwenu utafanywa saa ngapi na wapi?

12. Kuhudhuria mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana kunaweza kuwafaidi jinsi gani wanaopendezwa?

13, 14. Ni nani ambao tunapaswa kualika kwenye Ukumbusho, na jinsi gani?

15. Tunaweza kuwakaribishaje watu siku ya Ukumbusho?

16. Ni nini kinachoweza kufanywa ili kuwasaidia wale waliohudhuria wafanye maendeleo ya kiroho?

17. Kwa nini tunapaswa kuendelea kutangaza kazi za ajabu za Yehova?

[Chati katika ukurasa wa 5]

Je, Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi Ukitumia Mojawapo ya Ratiba Hizi?

Machi J2 J3* J4* J5* Al Ij J1 Mwezi Jumla

Kila Siku 2 1 1 1 1 1 5 51

Siku Mbili 0 5 0 5 0 0 0 50

Miisho-Juma Pekee 5 0 0 0 0 0 8 52

Miisho-Juma na

Siku Mbili za Juma 2 0 0 2 0 2 6 50

Aprili J2 J3 J4 J5 Al* Ij* J1 Mwezi Jumla

Kila Siku 2 1 1 1 1 1 5 50

Siku Mbili 0 0 0 0 5 5 0 50

Miisho-Juma Pekee 5 0 0 0 0 0 8 52

Miisho-Juma na

Siku Mbili za Juma 2 0 0 2 0 2 6 50

Mei J2* J3* J4 J5 Al Ij J1* Mwezi Jumla

Kila Siku 2 1 1 1 1 1 4 51

Siku Mbili 0 5 0 0 0 0 5 50

Miisho-Juma Pekee 3 0 0 0 0 0 7 50

Miisho-Juma na

Siku Mbili za Juma 2 0 0 2 0 2 5 51

*Tano katika mwezi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki